Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Priscus Jacob Tarimo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza: - Je, ni nini hatma ya biashara ya maduka ya kubadilisha fedha (Bureau de Change) yaliyofungwa na Serikali?

Supplementary Question 1

MHE. PRISCUS J. TARIMO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyogeza.

Kwa kuwa vigezo vipya vya kufungua maduka vimekuwa vigumu kwa wafanyabiashara wengi, ikiwa ni pamoja na uoga wa kupoteza fedha kama ilivyotokea mwanzo, Serikali ina mpango gani wa kuweka masharti ambayo ni rafiki ili wafanyabiashara wengi zaidi wafungue biashara hizo kwa sababu maeneo ya mpakani/mikoa hii ya mpakani kumeshaanza kuwepo kwa black market ambapo wale wanaobadilisha fedha wanabadilisha kwa bei ya chini sana? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; maduka yale yaliyofungwa fedha taslimu zilichukuliwa na baadhi ya wafanyabiashara zilichukuliwa mali zao nyingi ikiwepo hati za viwanja na nyumba, hati za magari kwa maana ya kadi za magari na hawajarejeshewa.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni nini hatma ya watu hawa ambao wamefungwa mikono na mali zao zimeshikiliwa na Serikali? (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Tarimo Mbunge wa Moshi Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge amesema kwamba vigezo vilivyowekwa ni vigumu, lakini bahati mbaya hakuainisha vigezo hivyo ni vipi vigumu; kwasababu imani yangu ni kwamba pengine angetusaidia kutuambia ni kipi kigumu tungeweza kukifanyia kazi. Hata hivyo kwa ujumla vigezo vilivyowekwa mpaka sasa hivi tunadhani tumeviwekwa kwa kuzingatia maslahi ya nchi pamoja na maslahi ya Serikali. Ingawa bado kuna mwanya wa kuweza kuviangalia kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge amesema, lakini kwa uelewa wangu vigezo hivyo kwa kweli si vingi sana. Labda kigezo kimoja ambacho kimekuwa kikilalamikiwa sana ni kigezo cha kiwango cha mtaji kutoka shilingi milioni 300 kuja bilioni moja.

Mheshimiwa Spika, mantiki ya kuweka kigezo hiki ilikuwa ni nia njema tu ya Serikali kuhakikisha kwamba hawa wafanyabiashara wa maduka haya ya kubadilisha fedha wanatumia fedha zao wenyewe kuendesha biashara. Kwasababu wakati ambapo umefanyika utafiti kupitia forensic audit iliyofanywa iligundulika kwamba wengi wafayabiashara wa biashara hizi za kigeni walikuwa wanazungusha fedha isiyokuwa yao, kwa hiyo, hiyo ndio ikawa mantiki ya kuweka kiwango hicho na hivyo nadhani ndiyo malalamiko mengi makubwa.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo Mheshimiwa Mbuge labda pengine angetusaidia kwa wakati wake kuweza kuainisha vigezo. Kama kuna vigezo ambavyo tunaona kwamba vinahitaji kuangaliwa basi tutaviangalia.

Mheshimiwa Spika, lakini swali lake lingine ambalo ameuliza anazungumzia kuhusiana na hatma ya vifaa vilivyochukuliwa. Ni kwamba baada ya hatua ambazo zimechukuliwa kujitokeza wafanyabiashara hawa waliitwa ili kufanya majadiliano na mamlaka husika; na baada ya majadilliano kumalizika walitakiwa wale ambao walipaswa kulipa walipe, wale ambao walitakiwa kwenda kuchukua vifaa vyao waende wakavichukue.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo nitoe wito, kama kuna wafanyabiashara ambao bado hawajachukua vifaa vyao na wanastahili kwenda kuvichukua vifaa vyao waende wakachukue vifaa vyao, na hakuna sababu yoyote ambayo Serikali inaweza kukaa na mali ya mtu bila sababu ya msingi. Kwa hiyo niendelee kuwasisistiza kwamba kauli rasmi ya Serikali ni kwamba kama ambavyo majadiliano yalifanyika wakaelezwa wale ambao wanastahili kwenda kuchukua au wanahitaji kuvichukua basi waende wakavichukue. Kama kuna mapungufu yoyote basi tuletewe hizo taarifa ili tuweze kuzifanyika kazi.

