Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Amour Khamis Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbe

Primary Question

MHE. AMOUR KHAMIS MBAROUK aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha vikundi vya wananchi ili kuhamasisha uhifadhi wa mazingira hasa katika fukwe za Bahari ya Hindi?

Supplementary Question 1

MHE. AMOUR K. MBAROUK: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba niulize maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza sijajua kwa nini mikoa ya Zanzibar haijaorodheshwa hapa, lakini pia sijajua Serikali inawezeshaje makundi haya 157 ili kumudu kazi hii ngumu sana?

Mheshimiwa Spika, swali la pili: Kwa kuwa zipo dini ambazo zinajinasibu na kujitahidi kusema kwamba kila kitu kitakachotokea duniani kwenye vitabu vyao wameeleza: Je, Serikali imeshaona umuhimu wa kuwashauri viongozi wa dini katika kuondoa tatizo hilo ambalo ni gumu sana hata pale Zanzibar ambapo visiwa ndiyo vinaondoka?

Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA): Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Khamis Amour Mbarouk kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kabla ya kujibu naomba nichukue nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Amour kwa juhudi yake ya kufuatilia masuala ya mazingira kule visiwani Zanzibar. Suala lake la kwanza ni kweli kwamba ipo haja ya kuhamasisha vikundi mbalimbali katika sehemu zote za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; na tayari tumewasiliana na wenzetu, Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais kule Zanzibar kwa ajili ya kuhamasisha wananchi wa Kanda za Pwani ili kusudi kuanzisha vikundi kama hivi kwa lengo la kutunza mazingira. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili, kwa kweli tunachukua hoja yake hii kwamba upo umuhimu wa kushirikisha taasisi za dini. Tumeanza kuwaita viongozi wa dini na kuzungumza nao kuhusu suala la utunzaji wa mazingira. Kwa mwelekeo ambao tunakwenda nao sasa, ni lazima tuzishirikishe taasisi za dini kuhusu suala la utunzaji wa mazingira, kwa sababu wao kwa asilimia kubwa wanakaa na wananchi. Kwa hiyo, tutawaomba viongozi wa Makanisa ama Misikiti iwe ni sehemu ya mahubiri yao ya utunzaji wa mazingira ili mazingira yetu yawe salama kwa maslahi ya Taifa letu. Ahsante. (Makofi)

Name

Asya Mwadini Mohammed

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AMOUR KHAMIS MBAROUK aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha vikundi vya wananchi ili kuhamasisha uhifadhi wa mazingira hasa katika fukwe za Bahari ya Hindi?

Supplementary Question 2

MHE. ASYA MWADINI MOHAMMED: Mheshimiwa Spika nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Huko nje hasa katika ukanda wa bahari, sisi tunatokea kwenye visiwa, hali ni mbaya sana kuhusu masuala mazima ya mazingira. Wakisema kwamba waanzishe vikundi, kwamba vikundi ndiyo viwe vinasimamia mazingira katika kukusanya taka, bado elimu haijafikiwa. Yaani wananchi walio wengi wanazalisha taka, lakini hawana taaluma ya utunzaji wa hizo taka hasa kwenye upande wa mazingira. Je, nini kauli ya Serikali juu ya usimamizi wa masuala mazima ya utoaji wa elimu ya usimamizi wa mazingira? (Makofi)

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA): Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Asya, ni kweli kabisa anachokisema Mheshimiwa Mbunge kwamba elimu bado ni ndogo, lakini tumieandaa programu maalumu za kutoa taaluma kwa wanavikundi na wananchi wa kawaida.

Mheshimiwa Spika, jibu langu la pili la nyongeza nilisema kwamba tutaenda mpaka kwa taasisi za dini ili suala la taaluma liwe na wigo mpana. Kwa hiyo, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba taaluma hiyo ya utunzaji wa mazingira itafika nchini kote.