Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka huduma ya maji safi na salama kwa wananchi wa Kata za Mwamala, Samuye, Busanda, Usule, Bukene na Imesela?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri. Kwa kuwa katika majibu yake ya msingi amesema kwamba mradi wa muda mrefu wa Shelui – Tinde utaweza kukidhi mahitaji ya wananchi wa Shinyanga: Je, ni lini sasa Mradi wa Shelui –Tinde utaanza kwa kuwa mkataba umeshasainiwa toka tarehe 25 mwezi wa Pili? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa tunajua Sera ya Maji ni kuhakikisha kwamba inasambaza maji katika vijiji vyote ambavyo vinapitiwa na bomba kuu la Ziwa Victoria.

Je, ni lini Serikali itaanza kusambaza maji katika Kata za Lyabukande, Lyamidati, Nindo, Imesela na Didia?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Mradi huu kama nilivyojibu kwenye jibu langu la msingi tunatarajia kutoa maji Ziwa Victoria na Shelui – Tinde pia itakuwa ni moja ya wanufaika mwaka ujao wa fedha, kadiri fedha tunavyozipata.

Mheshimiwa Mwenyrkiti, napenda sana kumshukuru Mheshimiwa Rais, tumesikia jana wakati Bajeti ya Serikali Mheshimiwa Waziri akihitimisha pale, Mheshimiwa Rais ametuongezea fedha ambazo zitatusaidia kuongeza maeneo mengi katika nchi hii kuhakikisha maji ya uhakika yanakwenda kupatikana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile suala la usambazaji maji katika miradi yetu hii ni lazima ifanyike. Lengo ni kuona kwamba, wananchi wanapelekewa maji karibu na makazi yao na kupunguziwa umbali mrefu wa kutembea. (Makofi)

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka huduma ya maji safi na salama kwa wananchi wa Kata za Mwamala, Samuye, Busanda, Usule, Bukene na Imesela?

Supplementary Question 2

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, je, Serikali lini itakamilisha mradi wa maji wa visima vya Kimbiji na Mpera kuwasaidia wananchi wa Halmashauri ya Kigamboni waweze kupata maji safi na salama; na pia katika Kata za Tuangoma, Chamazi, Mbande, Mianzini, Kibondemaji na Charambe wote hawa waweze kunufaika na mradi huo?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Visima hivi vya maji vya maeneo ya Kimbiji, Kigamboni na maeneo haya yote ya ukanda ule vinatarajiwa kuhakikishwa vinakamilika mwaka ujao wa fedha, kadiri fedha ambavyo tutakuwa tukiendelea kuzipokea ndani ya Wizara yetu. Maeneo ya Tuangoma, Majimatitu, kote huko Wizara inatupia jicho la kipekee kabisa. Tunafahamu ongezeko la wakazi ni kubwa, hivyo na sisi tutahakikisha tunafanya kazi usiku na mchana ili maji yaweze kuwafikia wananchi wa maeneo haya.

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka huduma ya maji safi na salama kwa wananchi wa Kata za Mwamala, Samuye, Busanda, Usule, Bukene na Imesela?

Supplementary Question 3

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwenye Wilaya ya Kyerwa, Kata ya Bugomora, Kata ya Mlongo, Kata ya Kimuli na Kata ya Kyerwa Kagenyi, kuna miradi ambayo usanifu wake umekamilika, lakini mpaka sasa hivi Serikali bado haijatoa fedha ili miradi hii ianze. Lini Serikali itatoa fedha miradi hii ianze? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa hiyo compliment. Kwa swali la Mheshimiwa Mbunge kutoka Jimbo la Kyerwa, eneo hili pia Serikali tumeendelea kulipa jicho la kipekee. Wizara kupitia RUWASA na mamlaka pale Mji wa Kyerwa wataendelea kushirikiana kuhakikisha miradi hii yote ambayo haijakamilika iweze kukamilika kwa wakati ili wananchi waweze kunufaika na Serikali ya Awamu ya Sita.

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka huduma ya maji safi na salama kwa wananchi wa Kata za Mwamala, Samuye, Busanda, Usule, Bukene na Imesela?

Supplementary Question 4

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Changamoto ya maji katika Kata za Murongo, Kibale, Bugomora ambazo ni kata za mpakani mwa Mto Kagera zinaweza kumalizwa kama kukianzishwa mradi mkubwa wa maji kutoka Mto Kagera kuja kuhudumia wakazi. Je, ni nini mpango wa Serikali kuhakikisha tunapata maji ya kutosha kutoka Mto Kagera kuhudumia hizi kata ambazo ziko pembezoni mwa huo mto? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Anatropia, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napenda kumpongeza Mheshimiwa Anatropia, hakika akina mama tunasemeana vema. Tunafahmu mwanamama ndiye anayepata shida ya kubeba maji kichwani na sisi kama Wizara tumesema lazima tumtue mama ndoo kichwani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maji kutoka Mto Kagera sisi kama Wizara ni moja ya vipaumbele vyetu kutumia mito na maziwa makuu kuhakikisha maji yanapatikana. Kama nilivyomjibu Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo, Mheshimiwa Anatropia tutakuja pamoja na Mheshimiwa wa Jimbo tutaweka mambo sawa, Kyerwa maji yatapatikana. (Makofi)