Name

Kilumbe Shabani Ng'enda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Mjini

Primary Question

MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza: - Je, ni nini hatma ya biashara ya maduka ya kubadilisha fedha (Bureau de Change) yaliyofungwa na Serikali?

Supplementary Question 2

MHE. KILUMBE S. NG’ENDA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, nilitaka kujua kama Serikali kupitia Wizara ya Fedha na Benki Kuu waliamua kufunga maduka ya fedha za kigeni kwa sababu yalikuwa hayafuati taratibu, na sasa zipo financial institution nyingi mjini humu ambazo zinakopesha kwa riba ya juu na kuumiza walimu na watumishi wengine wa umma. Hivi Serikali inapata kigugumizi gani kuzifunga hizi ambazo zinatesa wananchi na badala yake inakwenda kufunga maduka ya fedha za kigeni ambayo yalikuwa hayalalamikiwi na wananchi?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kilumbe Ng’enda, Mbunge wa Kigoma Mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kilichofanyika ilikuwa ni kuzifuta leseni kwa wale ambao walibainika kuwa wamekiuka taratibu; na hii ipo kwa mujibu wa sheria pamoja na regulation ambazo tumetunga za mabadiliko ya fedha za kigeni, wanaita Foreign Exchange Act, kwa hiyo hii ilichofanyika imefanyika kwa mujibu wa sheria.

Sasa kuhusiana na kwamba kwanini kuna taasisi nyingine ambazo zinaumiza wananchi wa riba kubwa, jana nilimpongeza sana Mheshimiwa Kilumbe hapa, kwasababu nilisema kwamba kama kuna Wabunge ambazo walishiriki katika mjadala wa Bunge la Bajeti lililopita, kuzungumza kwa uchungu na hisia kazi juu ya baadhi ya taasisi ambazo zimekuwa zikinyanyasa wananchi kwa kuwakopesha kwa riba kubwa bila msingi yeye alikuwa ni mmojawapo. Nikasema kwamba kwa kusikia kilio hicho hicho kwa Waheshimiwa Wabunge Mheshimiwa hakuchelewa kwa kutoa maelezo ili jambo hilo lifanyiwe kazi.

Mheshimiwa Spika, na nimewahakikishia juzi na jana wakati najibu maswali kwamba kwanza niwapongeze BOT kwa kutekeleza maelekezo ya Mheshimiwa Rais, sasa hivi mchakato huu umeshaanza. Kwa hiyo ni matarajio yangu sasa kile kilio cha Waheshimiwa Wabunge akiwepo Mheshimiwa Kilumbe cha kupunguza riba sasa kimepatiwa dawa. Kwa hiyo hoja hizo mbili zote zinachukuliwa hatua kwa utaratibu wake kulingana na sheria na taratibu za nchi yetu.

Name

Christopher Olonyokie Ole-Sendeka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Simanjiro

Primary Question

MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza: - Je, ni nini hatma ya biashara ya maduka ya kubadilisha fedha (Bureau de Change) yaliyofungwa na Serikali?

Supplementary Question 3

MHE. CHRISTOPHER O. OLE-SENDEKA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Kwa kuwa Serikali ya Awamu ya Sita imetangaza nia yake ya kuendelea kurejesha imani ya wafanyabiashara na kujenga mahusiano mazuri kati ya Serikali na wafanyabiashara. Na kwa kuwa sasa hivi Serikali inaendelea kujadiliana na watu hawa wa maduka ya kubadilisha fedha.

