Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA K.n.y. MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka Watumishi pamoja na vitendea kazi katika Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; katika Jimbo la Manyoni Mashariki hususan Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni, tuna upungufu mkubwa sana wa Watendaji wa Vijiji na tayari tulishapeleka maombi ya kupata kibali cha kuajiri Watendaji wa Vijiji na Watendaji wa Kata. Je, ni lini Serikali itatupatia kibali sasa cha kuwaajiri Watendaji wa Vijiji?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; katika Jimbo la Manyoni Mashariki tuna kilimo kikubwa sana cha korosho kwa kutumia block farming. Je, Serikali haioni sasa kuna umuhimu wa kusaidia kupeleka wataalam wa kilimo ili kuchochea uwekezaji huo? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwanza nichukue nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Dkt. Pius Chaya Mbunge wa Manyoni Mashariki, lakini pia Mheshimiwa Massare Mbunge wa Manyoni Magharibi na Mheshimiwa Aysharose Ndogholi Mattembe kwa kazi kubwa sana wanazozifanya kwa pamoja, kuhakikisha wananchi wa Manyoni na Singida kwa ujumla wanapata miradi ya maendeleo kwa ustawi wa jamii.

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba tuna changamoto ya upungufu ya Watendaji wa Vijiji na Kata katika halmashauri zetu zilizo nyingi. Serikali inaitambua changamoto hii na tathimini na mpango mkakati unaendelea kuandaliwa, hatua nzuri ili tuone namna gani tunakwenda kujaza nafasi za Watendaji wa Vijiji na Kata katika maeneo yetu ili waweze kusimamia kwa ufanisi zaidi shughuli za maendeleo. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inaendelea kulifanyia kazi hilo na litapatiwa ufumbuzi kwa awamu na kwa hatua stahiki.

Mheshimiwa Spika, ni kweli tunahitaji wataalam wa kilimo lakini pia wa kada mbalimbali. Nalo pia linafanyiwa kazi na kwa kadri ya uwezo wa Serikali na upatikanaji wa wataalam hao tutaendelea kuajiri ili wakafanye kazi hizo. Nakushukuru sana.