Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Yahya Ally Mhata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. ALLY Y. MHATA aliuliza: - Je Serikali ina mpango gani wa kuyatumia majengo yaliyoachwa na Kampuni ya Ujenzi ya China yaliyopo Kijiji cha Maneme yatumike kama Chuo cha Ufundi (VETA)?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY Y. MHATA: Mheshimiwa Spika, kwanza naishukuru sana Serikali kwa majibu mazuri kuhusiana na swali hili, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, Kijiji cha Maneme ambapo ndipo yalipo majengo haya kilishaandika barua kukabidhi majengo haya kwa Serikali. Mimi kama mwakilishi wao niliwasilisha barua yao ya kukabidhi hili eneo kwa Wizara. Kwa hiyo, nataka kupata commitment ya Serikali. Ni lini watendaji hawa wa Serikali watakuja ndani ya wilaya yangu ili kuyahakiki majengo haya? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa suala hili la ujenzi wa Vyuo vya VETA liko ndani ya Ilani ya Chama Cha Mapinduzi na sisi wananchi wa Jimbo la Nanyumbu tunayo majengo tayari, je, Serikali haioni haja kwa Mwaka ujao wa Fedha majengo haya yakatumika ili wananchi wa jimbo langu wakanufaika?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mhata, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyojibu kwenye majibu yangu ya msingi kwamba tayari timu yangu ya wataalam kutoka Wizara itakwenda eneo hili. Mheshimiwa Mbunge anataka kujua lini, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwa vile tuko hapa Bungeni na Makao Makuu ya VETA yako hapa Dodoma, nimwombe tu Mheshimiwa Mbunge mara baada ya kipindi hiki tuweze kuonana, twende wote kwa Mkurugenzi wa VETA pale ofisini, twende tukaipange vizuri ili tujue wataalam wetu wale lini watakwenda kwenye eneo hili la kuweza kufanya tathmini ya pamoja na kujua kitu gani cha kufanya kule Nanyumbu.

Mheshimiwa Spika, kwenye eneo la pili, kwamba majengo yapo, kuna baadhi ya miundombinu itahitaji kuongezwa; naomba hili tulichukue tuweze kuangalia katika bajeti ijayo iwapo kama itaturuhusu kuweza kuingiza bajeti ya kuongeza miundombinu katika eneo hili. Wakati tathmini hii ikishafanyika itatupa dira ya wapi tunakoelekea, mahitaji gani yatakayohitajika na ni commitment gani itahitajika ya kifedha kuweza kwenda kuongeza miundombinu kwenye eneo hili. Kwa hiyo hili tunaomba tulichukue tutaenda kulifanyia kazi na baada ya tathmini yetu hiyo tutakutana na Mheshimiwa Mbunge kumwonesha kitu gani tunachoweza kukifanya kwenye eneo hili. Ahsante sana.

Name

Godwin Emmanuel Kunambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. ALLY Y. MHATA aliuliza: - Je Serikali ina mpango gani wa kuyatumia majengo yaliyoachwa na Kampuni ya Ujenzi ya China yaliyopo Kijiji cha Maneme yatumike kama Chuo cha Ufundi (VETA)?

Supplementary Question 2

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa changamoto ya wananchi wa Nanyumbu inafanana kabisa na changamoto ya wananchi wa Jimbo la Mlimba pale Kata ya Mchombe.

Mheshimiwa Spika, Kata ya Mchombe tayari tuna majengo pale. Huko awali kulikuwa na kituo kidogo cha VETA na vijana walikuwa wakijifunza pale, sasa kituo kile kilifungwa na majengo yale hayatumiki.

Je, Wizara haioni umuhimu inavyoenda kufanya tathmnini Nanyumbu hiyo timu ya wataalamu ikafanya pia tathmini pale Mlimba Mchombe, kwa sababu majengo ya Serikali yanaendelea kuharibika tu?

Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika ahsante, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Kunambi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama ulivyoeleza kwenye utangulizi wako Mheshimiwa Kunambi nadhani wakati tunaunda hii timu kwa vile barabara ni hiyo hiyo moja ya kwenda Nanyumbu nadhani ni lazima tupite Morogoro, tutaona busara itakavyotutuma nadhani timu hii itapita katika eneo hilo. Ahsante sana.