Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Antipas Zeno Mgungusi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kutenga fedha za kuvunja Mlima Londo ili kuunganisha Wilaya ya Malinyi na Namtumbo hata kwa kiwango cha changarawe ili njia hii iweze kupitika huku Serikali ikiendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa kiwango cha lami wa Barabara ya Lupiro – Malinyi – Kilosa –Kwa Mpepo – Namtumbo Lumecha ya kilomita 296?

Supplementary Question 1

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Nilijitahidi kuwa specific kidogo; watu wa Malinyi na Namtumbo na Ruvuma yote tunahitaji kuona Mkoa wa Morogoro na Ruvuma unaunganishwa kwa maana ya kufunguliwa. Suala la lami tutavumilia kusubiria, tunajua gharama ni kubwa, kilometa ni nyingi, lakini kuunganisha tu hata kwa kiwango cha vumbi; je, Serikali iko tayari?

Mheshimiwa Naibu Spika, kama inaridhia, iko tayari kuweka fedha kidogo kwa ajili ya barabara hiyo katika bajeti inayofuata? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Antipas Mgungusi Mbunge wa Malinyi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama alivyosema, eneo analoliongelea lina milima mingi na linapita kwenye safu ya Mbuga ya Selous, ina urefu wa takribani kilometa zisizopungua kama kilometa 100. Ndiyo maana katika jibu letu la msingi tumesema tumeona tumefanya tathmini, kuvunja ule mlima ni gharama sana.

Kwa hiyo, kuna haja ya kutafuta fedha kubwa ili katika huo mradi tuweze kupindisha barabara kuzunguka hiyo milima ili tuweze kuwa na uhakika wa kuipitisha hiyo barabara.

Mheshimiwa Naibu Spika, ombi lake limechukuliwa, lakini ni wazi kwamba fedha inayohitajika ni eneo la zaidi ya kilometa 100. Kwa hiyo, ni bora tukaamua kabisa kuujenga huo mradi. Hata hivyo, bado tumeendelea kutoa fedha kidogo ili kufungua kulingana na fedha inavyopatikana kuunganisha Mkoa wa Ruvuma na Morogoro kati ya Wilaya hizo mbili za Malinyi na Namtumbo. Ahsante.

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kutenga fedha za kuvunja Mlima Londo ili kuunganisha Wilaya ya Malinyi na Namtumbo hata kwa kiwango cha changarawe ili njia hii iweze kupitika huku Serikali ikiendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa kiwango cha lami wa Barabara ya Lupiro – Malinyi – Kilosa –Kwa Mpepo – Namtumbo Lumecha ya kilomita 296?

Supplementary Question 2

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi nami niulize swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Serikali iligharamia barabara hii fedha nyingi sana; imejenga madaraja ya Mto Kilombero kwa gharama kubwa, imejenga Mto Furua, Mto Mwatisi, Mto Londo na Mto Luhila kwa upande wa Mkoa wa Ruvuma Jimbo la Namtumbo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali haioni sasa ipo haja kukifungua hiki kipande ili tuweze kupita angalau barabara iwe inapitika na gharama zilizoingia kwa Serikali kujenga haya madaraja, basi zionekane zina faida?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Vita Kawawa, Mbunge wa Namtumbo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sana nimpongeze Mheshimiwa Vita Kawawa kwa kutambua juhudi kubwa ambazo zinaendelea na Serikali hii ya Awamu ya Tano na ya Sita ambapo tumeshajenga madaraja haya aliyoyataja, dhamira njema ya Serikali ikiwa ni kuiunganisha iwe mkoa. Katika kitu kigumu kwenye barabara ni madaraja. Kwa hiyo, anaeleza pia kwamba Serikali ina dhamira kabisa na ndiyo maana tumeendelea kujenga hizo barabara.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tayari mwaka huu tumetenga shilingi bilioni mbili na nusu kwa ajili ya kuendelea kuijenga hiyo barabara. Kwa hiyo, kadri fedha zitakazopatikana naomba nimhakikishie Mheshimiwa Kawawa na Mheshimiwa wa Malinyi kwamba Serikali ina nia ya dhati. Kwa hiyo, tutaikamilisha hiyo barabara; na kama walivyosema, inawezekana tukaanzia eneo hilo ambalo sasa limekuwa ni kikwazo zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.

Name

Felista Deogratius Njau

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kutenga fedha za kuvunja Mlima Londo ili kuunganisha Wilaya ya Malinyi na Namtumbo hata kwa kiwango cha changarawe ili njia hii iweze kupitika huku Serikali ikiendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa kiwango cha lami wa Barabara ya Lupiro – Malinyi – Kilosa –Kwa Mpepo – Namtumbo Lumecha ya kilomita 296?

