Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza ujenzi wa barabara ya kutoka Manyoni - Sanza - Chipanga - Bahi hadi Dodoma kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza, kwa kuwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ulishafanyika wa daraja la Sanza.

Je, nini commitment ya Serikali kuhakikisha kwamba inaanza kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa kipande cha barabara ambacho kitaunganisha daraja hilo?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; je, ni lini Serikali itawamalizia kuwalipa fidia wananchi wa vijiji vya Sanza Chicheho na Ikasi ili ujenzi wa daraja uweze kuanza? Ahsante sana (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Pius Stephen Chaya, Mbunge wa Manyoni Mashariki, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, katika jibu langu la msingi, ni kwamba tayari tumeshakamilisha upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa daraja na ujenzi huo utaanza mara moja, ikiwa ni pamoja na approach roads zenye urefu wa kilometa tisa upande wa Singida na kilometa tano nukta kadhaa upande wa Dodoma kwa ajili ya kuondoa changamoto iliyokuwepo kwa sababu hilo daraja liko chini. Kwa hiyo ujenzi utaanza mara moja.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili la fidia; daraja hili limehamishwa mahali lilipokuwa na barabara inajengwa upya sehemu ya hilo daraja. Tayari fidia, atakubaliana nami Mheshimiwa Mbunge, Wizara na Serikali tumeshalipa zaidi ya milioni 300.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya wananchi kulalamika tumefanya tathmini upya na kuona kwamba zinahitajika si zaidi ya milioni 65. Tayari mchakato wa kupata hizo fedha unaendelea ili kabla ya kuanza ujenzi tumalize kwanza kuwalipa wananchi fidia halafu tutaanza ujenzi wa daraja hilo. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Manyoni kwamba fidia tayari tumeshafanya tathmini upya, tutawalipa, halafu tutaanza ujenzi wa hilo daraja na hizo barabara zake. Ahsante.

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza ujenzi wa barabara ya kutoka Manyoni - Sanza - Chipanga - Bahi hadi Dodoma kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Kwanza, naomba niipongeze Serikali kwa kutangaza barabara ambayo nilikuwa naipigania hapa Bungeni kwa muda mrefu ya kipande cha kilometa 25 kutoka Itigi kuelekea Noranga. Sasa, je, Serikali iko tayari kuongeza kipande kingine katika bajeti ijayo ya 2021/2022 angalau kufanya urefu uwe wa kutoshatosha? Barabara hii ni ndefu, ina kilometa 219.

NAIBU SPIKA: Unamaanisha bajeti ya 2022/2023 au? Kwa sababu hii si ndiyo tumetoka kuijadili sasa hivi?

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Naibu Spika, hapana, namaanisha bajeti iliyotangazwa ni hii ambayo inaishia Juni. Je, kuanzia Julai 2021/2022, Serikali iko tayari kuongeza kipande kingine ili barabara hii iweze kufanya vizuri zaidi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Yahaya Massare kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara zilizotangazwa zimetangazwa kwa bajeti ambayo tunaendelea kuitekeleza kabla ya tarehe 30 Juni na barabara anayoisema pia tumeitengea fedha kwa bajeti tutakayoanza kutekeleza Julai. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutaendelea na ujenzi kwa kipande kinachoendelea mpaka barabara itakapokamilika.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo bajeti tuliyotangaza ni kwa mwaka huu tunaoendelea nao kabla ya Juni, 30, lakini tumetenga pia fedha kwa ajili ya bajeti tunayoanza 2021/2022. Ahsante.