Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Primary Question

MHE. STANSLAUS H. NYONGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Bypass ya Mji wa Maswa?

Supplementary Question 1

MHE. STANSLAUS H. NYONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwanza niishukuru sana Serikali kwa kuingia mkataba na mkandarasi huyu ili ujenzi uanze tarehe Mosi, Julai, kwa hilo kwanza napongeza sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili, ili niweze kuuliza maswali yangu mawili ya nyongeza, ni kwamba swali la kwanza; mikataba mingi ya ujenzi inasainiwa, lakini ujenzi unapopita maeneo yao, watu wanakuwa hawajalipwa compensation ili ujenzi ule uanze. Je, Serikali imekwishalipa compensation kwa wale watu wa sehemu ambako mradi huo unapita ili mradi huo uanze?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; mkandarasi huyu waliyepatiwa wa CHICO Construction ndio huyu huyu aliyejenga barabara ya kilometa 50 kutoka Mwigumbi kwenda Maswa. Barabara hii hata kabla haijakabidhiwa ilikuwa tayari imekwishaanza kupata mashimo na kuharibika. Mkandarasi huyo sasa hivi anafanya mobilization ku-bypass ili aanze kukarabati barabara ambayo hata bado hajaikabidhi. Je, Serikali ina uhakika gani kwamba baada ya kumpa mkandarasi huyu kazi hiyo ya bypass atajenga kwa kiwango kinachostahili? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Nyongo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, utaratibu wa Serikali ni kwamba barabara haiwezi kuanza kujengwa kama wananchi hawajalipwa fidia katika eneo hilo. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kabla barabara haijaanza kujengwa, wananchi watalipwa fidia na baada ya hapo ndiyo ujenzi utaendelea; hilo namuondolea wasiwasi.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, anauliza mkandarasi ambaye amepewa barabara hii, M/S CHICO, kwamba alijenga barabara kutoka Mwigumbi kwenda Maswa na imeharibika. Bahati nzuri mwenyewe Mheshimiwa Mbunge amesema kwamba barabara hii haijakabidhiwa, utaratibu ni kwamba ukipata kazi, unafanya kazi yako, kabla hujakabidhi kuna muda wa matazamio na lolote likitokea, kama kuna sehemu imeharibika, unapaswa kutengeneza kwa gharama zako. Ameshaelekezwa maeneo yote ambayo yameharibika ayarekebishe ili aendelee na kazi nyingine.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge, kwamba huyu tutamfuatilia na kumsimamia kwa ukaribu, kazi lazima ikamilike. Kama kuna mahali kuna shida tutawasiliana mara kwa mara na Mheshimiwa Mbunge ambaye yuko karibu na wananchi wake, ili fedha ya Serikali ifanye kazi ambayo imekusudiwa. Ahsante.

Name

George Ranwell Mwenisongole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. STANSLAUS H. NYONGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Bypass ya Mji wa Maswa?

Supplementary Question 2

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii ili kuuliza swali. Napenda kuuliza swali; ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya kutoka Igawa, Mbeya mpaka Tunduma, zikiwemo njia nne za Mbeya Bypass kwa ajili ya kupunguza msongamano uliopo pale Mbeya? Ahsante. (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwenisongole, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba barabara ambayo Mheshimiwa Mbunge ameitaja ni barabara muhimu sana na kwako Mbeya Mjini ni shida. Bahati nzuri mwezi uliopita tulikwenda kule Mbeya, kulikuwa na mgomo wa bajaji, pikipiki na daladala, shida ni kwamba kuna msongamano mkubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna mpango mkubwa wa Serikali wa kujenga barabara ya njia nne. Tunafanya mpango na majadiliano na Benki ya Dunia, tukipata fedha hiyo wakati wowote kuanzia sasa, barabara hii itajengwa ili kuweza kupunguza msongamano katika Mji wa Mbeya na maeneo ya jirani. Ahsante.