Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Haji Makame Mlenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chwaka

Primary Question

MHE. HAJI MAKAME MLENGE aliuliza: - Je, ni lini Kituo cha Polisi cha Chwaka kitapatiwa gari ili kutimiza majukumu yake kwa ufanisi zaidi?

Supplementary Question 1

MHE. HAJI MAKAME MLENGE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Naomba kuuliza swali moja tu la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Jimbo la Chwaka lina kituo kingine kidogo cha Polisi kilichopo Jozani: Je, Serikali haioni kwamba kuna sababu ya kukipelekea usafiri angalau wa ma-ring mawili? Ahsante.

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Haji Makame Mlenge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba tunayo changamoto kubwa sana katika vituo vingi vya Polisi, shida kubwa ikiwa usafiri. Yapo maeneo hata ya wilaya nzima kabisa ikiwemo Wilaya ya Kongwa, gari pale ni mbovu na iko moja.

Mheshimiwa Spika, Zanzibar kule vituo hivi viko karibu karibu sana. Katika kugawa magari haya tutaangalia sana hata ukubwa wa jiografia, tutaangalia pia maeneo yenye changamoto kubwa zaidi hasa ya mipakani. Vile vile niseme tu, kwa maeneo ambayo vituo viko karibu karibu, huduma ile wanaweza kuipata katika wilaya, kwa sababu setup yetu katika vituo vya Polisi, bado ni ya kiwilaya zaidi, siyo vituo vile vidogo vidogo. Kwa hiyo, niseme tu tutakwenda kuangalia tuone umbali kati ya kituo hiki anachokisema na kituo cha wilaya halafu tuone kama hilo analolisema litawezekana. Ahsante sana.

Name

Godwin Emmanuel Kunambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. HAJI MAKAME MLENGE aliuliza: - Je, ni lini Kituo cha Polisi cha Chwaka kitapatiwa gari ili kutimiza majukumu yake kwa ufanisi zaidi?

Supplementary Question 2

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Kwa kuwa changamoto ya wananchi wa Chwaka inafanana kabisa na ya wananchi wa Jimbo la Mlimba, kwenye Kituo cha Polisi cha Mlimba: Je, Mheshimiwa Waziri haoni hayo magari yatakapofika katika mpango wake, basi aweze kukumbuka pia na Kituo hiki cha Polisi Mlimba? Ahsante.

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Godwin Kunambi, Mbunge wa Mlimba, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli tunafahamu kwamba changamoto hii, kama nilivyosema, iko katika vituo vingi. Naamini hata Kituo cha Polisi cha Mlimba ambacho kina hadhi ya Kituo cha Wilaya kina changamoto kubwa sana ya gari. Kwa kawaida hata angalau magari yakipungua sanakwenye Kituo cha Wilaya, yanapaswa kuwa angalau matatu au manne, lakini pale kuna gari moja na lingine bovu.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba maeneo yenye changamoto za miundombinu, changamoto za shughuli za uzalishaji ndiyo zitapewa kipaumbele magari haya yatakapofika.