Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa barabara kutoka Mnivata hadi Masasi kupitia Newala kwa kiwango cha lami utaanza?

Supplementary Question 1

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi.

Kwa kuwa, barabara hii ni muhimu sana kwa ajili ya usafirishaji wa zao la korosho na kwa kuwa bajeti ya mwaka jana zilitengwa kiasi cha fedha na mwaka huu imetengwa bilioni tatu, naomba sasa nijue Je, ni lini Serikali itatangaza barabara hii ili apatikane Mkandarasi wa kuanza kipande kilichobaki cha kilometa 110.

Pili, kwakuwa kilometa 50 ambazo zimeshajengwa kwa awamu ya kwanza bado kuna kazi chache zimebaki Serikali inatuhakikishia mpaka lini kipande hiki kitakuwa kimekamilika kwa asilimia 100? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Abdallah Dadi Chikota, Mbunge wa Nanyamba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii imetengewa fedha ambayo mara tu fedha itakapoanza kutumika za bajeti ambayo imepitishwa na Bunge lako barabara hii itatangazwa ili ianze kuendelea kipande cha Mnivata Tandahimba kwenda Newala, ameuliza barabara ambayo imejengwa ya Mtwara hadi Mnivata yenye kilometa 50 ni kweli haijakamilika kabisa lakini tumetenga shilingi bilioni Tatu kwa ajili ya kukamilisha barabara hiyo. Ahsante.

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa barabara kutoka Mnivata hadi Masasi kupitia Newala kwa kiwango cha lami utaanza?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza.

Kwa kuwa barabara ya Mwigumbi Maswa imejengwa chini ya kiwango na imeanza kubomoka bomoka. Je, ni lini Serikali itarudia ujenzi huo? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther, Mbunge kama Mheshimiwa Naibu Spika, ni kawaida barabara zikishajengwa baada ya muda hasa muda wake unapokuwa umekwisha zinachakaa na hivyo kufanyiwa mategenezo kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hiyo itaingizwa kwenye mpango wa ujenzi mara tu fedha itakapopatikana hasa katika awamu tunazoziendea, kwa sababu ni taratibu kwamba tunafanya tathmini kuangalia gharama halafu barabara hiyo itafanyiwa rehabilitation kubwa. Ahsante.

Name

Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa barabara kutoka Mnivata hadi Masasi kupitia Newala kwa kiwango cha lami utaanza?

Supplementary Question 3

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA: Mheshimiwa Naibu Spika, hii barabara ya Tandahimba ni barabara ya muda mrefu sana imeahidiwa kwa muda mrefu sana tangu wakati wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Serikali itakuwa imeamua lini kufanya kwa vitendo kutimiza ahadi zake kwa sababu barabara hii ni ya muda mrefu sana? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ally Mchungahela Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli barabara hii imeahidiwa muda mrefu lakini Mheshimiwa Mbunge atakubaliana nami kwamba barabara hii tayari Serikali imeshaanza kutekeleza kwa vitendo ambapo kilometa 50 zimeshajengwa na katika bajeti tunayoenda, bado tunaendelea tumetenga Billioni tatu kwa ajili ya kuanza barabara hii ya Mnivata kwenda Tandahimba. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mara bajeti itakapoanza kutekelezwa barabara hii itatangazwa na itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa barabara kutoka Mnivata hadi Masasi kupitia Newala kwa kiwango cha lami utaanza?

Supplementary Question 4

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kumekuwa na ahadi ya muda mrefu ya kujenga barabara katika Mji Mdogo wa Karatu kwa kiwango cha lami toka Serikali ya Awamu ya Nne na Awamu ya Tano.

Je, ni lini sasa ahadi hiyo itatekelezwa kujenga kilometa 10 za lami katika mji dogo wa Karatu?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cecilia Paresso kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara za Mjini Karatu zitajengwa kulingana na upatikanaji wa fedha kadri Serikali itakavyopata fedha. Kwa hiyo, nimhakikishe Mheshimiwa Mbunge kwamba Wizara yangu ya Ujenzi na Uchukuzi ikisaidiana na Wizara ya TAMISEMI tutahakikisha kwamba barabara hizi ambazo ni ahadi za viongozi na zipo kwenye Ilani zinajengwa kwa kiwango cha lami kama zilivyoahidiwa. Ahsante.

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa barabara kutoka Mnivata hadi Masasi kupitia Newala kwa kiwango cha lami utaanza?

Supplementary Question 5

MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa niulize swali moja la nyongeza.

Barabara ya kutoka Katumba - Suma – Mwakareli - Luwanga - Mbambo mpaka Tukuyu yenye urefu wa Kilometa 82, imeanza kujengwa kipande cha kutoka Luhangwa – Mbambo – Tukuyu.

Je, ni lini kipande cha kutoka Luhangwa - Mwakareli - Suma - Katumba kitajengwa? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwakibete kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii ni mwendelezo wa ujenzi ambao unaendelea, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika bajeti hii kuna fedha ambayo imetengwa ambapo barabara hii ya Katumba hadi Luhangwa itaendelea kujengwa, kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge wa Busokelo pamoja na wananchi wa Busokelo kwamba barabara hii itaendelea kujengwa kadri fedha itakapokuwa inapatikana na tayari imeshaanza kwa hiyo Serikali itaendelea kuijenga barabara hii. Ahsante.

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa barabara kutoka Mnivata hadi Masasi kupitia Newala kwa kiwango cha lami utaanza?

Supplementary Question 6

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipatia nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Barabara ya Bugene, Karagwe kupitia pori la Kimisi hadi Ngara Mheshimiwa Hayati Magufuli akiwa Karagwe mwaka huu mwezi wa Januari alitangaza ianzwe kuwekwa lami naomba kujua utekelezaji wake umefikia wapi? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Oliver Semuguruka Mbunge Viti Maalum kama ifuatavyo ni kweli barabara hii iliahidiwa na ilikuwa ni agizo la Mheshimiwa Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli barabara hii imetengewa fedha katika bajeti iliyopitishwa kwa hiyo itakuwa ni kati ya barabara ambazo zitaanza kutekelezwa kujengwa kwa kiwango cha lami mara bajeti itakavyoanza kutumika ahsante. (Makofi)