Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Primary Question

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa kiwango cha lami wa barabara ya Tanga – Mabokweni – Maramba – Daluni – Mtoni – Bombo – Magoma hadi Korogwe?

Supplementary Question 1

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, naomba kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hii imekuwa ikiahidiwa na Marais watatu waliopita. Je, Serikali haioni kwamba kutotekelezwa kwa ahadi za Marais wetu watatu ni kipindi kirefu sana? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; tunaishukuru Serikali kwamba kwa kipindi hiki sasa imetenga bilioni moja kwa ajili ya upembuzi yakinifu na usanifu. Je, Serikali inatuhakikishia kwamba kazi hii itaenda kufanyika na kukamilika kwa kiasi hiki cha fedha? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG.
GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dunstan Luka Kitandula, Mbunge wa Mkinga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba barabara hii imeahidiwa na Marais watatu kama alivyosema na ni kweli ni muda mrefu, lakini nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge wa Mkinga na wananchi wa Mkinga kwamba wawe na imani na Serikali na ndiyo maana hata fedha tumeonesha kiasi ambacho tumekitenga ili kutimiza ahadi hizo za Marais na awe na imani sana na Awamu hii ya Sita inayoongozwa na Rais wetu Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan. Naomba nimhakikishie kwamba itatekelezwa kama tulivyoahidi na tulivyopanga kwenye bajeti. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; nimhakikishie kwamba bajeti iliyotengwa kwa maana ya kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina itatosha kufanya kazi hii na kama ilivyopangwa kazi hii ya usanifu na upembuzi yakinifu itakamilika, ahsante. (Makofi)

Name

Florent Laurent Kyombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa kiwango cha lami wa barabara ya Tanga – Mabokweni – Maramba – Daluni – Mtoni – Bombo – Magoma hadi Korogwe?

Supplementary Question 2

MHE. FLORENT L. KYOMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi, viongozi wetu wa Kitaifa kwa nyakati mbalimbali wamefanya ziara ndani ya Wilaya ya Misenyi na kuahidi ujenzi wa barabara za lami. Barabara ya Mutukula kwenda Minziro lakini vilevile barabara kutoka Kadieli Kata ya Ishozi mpaka Gela njia panda. Je, ni lini Serikali itatimiza ahadi za viongozi wetu wapendwa? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Florent Kyombo, Mbunge wa Misenyi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli barabara ya Mtukula hadi Minziro iliahidiwa na anakubaliana na mimi kwamba kuna kazi tayari imeshanza. Baada ya kukamilisha kwa kiwango cha changarawe na kuifungua basi tutafanya kazi ya pili itakuwa ni kuisanifu kwa ajili ya kiwango cha lami.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara aliyoitaja ya pili ni barabara ambayo tayari ameshakuja mara kadhaa ofisini ni barabara ambayo ilikuwa inahudumiwa na Wakala wa Barabara (TARURA) na tayari tunafanya mawasiliano na wenzetu ili tuone namna ya kuipandisha hadhi lakini itategemea na wao watakavyoleta mapendekezo yao ili barabara hiyo kwa umuhimu wake iweze kuchukuliwa na TANROADS kama itakuwa imekidhi vigezo. Ahsante.

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya ujenzi wa kiwango cha lami wa barabara ya Tanga – Mabokweni – Maramba – Daluni – Mtoni – Bombo – Magoma hadi Korogwe?

Supplementary Question 3

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona na kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa kuna ahadi ya muda mrefu ya kujenga kwa kiwango cha lami barabara inayotoka Karatu – Kilimapunda – Mbulu, ahadi hii imekuwa ni ya muda mrefu sana.

Je, ni lini sasa Serikali mtatekeleza ahadi hiyo kwa kujenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG.
GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cecilia Paresso, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli barabara aliyoitaja ya kuanzia Karatu kuja Mbulu ni ahadi ya muda mrefu, lakini nataka nimhakikishie kwamba katika bajeti ijayo lakini hata mwaka huu barabara hii itatangazwa mara moja kuanzia kipande cha Mbulu kwenda Haydom ambayo ni sehemu ya barabara hiyo. Kwa hiyo, tayari Serikali imeanza kutekeleza hiyo ahadi. Ahsante. (Makofi)