Je, Serikali itakuwa tayari kuweka bayana kiasi cha fedha kilichokusanya wakati wa operation hiyo, na kiasi cha fedha ambazo zitakuwa zimerudishwa kwa wale wasio na hatia na sababu zitakazopelekea wale ambao fedha zao zitachukuliwa na kwamba zitakuwa zimechukuliwa kwa misingi ipi? Naliweka hili na naomba swali langu lijibiwe. (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ole-Sendeka, Mbunge wa Simanjiro kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni sahihi kabisa, Serikali ya Awamu ya Sita imedhamiria sana kuhakikisha kwamba imani ya wafanyabiashara inaimarika Zaidi. Na kama ambavyo Mheshimiwa Rais mwenyewe amekuwa akisema kwamba Serikali yake itahakikisha kwamba itafanya kila linalowezekana kuhakikisha inaibua vyanzo vya mapato. Jtihada mbalimbali mmeshaziona ambazo Mheshimiwa Rais mwenyewe binafsi amezifanya katika kuhakikisha kwamba anahamasisha uwekezaji nchini ili tuweze kupata wawekezaji wengi wakubwa waweze kutupatia kodi katika nchi hii; na amesema mara kadhaa kwamba hataki kuona kodi ya dhuluma.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo Wizara ya Fedha na Mipango tutakuwa watu wa mwisho sana kuona kwamba kama kuna mwananchi yeyote anadhumumiwa kupitia utaratibu wa kodi na tukalifumbia macho jambo hilo.

Kwa hiyo, niwahakikishie tu kwamba katika hoja hii hawa ambao wanahusiana na maduka ya fedha za kigeni tumefuatilia kwa kina na tumebaini kulingana na taarifa ambazo tunazo na vielelezo kadhaa ambavyo tunavyo, kwamba walihusishwa wenyewe mara kadhaa katika mchakato mzima wa mgogoro uliojitokeza. Imani yetu ni kwamba kama nilivyozungumza, kwamba wengi wao wamekubaliana na hali halisi baada ya kupewa ushahidi juu ya matukio mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, lakini kama kuna wale mnadhani bado, basi bado nafasi hiyo ipo kwa sababu Serikali hii imetoa mwanya na nafasi kwa yeyote ambaye anadhani bado hajatendewa haki kuweza kufuata taratibu za kudai haki yake ili aweze kuipata.

Name

Mrisho Mashaka Gambo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arusha Mjini

Primary Question

MHE. PRISCUS J. TARIMO aliuliza: - Je, ni nini hatma ya biashara ya maduka ya kubadilisha fedha (Bureau de Change) yaliyofungwa na Serikali?

Supplementary Question 4

MHE. MRISHO M. GAMBO: Mheshimiwa Spika, kwa sababu kumekuwa na malalamiko mengi sana kwa wafanyabiashara wa bureau, kwamba assessment ambazo zimefanyika hazikufanya na competent authority kwa sababu zilifanya na task force badala ya kufanywa na TRA kama wahusika.

Je, Wizara ya Fedha haioni sasa kwamba wakati umefika kwa TRA kwenda kupitia upya zile assessment ili yale makadirio yaani makadirio ambayo yapo kwa mujibu wa sheria?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mrisho Gambo Mbunge wa Arusha Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ninatambua Mheshimiwa Mrisho Gambo ni miongoni mwa watu ambao wananchi wa jimboni kwake wameathirika na jambo hili; na ikiwa kama Mbunge anawajibu anapopelekewa malalamiko na wananchi hapa ndipo sehemu yake pa kuyasemea.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo nimhakikishie Mheshimiwa Gambo kwamba assessment hii imefanywa na TRA kupitia Kitengo kile cha Investigation, kwa hiyo ni assessment ambayo imefanywa kwa mujibu wa taratibu na sheria na mamlaka sahihi kabisa ambayo inapaswa kufanya assessment.

Mheshimiwa Spika, lakini kama nilivyosema mwanzo, kwamba tuna utaratibu ambao iwapo mtu hajaridhika na assessment yote kuna utaratibu wa kufuata ili kuweza kuhakikisha kwamba anakata rufaa katika ngazi mbalimbali na kuangalia kama kuna uwezekano wa kuweza kui-review assessment yake ukafanyika hivyo.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie tu kwamba jambo hili lilisimamiwa na TRA wenyewe katika eneo la investigation.