Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Soud Mohammed Jumah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Donge

Primary Question

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH aliuliza: - Je, Taasisis ngapi zimeweza kujisajili hadi sasa na Mfuko wa Mabadiliko ya Tabianchi (Green Climate Fund) nchini, na miradi mingapi imeshaombewa kupitiwa mfuko huo?

Supplementary Question 1

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa kuna taasisi tatu hapa nchini za NEMC, Wizara ya fedha pamoja na TAMISEMI, zimeanza mchakato karibu miaka sita mapaka kumi iliyopita, na mpaka leo hazijaweza kukamilisha utaratibu wa kuweza accredited.

Je, Wizara au Ofisi Makamo wa Rais Mazingira, ina mpango gani wa kuweza kuzihamasisha na kuzijengea uwezo taasisi hizi ziweze kukamilisha mchakato huu na kuweza kufaidika na fedha hizi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, kwa vile Zanzibar hakuna taasisi hata moja ambayo imeanza mchakato huu. Je, kuna utaratibu gani au mikakati gani ambayo imepangwa na Ofisi ya Makamo wa Rais Mazingira, kuweza kuzijengea uwezo taasisi za Zanzibar na kuzihamasisha ziweze kuanzisha mchakato wa kujiunga na mfuko huu wa taibanchi. Ahsant sana. (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS
(MUUNGANO NA MAZINGIRA): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali na Mhesimiwa Soud Mohammed Jumah kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa mwenyekiti, ni kweli katika hizi fedha za mifuko hii miwili ya Adaptation na Green fund, hizi mara nyingi sana tushindwa kuzi – access kwa muda mrefu, hata hivyo Ofisi ya Makamo wa Rais Muungano na Mazingira, imeweza kuhakikisha kwamba katika kipindi cha hivi karibuni imejitahidi kufanya kazi yake kubwa vya kutosha, na tushukuru sasa hivi, kwa mfano, NEMC imefanikiwa kupata fedha kutoka mfuko wa Adaptation Funds, ambao ni wastani wa shilingi billion 6 ambazo hizi tupo katika mchakato na Wizara ya fedha kuweza kuzi – access vizuri ili ziweze kufanyakazi nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, tunaendelea kuzijengea uwezo taasisi hizo. Tunafahamu kwamba TAMISEMI walianza mchakato takriban miaka mitatu, na bado kuna suala la capacity tunaendelea kulifanyia kazi. Kwa upande huu wa Zanzibar, juzi tulikuwa na ziara kule Zanzibar (Unguja na Pemba) na jana tulimaliza. Miongoni mwa jambo kubwa sana tulokubaliana nalo ni suala zima la kuangalia jinsi gani tutafanya kazi kwa pamoja katika upande wa kimazingira, kwa sababu jambo la mazingira linakata maeneo yote mawili.

Mheshimiwa mwenyekiti, hili naomba nikuhakikishie Mheshimiwa mbunge, mimi na dada yangu kule Mheshimiwa Saada Mkuya, ambae anahusiana na upande wa Mazingira kwa upande wa Zanzibar, tutafanya kila liwezekanalo kwa umoja wetu. Na hivi sasa Mkurugenzi wetu wa Mazingira anaitwa Dkt. Andrew Komba hivi muda huu ninayozungumza yuko Zanzibar akifanya kikao na wakuu wa Mikoa kule Pemba, katika ajenda kubwa ya kuangalia jinsi gani tutafanya ajenda ya pamoja ya mazingira ndani ya nchi yetu.