Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza vituo vya kuchotea maji katika Mji Mdogo wa Gairo?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Licha ya majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kwanza niishukuru Serikali, nina furaha sana kuona kuwa Mradi wa Chagongwe, ambao ni wa muda mrefu, unaanza. Je, mradi huu wa kutoka Milima ya Chagongwe na Nongwe utaanza kutekelezwa lini?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; Manispaa ya Morogoro, nashukuru Serikali inaendesha miradi ya maji kwenye manispaa yetu, lakini hata hivyo bado tunapata maji ya mgao. Je, miradi hii, hasa mradi wa Bwawa letu lile la Mindu, ni lini hasa litakamilika na miradi mingine, ili wananchi wa manispaa waweze kupata maji kila siku na waondokane na maji ya mgao? Ahsante sana.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge mama yangu Dkt. Christine Ishengoma ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati yetu ya Kilimo, Mifugo na Maji kwa kazi kubwa na nzuri na anatusimamia vizuri sana ili sisi Wizara kuhakikisha watu wanapata huduma ya maji safi na salama.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge, ambacho ninataka kukuhakikishia Mheshimiwa Mwenyekiti wetu ni kwamba eneo la Mradi huu wa Chagongwe, katika mwaka huu wa fedha tunaokwenda nao tumepata fedha ambazo ni za ziada za Mheshimiwa Rais, zaidi ya bilioni 207. Hili ni eneo ambalo tutalipa umuhimu mkubwa kuhakikisha katika mwaka huu unaoanza wa fedha, kwenda kuanza mradi huu na wananchi wa Gairo waweze kupata huduma ya maji safi na salama.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili la Mheshimiwa Mbunge ni kuhusu suala zima la maji katika eneo la Morogoro. Mji wa Morogoro uzalishaji wake ni lita milioni 35, lakini mahitaji yake kwa sasa ni lita milioni 67, kwa hiyo, kuna uhitaji mkubwa sana wa maji, kwa hiyo mkakati wa haraka katika siku 100 za Mheshimiwa Rais, mama Samia Suluhu Hassan, ametupatia fedha zaidi ya bilioni nne kwa ajili ya kujenga mradi wa haraka.

Mheshimiwa Naibu Spika, na tumejenga tenki la lita milioni mbili eneo la Mgulu wa Ndege ambapo tutakwenda kutumia chanzo cha maji cha Mambogo ambao tumeweka maji katika tenki lile la Mgulu wa Ndege ambapo maji yale yatakwenda Kihonda, maji yale ambayo yatakwenda eneo la SGR, Lukobe na Mkundi katika ili kuhakikisha wananchi wa Morogoro wanapata huduma ya maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mkakati wa kumaliza kabisa tatizo la maji katika Mji wa Morogoro, tumepata fedha zaidi ya Euro milioni 70, ambapo tumekwishasaini mkataba na wahandisi washauri, mradi ule tunakwenda kuhakikisha unaanza kwa haraka ili wananchi wa Morogoro waweze kupata huduma ya maji safi na salama.

Name

Dr. Florence George Samizi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Primary Question

MHE. DKT CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza vituo vya kuchotea maji katika Mji Mdogo wa Gairo?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nami nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Je, ni lini Serikali itajenga na kuboresha miundombinu ya maji katika Jimbo la Muhambwe, hususan Kata za Kibondo Mjini, Bunyambo na Kitahana ili kukabiliana na uhaba mkubwa wa maji ulioko katika jimbo hilo?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ikumbukwe, nadhani mwezi mmoja ama miwili iliyopita, Mheshimiwa Mbunge wa Mihambwe ameingia katika Bunge hili. Amekuja ofisini, na jana tumekwisha mpa pesa, zaidi ya milioni 100 ili kuhakikisha kwamba wananchi wake wanakwenda kupata huduma ya maji safi na salama. Ahsante sana.

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. DKT CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza vituo vya kuchotea maji katika Mji Mdogo wa Gairo?

