Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Francis Leonard Mtega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbarali

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: - Je, ni lini viongozi wa Kitaifa wataanza kutembelea nchi za nje mahsusi kwa ajili ya kutafuta masoko ya mazao hususan mpunga na mahindi?

Supplementary Question 1

MHE. FRANCIS L. MTEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, nimshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri na zaidi nimshukuru na kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa kazi kubwa na nzuri anayoifanya. Hata hivyo, nina swali la nyongeza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa wakulima wale mpaka sasa hivi tunavyoongea, bado mazao ya mahindi na mpunga ni mengi sana na kwa kuwa, wanaelekea msimu mpya wa kilimo na bei ya mbolea iko juu na wengine wanashindwa kufanya marejesho ya benki.

Je, Mheshimiwa Naibu Waziri atakubaliana nami kwamba muda umefika sasa wa kuunda task force maalum ya Waheshimiwa Mawaziri. Pengine ikijumuisha na baadhi ya Waheshimiwa Wabunge wa Kamati za sekta husika, ili waende mahsusi kutafuta masoko kabla ya msimu mpya wa kilimo? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Amber. Mbarouk Nassor Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA
AFRIKA MASHARIKI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Francis Leonard Mtega, Mbunge wa Mbarali kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa jinsi anavyofuatilia upatikanaji wa masoko ya bidhaa ikiwemo mchele, na mahindi. Lakini pia, ninakubaliana na wazo la Mheshimiwa Mbunge kwa kuunda hiyo task maalum kwa ajili ya kutafuta hayo masoko. Lakini pia ninaomba kumfahamisha Mheshimiwa Mbunge kwamba, juhudi nyingi sana hivi sasa zinachukuliwa na Serikali katika kutafuta masoko ya bidhaa hizo. Hivi sasa ninavyosema kuna timu ya Wizara ya Kilimo ambayo iko nchini Comoro, mahsusi kwa kutafuta soko la bidhaa ya mchele na mahindi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia ni juzi tu, timu hiyo ilitoka South Sudan kwa nia hiyo hiyo ya kutafuta soko la mahindi na mpunga na mwisho ninapenda kumfahamisha Mheshimiwa Mbunge kwamba, TANTRADE wana utaratibu maalum wa kuwasiliana na Balozi zetu ambazo ziko nje mahsusi kwa ajili ya kutafuta soko kwa bidhaa za Tanzania ikiwemo za mpunga na mahindi. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FRANCIS L. MTEGA aliuliza: - Je, ni lini viongozi wa Kitaifa wataanza kutembelea nchi za nje mahsusi kwa ajili ya kutafuta masoko ya mazao hususan mpunga na mahindi?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niulize swali.

Kwa kuwa tatizo la masoko liko pia katika mazao mbalimbali nchini na kwa kuwa sasa hivi, ni lini Serikali itaona umuhimu wa kuweka kitengo cha kutafuta masoko katika Balozi zetu, ili kiweze kushughulikia tatizo la masoko katika mazao mbalimbali nchini? (Makofi)

Name

Amber. Mbarouk Nassor Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ritta Kabati kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, hivi sasa tayari Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imeunda Idara maalum ya Economic Diplomacy, kwa ajili mahsusi ya kutafuta masoko ya bidhaa zetu. Ahsante sana. (Makofi)