Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdallah Jafari Chaurembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuyarudisha kwenye Halmashauri maeneo yote yasiyoendelezwa na Mashirika ya Umma kwa zaidi ya miaka kumi ili Halmashauri zijenge miundombinu ya huduma za jamii?

Supplementary Question 1

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Halmashauri ndiyo Mamlaka za Upangaji: ni lini Wizara ya Ardhi itakabidhi viwanja vya mradi wa viwanja 20,000 kwa Halmashauri ya Manispaa ya Temeke ili kuyapangia matumizi mengine maeneo yote ya Taasisi ambayo hayakuendelezwa katika Kata ya Tuangoma na Kibada hasa katika Kiwanja kilichopo Goroka Block D, Block 10 Kiwanja Na. 219, Changanyikeni Block 9 Kiwanja Na. 215, mashamba pori ya NSSF ya Mtaa wa Masuliza, Mwapemba, Vikunai na Changanyikeni? (Makofi)

Swali la pili: Je, ni lini Wizara ya Ardhi itaweka miundombinu ya barabara katika mradi wa viwanja 20,000 katika maeneo yote ya Kata ya Tuangoma. (Makofi)

Name

William Vangimembe Lukuvi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ismani

Answer

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri sana ya Naibu Waziri, Mheshimiwa Dkt. Angeline Mabula, nataka tu niwaeleze Waheshimiwa Wabunge, alichosema Mheshimiwa Chaurembo ni kweli kwamba kwa mujibu wa Sheria Mamlaka za Upangaji wa Ardhi ni Halmashauri. Kwa hiyo, sisi kama Madiwani ni sehemu ya Mamlaka ya Upangaji wa Ardhi. Kila Halmashauri inapanga yenyewe matumizi ya ardhi yake. Ingawa tunashirikiana katika kuthibitisha ule upangaji, lazima uthibitishwe na Wizara ya Ardhi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Dar es Salaam kuna mradi ulianzishwa miaka ya nyuma ya viwanja 20,000. Sasa leo nataka niseme hapa mbele ya Mheshimiwa Mbunge, viwanja 20,000 vilivyopimwa katika Wilaya ya Temeke, kwa mfano hivi vya Tuangoma iliyokuwa miradi 20,000 na Kibada, nimeshaagiza na ninarudia tena kuagiza, Wizara ya Ardhi ikabidhi michoro ya viwanja hivi 20,000 kwa Manispaa ya Temeke na wiki hii lazima makabidhiano yafanyike ili wananchi na Wilaya ya Kigamboni waweze kusimamia ipasavyo miradi hii ya viwanja 20,000.

Mheshimiwa Naibu Spika, ulikuwa ni mradi ndani ya Wilaya ya Temeke, sasa michoro yote na taarifa zote za umiliki ziwe ni open space, maeneo ambayo hayajaendelezwa, Temeke liwe ni jukumu lao kufuatilia. Kama kuna watu hawajaendeleza Temeke ni Mamlaka halisi. Pekuweni tutoe notice kwa watu ambao hawajaendeleza tuchukue hatua mchukue ardhi hizo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naagiza Kamishina wa Ardhi akabidhi michoro na taarifa zote. Kuanzia leo, eneo lote la Viwanja 20,000 la Kibada na Tuangoma lazima liwe chini ya Mamlaka ya Manispaa ya Temeke. Hayo mengine mtafanya wenyewe. (Makofi)