Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza: - Je, ni lini Barabara ya kutoka Kibaoni – Kasansa – Muze – Ilemba – Kilyamatundu hadi Mlowo itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyogeza. Kwanza kabisa nipende kuipongeza na kuishukuru Serikali kwa kutujengea hilo daraja liligharimu zaidi ya karibu bilioni 17. Tunashukuru sana. lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza; Serikali sasa ina mpango gani wa kutujengea hata basi kuitengeneza hiyo barabara hata kwa kiwango cha changarawe ili wananchi waweze kupita katika barabara hiyo?

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali la pili ninaomba sasa commitment ya Serikali, kwa sababu barabara hiyo ni muhimu sana kwa uchumi wa Mikoa ya Rukwa, Katavi na Songwe. Ni lini sasa Serikali itaanza ujenzi wa barabara hiyo? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Bupe Mwakang’ata Mbunge wa Viti Maalum wa Mkoa wa Rukwa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii ni kweli kwa mwaka jana na mwaka huu ilikuwa imeharibika sana. Nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, hivi ninavyoongea madaraja yote yameshajengwa, bado madaraja mawili ambayo mkandarasi anakamilisha. Kwa sasa barabara hii inapitika vizuri kwa kiwango cha changarawe.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali la pili la Mheshimiwa Mbunge, kwamba ni lini tutaanza ujenzi; kama nilivyojibu katika jibu langu la msingi. Barabara hii tunatambua umuhimu wake ndiyo maana tayari tumeshakamilisha usanifu wa kina kwenye kilomita zote, na bado kilomita 27 ambazo wako tayari wanafanyia usanifu ili barabara yote ikamilike kwa usanifu na baada ya hapo ndipo ujenzi kwa kiwango cha lami utaanza.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia kwa niaba ya Wizara nimshukuru kwamba ameipongeza Serikali kwa kujenga Daraja la Mto Momba ambalo lilikuwa ni kikwazo kikubwa. Hiyo ndiyo adhma ya Serikali; na sasa mizigo yote kutoka Rukwa inapita daraja la Momba kwenye Mlowo. Ahsante.

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza: - Je, ni lini Barabara ya kutoka Kibaoni – Kasansa – Muze – Ilemba – Kilyamatundu hadi Mlowo itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa
Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi ya swali la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya mchepuo ya Morogoro Manispaa ambayo Mheshimiwa Naibu Spika unaifahamu na unaitumia kila mara unapokwenda Dar es Salaam ili kupunguza msongamano wa magari pale Msamvu? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG.
GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Ishengoma kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara anayosema ambayo itakuwa barabara ya by-pass ni barabara ambayo muhimu, binafsi nimepita na Mheshimiwa Ishengoma tumeongea naye. Ni kweli kwamba barabara hii ni muhimu na tutaingiza kwenye mpango ili iweze kujengwa kwa kiwango cha lami kupunguza msongamano wa kupita magari yote katikati ya Mji wa Morogoro. Kwa hiyo nimuhakikishie Mheshimiwa Ishengoma kwamba mpango huo upo na katika siku zinazokuja kadri ya fedha zitakapopatikana barabara hii itajengwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza: - Je, ni lini Barabara ya kutoka Kibaoni – Kasansa – Muze – Ilemba – Kilyamatundu hadi Mlowo itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kuna barabara ambayo inatoka Lumecha – Kitanda, Londo inakwenda mpaka Malinyi kutokea Lupilo, Ifakara na ipo katika Ilani ya Uchaguzi na barabara ile ya Serikali Kuu.

Je, Serikali inaweza ika-concentrate kuanza kuifungua ile barabara kutokea Kitanda – Londo mpaka Kilosa kwa Mpepo mpaka Malinyi ili ianze kupitika wakati utaratibu wa kuijenga kwa lami unaendelea?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Vita Kawawa Mbunge wa Namtumbo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara anayoisema ya Lumecha – Londo Kilosa kwa Mpepo – Malinyi hadi Ifakara na Mikumi ni barabara kuu kama alivyoisema. Tunafikiria kuifungua barabara hii ili iweze kutumia, na hasa kuanza na kipande ambacho kina miinuko mikali kati ya Londo na Kilosa kwa Mpepo. Ikishafunguka nadhani itapitika kwa kiwango cha lami. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge avute subira Serikali itafute fedha ili hapo paweze kukamilika na kupatengeneza vizuri, kwa sababu ndiyo changamoto kubwa ya hiyo barabara kushindwa kupitika muda wote wa mwaka. Ahsante.

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza: - Je, ni lini Barabara ya kutoka Kibaoni – Kasansa – Muze – Ilemba – Kilyamatundu hadi Mlowo itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Iko nia ya Serikali ya kujenga barabara ya kutoka Mkiwa kwenda Noranga kilometa 56.9 ambayo ilikuwa imetangazwa mwaka 2017, na sasa hivi katika bajeti iliyopita alisema kwamba wataitangaza. Je, ni lini sasa barabara hii itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG.
GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Massare kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara iliyotajwa ni barabara ambayo imepata kibali na taratibu zote zimekamilika; muda wowote itatangazwa kuanza kujengwa kwa kiwango cha lami. Mheshimiwa Mbunge tumeongea naye mara kadhaa, pamoja na Mbunge wa Chunya Mheshimiwa Kassaka.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii inatarajiwa kutangazwa muda wowote kwa sababu imeshapata kila kitu na imekamilika, kwa maana ya kutangazwa. Ahsante.

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza: - Je, ni lini Barabara ya kutoka Kibaoni – Kasansa – Muze – Ilemba – Kilyamatundu hadi Mlowo itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 5

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Swali langu ni kwamba, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba Daraja la Mto Luhuhu linalounganisha Wilaya ya Nyasa na Ludewa linakamilika? Kwa sababu kwa sasa hata ile Pantoni iliyokuwa inatumika nayo imeharibika.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG.
GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mhandisi Stella Manyanya Mbunge wa Nyasa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, daraja analolisema linaunganisha Wilaya ya Nyasa na Wilaya ya Ludewa. Katika bajeti yetu ni kati ya madaraja ambayo yamepangiwa fedha kwa ajili ya kujengwa katika bajeti inayokuja. Kwa hiyo, nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mara bajeti itakapoanza kutekelezwa daraja hili litaendelezwa kujengwa ili liweze kukamilika. Ahsante.