Supplementary Question 3

MHE. MAIMUNA S. MTANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipatia fursa hii. Chanzo cha maji ya Mitema ambacho kipo katika Jimbo la Newala Vijijini kina maji ya kutosha kiasi kwamba kama uwekezaji wa fedha utakuwa wa kutosha, tatizo la maji katika Jimbo ya Newala Vijijini, Newala Mjini, Tandahimba na baadhi ya Kata za Nanyama zitaondokana na shida ya maji. Je, ni lini Serikali itawekeza fedha za kutosha katika chanzo cha maji cha Mitema ili kuondoa kadhia ya maji kwa wananchi wa maeneo tajwa? Ahsante.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge wa Newala Vijijini. Lakini pia nimpongeze sana, juzi tuliweza kukutana pia na Mheshimiwa Mbunge wa Newala Mjini, baba yangu, mzee wangu, Mheshimiwa Kapteni Mkuchika, juu ya Mradi huu wa Makonde. Ni mradi wa muda mrefu sana ambao umekuwa na maneno mengi sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka niwahakikishie nikiwa mwenye dhamana ya Wizara ya Maji, Mheshimiwa Rais ametupa maelekezo mahususi kwa ajili ya Watanzania, waweze kupata huduma ya maji safi na salama. Juzi tumekaa kikao baada ya mazungumzo yale, maelekezo ambayo tumeyatoa ni kwamba mradi ule tunakwenda kuuanza, iwe jua iwe mvua, ili wananchi wa Newala waweze kupata huduma ya maji safi na salama. Ahsante sana.

Name

Tabasamu Hamisi Hussein Mwagao

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sengerema

Primary Question

MHE. DKT CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza vituo vya kuchotea maji katika Mji Mdogo wa Gairo?

Supplementary Question 4

MHE. TABASAM H. MWAGAO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kupata nafasi ya kuuliza swali la nyongeza kwa Waziri wa Maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninachosema ni kwamba Sengerema tunadaiwa pesa, shilingi milioni 300 kwa ajili ya umeme, na hili deni limekuwa la muda mrefu. Nini kauli ya Waziri kuhusiana na deni hilo ili tuanze kuanza upya, kwa sababu tumepata meneja mpya Sengerema? Ahsante.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge wa Sengerema kwa kazi kubwa na nzuri anayoifanya. Ni haki ya mwananchi kupatiwa huduma ya maji. Na mwenye wajibu na jukumu la kumpatia huduma ya maji ni Wizara ya Maji, kwa maana ya Serikali.

Mheshimiwa Naibu Spika, Sengerema ni eneo ambalo lilikuwa na changamoto sana ya maji. Serikali kwa dhamira
njema imewekeza mradi wa zaidi ya bilioni 25 wananchi wa Sengerema waweze kupata huduma ya maji safi na salama. Sasa ni jukumu la Mamlaka ya Maji ya Sengerema kuhakikisha kwamba inakusanya bili na kulipia umeme ili uendeshaji wake uwe vizuri sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, tulikuwa tuna changamoto ya uendeshaji; Meneja, kwa maana ya Mkurugenzi wa mamlaka ile nimemuondoa, fedha hizi za deni tutazilipa, lakini kwa masharti ya kuhakikisha kwamba wanajitegemea na wanaendesha mamlaka ile vizuri na wananchi wa Sengerema wanapata huduma ya maji safi na salama. Ahsante sana.

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. DKT CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza vituo vya kuchotea maji katika Mji Mdogo wa Gairo?

Supplementary Question 5

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana, kumekuwepo na tatizo kubwa la kukatika sana kwa maji katika Mji wa Munze, Kishapu, Kata ya Mwadui Lohumbo, na Maganzo. Lakini Mheshimiwa Waziri aliwahi kujibu kwamba tatizo kubwa ni malipo ya madeni ya muda mrefu ya wateja, lakini wateja wamelipia madeni yao kwa wakati. na hili nimefuatilia mwenyewe nimeona kwamba kweli hawadaiwi.

Mheshimiwa Naibu Spika, je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kufika katika Jimbo la Kishapu kujionea na kutoa utatuzi wa kudumu juu ya tatizo la kukatika kwa maji katika Mji wa Munze na maeneo mengine?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze sana kaka yangu, Mbunge wa Kishapu; kwa kweli unafanya kazi kubwa na nzuri sana katika jimbo lako.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niweke wazi kabisa maeneo ambapo Serikali imewekeza miradi mikubwa kwa
ajili ya wananchi waweze kupata huduma ya maji, na wananchi wanalipia bili za maji ili kuhakikisha kwamba mamlaka inajiendesha, maeneo ambayo wananchi wanalipia bili zile za maji lakini wakurugenzi ama watendaji ambao wanashindwa kuendesha mamlaka hizo, hakuna neno lingine zaidi ya kutupisha. Tutaweka watu ambao wataweza kutuendesha ili mamlaka zetu ziweze kwenda na Watanzania waweze kupata huduma ya maji safi na salama. Ahsante sana.