Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Pindi Hazara Chana

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BALOZI DKT. PINDI H. CHANA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuwaunganisha Wakulima wa Mikoa ya Kusini hususan Mkoa wa Njombe na Wawekezaji wa nje na ndani?

Supplementary Question 1

MHE. BALOZI DKT. PINDI H. CHANA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri sana ya Serikali hususan kuhusu zao la parachichi, bado mikoa ya Kusini hususan Njombe, zao la mahindi limeendelea kuwa ni changamoto. Serikali ina mpango gani wa muda mrefu wa kuondokana na hii changamoto ya zao la mahindi? Ikiwa ni bei ya mahindi pamoja na changamoto ya mbolea kwa Mkoa wa Njombe na Mikoa ya Kusini?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Balozi Dkt. Pindi Chana, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, moja; Serikali kupitia Wizara ya Kilimo tukishirikiana na wenzetu wa Wizara ya Viwanda na Biashara tumeamua sasa hivi kubadili mfumo wa uuzaji wa mazao ya kilimo badala ya kusubiri wanunuzi kuja ndani ya mipaka ya Tanzania sasa tunawafuata katika maeneo yao. Serikali sasa hivi imeanza mchakato wa kufungua maghala katika baadhi ya nchi ikiwemo nchi ya South Sudan, tunafungua ghala letu la kwanza kwa ajili ya kuuza mazao, ghala hilo litatumika vilevile na private sector pale ambapo private sector wanataka kuuza. Vilevile tunafungua ghala la kuuza mazao ya chakula katika Jiji la Nairobi kwa ajili ya kuuza processed products kwa maana ya unga wa mahindi, mchele na mafuta ya kula ya alizeti, pia tunafungua ghala katika Jiji la Mombasa kwa ajili ya kuhudumia processors walioko katika nchi ya Kenya.

Mheshimiwa Spika, pia tumeanza juhudi ya kuangalia uwezekano wa kufungua maghala katika nchi ya Kongo, especially Kongo Mashariki ili badala ya sisi kusubiri wanunuzi kuja katika nchi yetu tunahakikisha kwamba bidhaa zinakuwepo katika masoko yao na inakuwa rahisi kuwahudumia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo jingine la muda mrefu ni uwekezaji katika tija ili kupunguza gharama za uzalishaji na cost per unit na kufanya mazao yetu kuwa competitive katika masoko yanayotuzunguka. Moja ya soko kubwa ni nchi kama Kenya ambayo ina deficit ya zaidi ya tani laki sita kwa mwaka ya mahindi ambayo tunaichukulia kama ni fursa kubwa na kipato cha mwananchi wa Kenya asilimia 50 anatumia katika chakula.

Mheshimiwa Spika, hivyo, kwetu hili ni eneo la fursa na ndiyo maana tunaamua kuwekeza katika miundombinu ambayo itatumika na Serikali lakini vilevile na sekta binafsi wanaweza kutumia kuuzia hizo outlets tunazofungua katika nchi hizo. (Makofi)

Name

Neema Kichiki Lugangira

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BALOZI DKT. PINDI H. CHANA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuwaunganisha Wakulima wa Mikoa ya Kusini hususan Mkoa wa Njombe na Wawekezaji wa nje na ndani?

Supplementary Question 2

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa, hitaji la wakulima kuunganishwa na wawekezaji wa nje na ndani lililopo kule Mikoa ya Kusini linafanana kabisa na hitaji la wakulima wa zao la vanilla kutoka Wilaya za Bukoba, Misenyi, pamoja na Muleba Mkoani Kagera, ningependa kufahamu Serikali ina mpango gani wa kuunganisha wakulima wa zao la vanilla na wawekezaji wa kutoka nje na ndani ya nchi? Ahsante.

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Neema, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli zao la vanilla linalimwa katika Mkoa wa Kagera, vilevile ni moja kati ya zao linalokua katika Mkoa wa Kilimanjaro. Nikiri tu hapa kwamba miongoni mwa Wabunge ambao wamekuwa wakilifuatilia zao hili mmojawapo ni Mheshimiwa Neema na Mheshimiwa Saasisha Mafuwe, Mbunge wa Mwanga - Kilimanjaro. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nataka tu niwahakikishie tumeanza mazungumzo na local exporters wa zao hili la vanilla ili tuanze kutengeneza mfumo wa contract farming moja kwa moja na mikataba. Mheshimiwa Shigongo naye ni mmoja kati ya waathirika wa zao hili, ili tuhakikishe zao hili linakua kwenye ramani, hili ni high value commodity na Wizara tumeanza kuwekeza kwenye research and development.

Kwa hiyo, niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge ni zao jipya ambalo limeanza kuchukua nafasi na tunalitazama kwa ukaribu sana na kuwaunganisha na masoko. (Makofi)

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. BALOZI DKT. PINDI H. CHANA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuwaunganisha Wakulima wa Mikoa ya Kusini hususan Mkoa wa Njombe na Wawekezaji wa nje na ndani?

Supplementary Question 3

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Mheshimiwa Spika, kwanza nimshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri wa Kilimo nami nilikuwa nauliza kuhusu vanilla, amenijibu vizuri mno na kutambua Wilaya yetu inalima zao hili.

Serikali kwa kuwa sasa imeona zao hili ambalo lina bei nzuri sana sokoni, mwanzoni ilikuwa ni 120,000 sasa hivi limeshuka kwa sababu ya kukosa watu wa kuwaunganisha, kilo inauzwa 20,000.

Je, Serikali ina mkakati gani sasa wa kuhakikisha inatuletea wataalam sambamba na hili ambalo ametuambia la kutafutia masoko? Ahsante. (Makofi)

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Saashisha Mafuwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika Bunge lako Tukufu hili mlitupitishia ongezeko la bajeti ya Wizara ya Kilimo kwenye utafiti zaidi ya asilimia 90. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge moja ya eneo ambalo tunaenda kuwekeza sana ni kwenye utafiti na training ya Wataalam hasa wanaoshiriki katika shughuli za uzalishaji kwa maana ya Wagani.

Kwa hiyo, nimhakikishie kwamba, mwaka huu tunaanza program ya training na Waziri wa kilimo wiki iliyopita amezindua training ya kwanza katika Wilaya ya Mpwapwa, Mkoa wa Dodoma na zoezi hili linaendelea nchi nzima tutakuwa tuna-train kutokana na ikolojia na mazao husika ya eneo husika ya eneo husika ili kuwafanya wataalam waweze kufanana na mazao yaliyoko eneo hilo. (Makofi)