Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUBIRA K. MGALU K.n.y. MHE. TWAHA A. MPEMBENWE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza Ujenzi wa barabara ya Nyamisati hadi Bungu katika Jimbo la Kibiti?

Supplementary Question 1

MHE. SUBIRA K. MGALU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza nimshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri na Serikali kwa majibu mazuri yenye kutia matumaini ya wakazi wa Jimbo la Kibiti. Hususani walio jirani na barabara ya Bungu Nyamisati kwa kuwa Serikali imetenga fedha, ya kuanza upembuzi yakinifu na hizi milioni 700 kwa ajili ya matengenezo ili ipitike muda wote.

Mheshimiwa Spika naomba sasa niulize swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa katika hilo Jimbo la Kibiti kuna barabara muhimu ya Kibiti Dimani Mloka ambapo pia, magari yanayoelekea kwenye mradi muhimu wa kimkakati wa ujenzi wa Bwawa la Mwalimu Nyerere wanaitumia.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza upembuzi yakinifu kwa kuwa barabara hii pia ipo kwenye ilani ya uchaguzi ya mwaka 2025, kwa ajili ya ujenzi wa kiwango cha lami? Ili kuwezesha ipitike muda wote kuelekea kwenye Mradi wa Bwawa la Mwalimu Nyerere. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Subira Mgalu Mbunge wa Viti Maalum Pwani kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli barabara aliyotaja ni kati ya barabara ambazo zinafika kwenye mradi wetu wa kimkakati na imeainishwa kwenye ilani ya Chama cha Mapinduzi kama alivyosema ambayo ni ya 2020 – 2025. Naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara zote ambazo zimeainishwa katika ilani haziwezi zote zikatekelezwa kwa mwaka mmoja. Lakini nimuhakikishie kwamba zipo kwenye mpango na zitafanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina, kama ilivyoainishwa kwenye ilani katika kipindi hiki cha miaka mitano. Ahsante.