Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. DAVID M. KIHENZILE aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kupunguza Kodi kwenye Vifaa vya Mchezo ili Sekta ya Michezo iweze kustawi?

Supplementary Question 1

MHE. DAVID M. KIHENZILE: Mheshimiwa Spika, sote tunafahamu dhamira ya Rais wetu aliyoionesha kwenye eneo la michezo, na tarehe 15 Juni, 2021 alipokuwa anazungumza na vijana wa nchi hii pale Mwanza alizungumzia eneo hili la msamaha wa kodi. Na katika maelezo ya Mheshimiwa Naibu Waziri amesema wataanza kufanya practice kwenye upande wa majijii na halmashauri za manispaa, na wakifanya vizuri watahamia kwenye Wilaya.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza; ina maana wanamaanisha kwa mfano kama Dodoma Mjini wakipewa hayo majaribio waki under perform basi ina maana Kongwa hawatapewa kwenye phase two.

Mheshimiwa Spika, hii nadhani si sawa. Ni vyema kama wanakwenda kufanya majaribio wafanye kote kwenye halmashauri za manispaa, majiji na kule kwingine.

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Ili kurahisisha utekelezaji wa jambo hili Je, Mheshimiwa Naibu Waziri na Serikali kwa ujumla haioni sasa umefika wakati wa kuanzisha wakala wa vifaa vya michezo nchini ili kurahisisha upatikanaji wa vifaa vya michezo kirahisi kuanzia kwenye shule zetu hata kwa Wabunge wenyewe ambao kimsingi kila mwaka wamekuwa wakiagiza vifaa vya michezo kwa wananchi wao? (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mwakiposa Mbunge wa Mufindi Kusini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, dhamira ya Serikali kuanza na majiji na halmashauri hayakuwa na maana ya kuangalia mapungufu ambayo yanaweza kusababisha maeneo mengine yasipate sipokuwa yalikuwa yana lengo la kuangalia mapungufu ili yatakapopelekwa maeneo mengine mapungufu yale yasijitokeze. Kwa mfano katika matumizi ya nyasi hizi bandia yamekuwa yakitumika katika shughuli mbalimbali wakati mwingine unaweza ukaenda hata kwenye bar ukakuta hizi nyasi bandia zipo.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo nikuhakikishie kwamba Serikali inadhibiti matumizi mabaya ya fursa hii njema iliyowekwa na kwa dhamira njema ya Serikali ni vyema tungeanza hatua kwa kwa hatua. Kwa hiyo elimu ambayo tumeipata katika utekelezaji katika awamu ya halmashauri na majiji itatusaidia tunapopanua wigo katika maeneo mengine mengi zaidi kuweza kufahamu ni mapungufu yapi na tukayoweza kuyadhibiti kirahisi ili kuepuka madhara na hasara kwa Serikali; hiyo ndiyo iliyokuwa dhamira. Malengo ni kuhakikisha kwamba tunasambaza huduma hizi katika maeneo yote nchini hatua kwa hatua na awamu kwa awamu.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na wazo lake la pili, ni jambo jema sana na Mheshimiwa Mwakiposa amekuwa kwakweli ni mpambanaji sana wa suala hili. Mara nyingi amekuwa akija akituulizia kuhusiana na utekelezaji, na kwamba angependa kuona mabadiliko na maboresho makubwa katika eneo hili. Kwa hiyo kuhusiana na hoja hii ya pili nadhani ni hoja ya msingi. Mheshimiwa Waziri wa Michezo na Mheshimiwa Naibu wake hapa wapo, wamesikia na ninahakika watalitafakari na kama wataona kuna tija basi watalitekeleza. Hili lipo katika Wizara ya Michezo na Serikali hapa ipo, tumelisikia.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DAVID M. KIHENZILE aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kupunguza Kodi kwenye Vifaa vya Mchezo ili Sekta ya Michezo iweze kustawi?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwa kuwa michezo ni afya na kwa sasa dunia nzima ikiwemo Tanzania tunakabiliwa na hili janga la corona na hivyo tunawahamasisha wananchi wetu waweze kufanya mazoezi ikiwepo kushiriki michezo na vifaa vya michezo ni ghali sana. Na kwa kuwa michezo ni ajira kama Taifa tunahitaji kuwekeza kwenye michezo kuanzia kwenye makuzi ya awali ya watoto wetu ili baadaye waje kuwa na vipaji mbalimbali kwenye soka, riadha, basket na mengine; lakini zaidi michezo ni moja ya sekta ambayo inatangaza nchi yetu na kutangaza utalii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, je, Serikali haioni kwamba ni vyema sasa iweze kufanya exemption kwa vifaa vyote vya michezo ili viweze kuwa na bei nafuu na watanzania wengi waweze kununua na kujiendeleza kimichezo?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Esther Matiko Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, suala la exemption si jambo ambalo linaweza likatolewa kauli Bungeni, linahitaji mambo mengi ikiwemo uchambuzi wa kina wa kitaalam juu ya faida na hasara zake. Sisemi kwamba vifaa vya michezo havina faida lakini ni jambo ambalo siwezi ukalizungumza hapa. Niseme tu kwamba tumelichukua tuone jinsi gani litakavyokuwa linakidhi mahitaji na vigezo kwa wakati husika basi tutalifanyia kazi.