Supplementary Question 3

MHE. FELISTA D. NJAU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Ni lini Serikali itajenga barabara inayoanzia Bunju A kupitia Mabwepande ikiunganisha na Jimbo la Kibamba ambayo barabara hiyo imekaa muda mrefu na ikitolewa ahadi bila utekelezaji? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Felista Njau, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba yalikuwa pia ni ahadi ya Mheshimiwa Hayati Rais na pia yalikuwa ni maagizo. Kwa hiyo, nimhakikishie kwamba hizo barabara, TANROADS kwa maana ya Mkoa wa Dar es Salaam kusaidiana na Ofisi ya Rais, TAMISEMI (TARURA) tutahakikisha kwamba hizi barabara zinatekelezwa kuanzia kipindi hiki cha mwaka wakati wa utekelezaji wa bajeti ya kuanzia mwaka huu 2021. Ahsante.

Name

Michael Mwita Kembaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Mjini

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kutenga fedha za kuvunja Mlima Londo ili kuunganisha Wilaya ya Malinyi na Namtumbo hata kwa kiwango cha changarawe ili njia hii iweze kupitika huku Serikali ikiendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa kiwango cha lami wa Barabara ya Lupiro – Malinyi – Kilosa –Kwa Mpepo – Namtumbo Lumecha ya kilomita 296?

Supplementary Question 4

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa nachukua nafasi hii kuipongeza Serikali kwa kutupa zaidi ya kilometa 80 ya barabara ya lami kutoka Tarime Mjini, kuelekea Serengeti.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu ni kwamba kwa sababu tayari wananchi wakazi wale wa Tarime waliopo pembezoni mwa barabara wameshabomoa nyumba zao kwa ajili ya kulima barabara ile, lakini kuna kipande ambacho kulikuwepo na Mkandarasi ambaye alikuwa anajenga kipande pale Lebu Center kwenda Mugabiri na tayari yule Mkandarasi anaendelea…

NAIBU SPIKA: Uliza swali Mheshimiwa Kembaki.

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI: Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo najenga hoja ya swali langu.

NAIBU SPIKA: Huna haja ya kujenga hoja, wewe taja barabara unayotaka kuulizia swali.

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI: Mheshimiwa Naibu Spika, Mkandarasi yule anaendelea na ujenzi wa kile kipande na tayari wananchi wamebomoa kwamba ile barabara inajengwa upya kutoka hapo mjini kuelekea…

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Kembaki uliza swali.

MHE. MICHAEL M. KEMBAKI: Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu ni hivi ni kwa nini Mkandarasi yule asingepewa sehemu nyingine ajenge badala ya kujenga sehemu ambayo tayari TANROADS watakuja kujenga?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Michael Kembaki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Mkandarasi yupo site na anajenga, namwomba Mheshimiwa Mbunge baada ya hapa nikutane naye kupata maelezo sahihi kwa ajili ya kutatua hiyo changamoto anayosema ili kwa pamoja na Meneja wa TANROADS Mkoa tuone namna ya kuondoa hiyo changamoto. Ahsante.

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kutenga fedha za kuvunja Mlima Londo ili kuunganisha Wilaya ya Malinyi na Namtumbo hata kwa kiwango cha changarawe ili njia hii iweze kupitika huku Serikali ikiendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa kiwango cha lami wa Barabara ya Lupiro – Malinyi – Kilosa –Kwa Mpepo – Namtumbo Lumecha ya kilomita 296?

Supplementary Question 5

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii nami niweze kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kumekuwepo na ahadi za viongozi wetu Wakuu wa Serikali na ahadi hizi zimekuwa zikitolewa tangu Awamu ya Nne, Awamu ya Tano na sasa Awamu ya Sita na ahadi hizo zimekuwa hazipo katika mkakati mzuri wa kuziratibu na pengine kuweka bajeti kwa ajili ya kuzitekeleza: Nini mpango mkakati wa Serikali wa kuhakikisha kwamba sasa ahadi zile zote zinaratibiwa nchi nzima na kuwekewa mkakati wa kibajeti ili mradi ahadi hizi ziwe ni ahadi zinazotekelezeka? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Boniphace Butondo, Mbunge wa Kishapu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Boniphace Butondo kwamba ahadi zote zinazotolewa na viongozi wa kitaifa zimeratibiwa na kwa kweli tunazifahamu na ndiyo maana tunakuwa tunazitambua kwamba zinatakiwa zitekelezwe. Zikishatolewa ahadi zinakuwa ni kipaumbele.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mbunge kwamba kinachogomba hapa wakati fulani huwa ni bajeti kwamba unapanga, lakini hutegemea na bajeti ya Serikali. Kwa hiyo, ahadi zote ambazo zimetolewa zikiwepo na ahadi ambazo zimetolewa katika Jimbo lake, tunazifahamu na tumeziratibu na nyingine tumezipangia bajeti.

Kwa hiyo, ndiyo maana tunasema kulingana na upatikanaji wa fedha zikipatikana, miradi yote ambayo Waheshimiwa Viongozi wetu wa Kitaifa wamezitoa tutaitekeleza. Ahsante.