Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Taska Restituta Mbogo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka Umeme wa Grid ya Taifa katika Mkoa wa Katavi?

Supplementary Question 1

MHE. TASKA R. MBOGO: Mheshimiwa Spika ahsante, kwa kunipa nafasi kwa kuuliza maswali ya nyongeza. Pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri kuhusu umeme ninayo maswali mawili ya nyongeza kwa Mkoa wa Katavi.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza wananchi wa Mkoa wa Katavi wanahitaji umeme wa gridi kwa haraka ili waweze kujenga viwanda, lakini pia ili waweze kufanya biashara zao mbali mbali zinazotumia umeme. Kumekuwepo na kusuasua kwa mradi huu wa umeme wa gridi na ujenzi wake unakwenda taratibu kwa sababu ya ufinyu wa pesa zainazotolewa Serikalini kwenda TANESCO: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuongeza bajeti ya TANESCO ili waweze kujenga miundombinu ya umeme kwa Mkoani Katavi? (Makofi)

Swali la pili; umeme uliopo sasa hivi Mkoa wa Katavi hautoshelezi kwa sababu kumeuwa na usambazaji wa umeme wa REA, hivyo watumiaji wa umeme ni wengi mkoani Katavi. Swali langu na ombi langu kwa Serikali: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kutupunguzia muda wa ukamilishaji wa ujenzi wa umeme wa gridi badala ya kuwa 2023 uwe 2022? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Taska Restituta Mbogo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ya Awamu ya Sita imejipambanua kuwa na uwezo wa kutekeleza miradi ambayo imeianzisha na ile ambayo imeikuta ikiwa inaendelea, nasi tuna uhakika kwamba fedha iliyopo TANESCO itaendelea kutosha na pale ambapo watapungukiwa Serikali itaongeza. Katika bajeti ambayo Bunge lako limepitisha jusi, takribani shilingi bilioni 35 zilitengwa kwa ajili ya kuendelea na hii kazi ya ujenzi wa hiyo njia ya msongo wa kilovolti 132 kutoka Tabora kwenda Mpanda.

Mheshimiwa Spika, tunaamini fedha hizo zitatosha na kwa kadri itakavyohitajika kutoka kwa wataalamu basi Serikali itaongeza pesa hizo kwa sababu inazo.

Mheshimiwa Spika, kwenye swali la pili, kwa kuwa wenzetu wa Katavi hawajafikiwa na gridi; na gridi kwa mujibu wa ratiba ya TANESCO iliyowekwa kwa mchanganuo ule wa kitaalamu wa kwamba tuanze kupembua njia ya kupitisha umeme tulipe fidia, tujenge majengo tuchukue na hatua nyengine; naomba Bunge lako Tukufu, liruhusu na kuielekeza Wizara iende ikakae na kuona kama muda huu unaweza ukaminywa kwa kuzingatia matakwa ya kitaalamu na bajeti tuliyojipangia ili wenzetu wa Katavi waweze kupata gridi hii kwa wakati.

Mheshimiwa Spika, niongeze kwamba Mkoa wa Katavi unatumia umeme karibia Megawati 1 na kilowati kama 200, tutaenda kuona namna ambavyo tunaweza tukaongeza mashine na mitambo ya kuweza kufua umeme zaidi katika eneo hilo katika kipindi hiki ambacho bado tunaendelea na utengenezaji wa miundombinu yetu ya kufikisha gridi katika Mkoa wetu wa Katavi. (Makofi)

Name

Tabasamu Hamisi Hussein Mwagao

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sengerema

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka Umeme wa Grid ya Taifa katika Mkoa wa Katavi?

Supplementary Question 2

MHE. TABASAM H. MWAGAO: Mheshimiwa Spika, nami naomba kumwuliza Mheshimiwa Naibu Waziri wa Nishati, Sengerema imekuwa inakatika umeme mara 30 kwa siku na tayari umeme umeshatengenezwa katika eneo letu la kupoozea umeme pale Pomvu Geita, kwa nini Sengerema msituunganishe katika laini ya Geita ili tukaacha kukatikiwa umeme kwa mfumo huu wa kukatika mara 10 kwa siku?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Tabasamu, Mbunge wa Sengerema kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpe pole Mheshimiwa Mbunge kwa adha ambayo wananchi wake wamekuwa wakiipata, lakini kama nilivyosema tangu awali, Serikali imepambanua kwa muundo na msukumo mpya uliopo, haya matatio makubwa yataaenda kupunguzwa katika maeneo yetu mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, kukatika umeme kama nilivyosema, kunaweza kusababishwa na laini ya umeme kuwa ndefu au mazingira mengine kwa na vitu hatarishi kama maeneo ambayo ni oevu na tunafahamu maeneo mengi ya kanda ya ziwa ni oevu, kwa hiyo, nguzo zetu zimekuwa zikianguka au pengine laini kuwa na watumiaji wengi na pengine ikazidiwa. Kwa hiyo, mambo yote hayo yanachukuliwa maanani na kuangalia namna gani ambavyo tutaweza kurekebisha katika maeneo mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, namwomba Mheshimiwa Tabasamu aniruhusu baada ya hapa nikae nae niongee naye nichukue eneo lake kazi, ili nikakae na wataalamu tuweze kujua tatizo hasa linasababishwa na nini katika sababu mbalimbali. Maana inawezekana ukajenga kituo cha kupooza umeme katika eneo hilo, lakini bado umeme ukaendelea ukakatika kwa sababu tatizo halikuwa kituo cha umeme, pengine ilikuwa tatizo lingine, tukibaini tatizo lenyewe tutaweza kulifanyia kazi kwa usahihi.