Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Edwin Enosy Swalle

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza: - Je, upi mpango wa Serikali katika kukwamua zao la zhai ambalo ni miongoni mwa mazao ya kimkakati yenye changamoto nyingi nchini?

Supplementary Question 1

MHE. EDWIN E. SWALLE: Mheshimiwa Spika, ahsante, kwanza nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali juu ya mpango wa zao hili la chai. Ninayo maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, kwa kuwa tatizo kubwa la wakulima wa chai sasa hivi nchini ni kutokulipwa kwa wakati na wawekezaji; na viongozi wetu wa Serikali wamekuja Mkoa wa Njombe akiwemo Waziri wetu Mkuu na alitoa maelekezo wakulima walipwe kwa wakati lakini mpaka sasa wakulima hawajalipwa hela yao ya chai. Je, ni kauli ipi ya matumaini ya Serikali juu ya wananchi kulipwa fedha zao za chai? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa wawekezaji wengi waliopo sasa hasa Mkoa wa Njombe wanaonekana kutokuwa na uwezo na wakulima wamehamasika kufufua mashamba yao mengi ya chai hivi sasa.

Je, Serikali haioni haja sasa ya kutafuta wawekezaji wengine kwa ajili ya zao la chai Mkoani Njombe? (Makofi)

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Swalle kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nikiri kwa niaba ya Serikali kwamba Wabunge wa maeneo ya Mufindi, Lupembe na Mkoa wa Njombe kwa ujumla wamekuwa wakifanya jitihada kubwa sana kufanya follow-up kuonesha stability ya zao la chai. Na nipitie Bunge lako hili na kuwahakikishia Wabunge kwamba kampuni zinazosuasua ni kampuni mbili; Uniliver nalipa vizuri na hana matatizo na wakulima wote wanaomhudumia. Tumebaki na changamoto na Kampuni ya DL na mwekezaji wa Lupembe Tea Company Ltd.

Kwa hiyo, kupitia Bunge lako nataka tu niwahakikishie Wabunge kwamba tumewa-summon hawa wawekezaji wawili na tutakutana nao katika Ofisi ya Wizara ya Kilimo, Mwenyezi Mungu akitujaalia kabla ya tarehe 30. Na kwa kuwa Wabunge mtakuwepo, tutawahusisha katika kikao hicho ili tuweze kufikia solution. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuhusu mwekezaji wa Kampuni ya Lupembe, hana option either ku-implement tulichokubaliana ama apishe menejimenti kwa sababu Chama cha Ushirika ni sehemu ya shareholders wa ile kampuni; kaongoza kwa muda mrefu hatujaona performance, tutaweka menejimenti ya muda ambayo itahusisha watu watakaotoka ndani ya Serikali na ushirika na yeye ili waweze kuendesha kile kiwanda kwa sababu kwa muda mrefu tumempa nafasi na ameshindwa kutimiza wajibu wake.

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza: - Je, upi mpango wa Serikali katika kukwamua zao la zhai ambalo ni miongoni mwa mazao ya kimkakati yenye changamoto nyingi nchini?

Supplementary Question 2

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI: Mheshimiwa Spika,
asante sana kwa kunipa fursa na naomba nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba Serikali inatoa kauli gani kuhusiana na bughudha wanazopata wafanyabiashara na wakulima wa soya wa Mikoa ya Ruvuma na Mbeya kwa sababu wanazuiliwa kuuza na kununua wanavyotaka na tunajua zao hili limepata soko huko China sasa hivi. Serikali inatoa kauli gani? (Makofi)

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo naomba kujibu swali la Profesa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, position ya Wizara ya Kilimo na Serikali ipo very clear na nitumie Bunge lako Tukufu kusema zao la soya Mkoa wa Ruvuma na mikoa yote inayolima soya halimo kwenye stakabdhi ya ghala. Ninaomba Wakurugenzi wa Halmashauri, Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Mikoa wasibughudhi mnunuzi yeyote anayeenda kununua kwa mkulima zao hili. Tumelisema kwa mdomo na tumeandika, tunarudia tena, asibughudhiwe mnunuzi yeyote anayenunua zao la soya, volume ya soya aina economic viability kuingiza kwenye stakabadhi ya ghala, bado volume ni ndogo. Wizara ya Kilimo ndio ina-mandate ya kutangaza zao gani liingie kwenye stakabadhi ya ghala. Tumesema mwaka huu waliondoe. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, zao lingine ni choroko na dengu yaliyopo katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa hayaingii katika mfumo wa ushirika kwanza, tutayaingiza wakati utakapofika na tutakapoona kwamba sasa ni muhimu kufanya namna hiyo. Tumetoa guidance kwenye price wanachotakiwa Wakurugenzi na Wakuu wa Wilaya ni kufuatilia guided price iliyotolewa na Wizara ya Kilimo as indicated price kwenye masoko na wasiwabughudhi wanunuzi. (Makofi)

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza: - Je, upi mpango wa Serikali katika kukwamua zao la zhai ambalo ni miongoni mwa mazao ya kimkakati yenye changamoto nyingi nchini?

Supplementary Question 3

MHE. JUSTINE L. NYAMOGA: Mheshimiwa Spika, aHsante kwa nafasi hii.

Kwanza nashukuru sana kwamba Waziri wa Kilimo ametembelea shamba la chai pale Kilolo Jumamosi wiki iliyopita na kujionea mwenyewe lile pori ambalo nimekuwa nikilisema hapa. Na kwa kuwa Benki ya Kilimo iko tayari na ina fedha tayari kwa ajili ya kukopesha mwekezaji yeyote, sasa je, ni lini ule mchakato wa kutafuta mwekezaji utaanza tena bada ya kuwa ulisimama katika kipindi hiki cha mwaka karibu mmoja uliopita? (Makofi)

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Kilolo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza Waziri wa Kilimo Profesa Mkenda amekuwepo huko wiki iliyopita akiwa pamoja na Mkurugenzi wa Tanzania Agricultural Development Bank. Baada ya muda mrefu kuhangaika kutafuta mwekezaji, position ambayo tunayo kama Wizara ya Kilimo na ambayo tutaenda kuitekeleza ni kuanzisha special purpose vehicle ambayo shareholding structure itawahusisha wakulima wadogo na Tanzania Agricultural Development Bank kwa sababu wao ndio wanaleta mtaji na wao wataleta menejimenti.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nimhakikishie Mbunge kwamba ule mpango wa kuhangaika kutafuta mwekezaji wa nje tumeachana nao, tutatumia our own resources kufufua hilo shamba na tutaweka menejimenti ambayo ita- run, kwa sababu tumefanya majaribio kwenye Vyama vya Ushirika vya KAKU, Mbogwe na Chato tumefanikiwa.

Kwa hiyo, huu ndio utakuwa mwelekeo kwenye maeneo ambayo tutaweka mitaji, tutaanzisha special purpose vehicle, halafu tutaendelea kufanya biashara na ushirika utashindana. (Makofi)