Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapandisha hadhi Zahanati ya Ihalula kuwa Kituo cha Afya baada ya kukidhi vigezo vyote kwa muda mrefu?

Supplementary Question 1

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu yaliyotolewa lakini bado kuna sintofahamu kuhusiana na status ya hiki Kituo. Nitaomba Mheshimiwa Waziri alifuatilie kwa karibu kwa sababu, wananchi wale wenye Bima wanashindwa kupata huduma kwa sababu wanasema officially hakijawa registered kwa hiyo kuna sintofahamu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini swali la pili, pamoja na Kituo hiki lakini Njombe tuna vituo vingine viwili vya Afya ambavyo havina vifaa ambavyo tumeahidiwa kwa muda mrefu, Kituo cha Makoo pamoja na Kituo cha Kifanya. Mawaziri wametembelea pale lakini tumepewa ahadi na hatuelewi. Sasa je, Serikali inaweza ikatoa kauli kuhusiana na hivyo vituo viwili? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Deodatus Phillip Mwanyika, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Zahanati ya Ihalula imekwisha pandishwa hadhi kuwa Kituo cha Afya na imekwishapewa namba ya usajili kama Kituo cha Afya. Kwa hivyo, naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba hiyo sintofahamu ilikuwa kwa sababu hatukuwa tumepata namba rasmi ya usajili kuwa kituo cha Afya ili National Health Insurance Fund waanze kuilipa moja kwa moja. Kwa hiyo, sasa limeshafanyika, lakini kama kuna changamoto nyingine zote tutakwenda kuzifuatilia kuhakikisha wananchi wetu wanapata huduma za ngazi ya Kituo cha Afya.

Mheshimiwa Spika, lakini pili, tumekuwa na ujenzi wa Vituo vingi vya Afya, vikiwemo Kituo cha Afya cha Makoo na Kifanya; na mpango wa Serikali ni kuendelea kutenga fedha za ununuzi wa Vifaa Tiba na Makoo ni moja ya vituo ambavyo Mheshimiwa Waziri wa Nchi alitembelea, aliahidi Vifaa Tiba na utaratibu unaendelea kuhakikisha Vifaa Tiba vinafika pale. Kwa hiyo, nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba suala hili linafanyiwa kazi. Ahsante. (Makofi)