Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza: - Je, Serikali imeweka vivutio gani maalum ili kuwavutia wasafirishaji kutumia Bandari ya Mtwara kusafirisha mizigo ya nchi za Msumbiji, Malawi na Zambia?

Supplementary Question 1

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Spika nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza. Ili Bandari ya Mtwara iweze kufanya kazi kwa ufanisi na kuweza kushughulikia mzigo mkubwa inategemea ujenzi wa reli kutoka Mtwara hadi Mbambabay.

Je, ni nini kauli ya Serikali kuhusu radi huu?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, baada ya upanuzi mkubwa wa Bandari ya Mtwara, bandari hii sasa inakabiliwa na changamoto ya vitendea kazi vya kisasa:

Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka vitendea kazi vya kisasa katika Bandari yetu ya Mtwara?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI YA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Abdallah Chikota kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Mheshimiwa Mbunge anataka kujua mpango wa Serikali kujenga reli ya kutoka Mtwara kwenda Mbambabay; huu mpango ndiyo unaosimamiwa na watu wa TPA wanaufanyia kazi. Tunajua umuhimu wa eneo hilo, Mheshimiwa Mbunge atupe muda, hili jambo tukalifanyia kazi mapema iwezekanavyo.

Mheshimiwa Spika, swali la pili anataka kujua kama kuna mpango wa kununua vitendea kazi. Mpango mkakati sasa wa TPA wa kuweza kuboresha bandari zetu na hasa eneo la Mtwara, ni mpango ambao upo katika mpango kabambe wa awamu ya pili na fedha zinaendelea kutafutwa na tumeshawaelekeza watu wa TPA waje na mpango mkakati wa maandishi twende kuboresha maeneo haya na bandari zote muhimu kimkakati kutokana na kupatikana fedha.

Mheshimiwa Mbunge tunaendeleza ushirikiano, jambo hili limepokelewa na Serikali na Kamati ya Bunge ya Bajeti imetoa maelekezo, vile vile na Kamati ya Miundombinu na tumelipa uzito unaostahili.

Mheshimiwa Spika, ahsante.