Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Fakharia Shomar Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaondoa kabisa utaratibu wa kununua mazao kwa mkopo ambao unaendelea kutumiwa na baadhi ya Taasisi jambo ambalo linasababisha manung’uniko kwa Wakulima?

Supplementary Question 1

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS: Mheshimiwa Spika, ahsante. Nimepokea maelezo yake aliyonipa katika swali langu, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa, Serikali inafahamu kwamba, suala hili la mikopo linaathiri sana wakulima wetu. Je, Serikali haioni kwamba, sasa ni wakati wa kuwafungulia milango wakulima kuweza kuuza mazao yao wao wenyewe ikiwa ndani au nje ya nchi ili kuweza kunusuru mazao yao kuharibika? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa, Serikali inawajali wakulima na inawathamini. Je, kwa nini Wizara haitengi bajeti maalum kwa ajili ya kununua mazao ya wakulima yale yanayorundikana majumbani ambayo yanakosa soko ili kuweza kuwasaidia wakulima wao kunusuru nguvu zao na maharibiko ya mazao yao? Ahsante. (Makofi)

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Fakharia, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, suala la kufungua milango Serikali imefungua milango kwa mkulima mfanyabiashara yeyote wa mazao kuuza popote pale duniani na hatazuiliwa na mtu yeyote. Wizara ya Kilimo tunatoa vibali vya export bure kwa ajili ya kuuza mazao ndani na nje ya nchi na hakuna mfanyabiashara wala mkulima yeyote atakayezuiliwa kuuza popote anapopata soko.

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la kuongeza bajeti kwa ajili ya kununua mazao ya wakulima, sisi kama Wizara kama utakumbuka mpaka sasa hivi Serikali imekuwa ikichukua hatua mbalimbali za kuongeza fedha za kununua mazao pale ambapo linapojitokeza tatizo na Serikali hununua mazao kwa sababu kubwa mbili.

Mheshimiwa Spika, moja kwa ajili ya kuhifadhi; lakini mbili kwa ajili ya ku-stimulate soko pale ambapo mazao ya wakulima yanaanguka bei. Na utakumbuka hapa Bunge lako Tukufu lilileta hoja na Wabunge waliibuka na hoja ya ku- rescue zao la mahindi na Serikali na Mheshimiwa Rais akaidhinisha matumizi ya shilingi bilioni 100 ambazo tumeenda kununulia mazao na mpaka sasa tunanunua mahindi kwa shilingi 500 kupitia taasisi yetu ya NFRA na ununuzi unaendelea. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hatua ya kununua mazao tutaendelea kuifanya kadri ambavyo bajeti itakuwa inaruhusu na Bunge lako Tukufu likitupitishia fedha sisi tutaenda kutekeleza field. (Makofi)