Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Bandari ya Uvuvi na kununua Meli ya uvuvi katika Mkoa wa Mtwara?

Supplementary Question 1

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, kwa majibu haya Mheshimiwa Waziri ni wazi kwamba suala la ujenzi wa bandari na ununuzi wa meli katika Mkoa wa Mtwara bado. Sasa nina maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la kwanza; kwa kuwa wavuvi ili waweze kutengeneza vyombo vyao, wanahitaji kununua miti ama mbao kutoka kwa wauza mbao ambao TFS wanatoa kibali kwao. Nataka kujua Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha inawapa vibali wavuvi ili waweze kukata ile miti na kutengeneza vyombo kuepusha gharama inayopatikana kwa kwenda kununua kule kwa wauza mbao. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili; kwa kuwa hakuna uelekeo wa sasa hivi wa kuonekana kutajengwa Bandari ya Uvuvi pamoja na ununuzi wa meli katika Mkoa wa Mtwara, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha inawawezesha wavuvi wa Mtwara kupata vyombo vya kisasa vile vya fibbers nakushukuru. (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Tunza Issa Malapo, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la kwanza ni upatikanaji wa mbao na kwa kuwa vibali vinatoka TFS, Wizara ya Maliasili na Utalii, naomba nichukue rai hii ya Mheshimiwa Mbunge na nataka nimhakikishie yeye na wavuvi wote ya kwamba ndani ya Serikali tutalizungumza jambo hili ili kuweza kuona unafuu wa hao wavuvi ambao wanahitaji mbao 10 hadi 15 waweze kuzipata kwa urahisi kwa ajili ya ku-repair au kutengeneza vyombo vipya kwa kuwa ikizingatiwa wao hawaendi kufanya biashara bali wanakwenda kutengeneza vyombo kwa ajili ya matumizi yao. Kwa hivyo, hili ni jambo jema na nalichukua kwa ajili ya utekelezaji wake.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili ni suala la upatikanaji wa fibbers. Tunaanzisha upya Shirika letu la TAFICO na moja ya hadidu za rejea za kuhakikisha TAFICO mpya iweze kufanya vyema ni kuingia ubia kwa maana ya PPP na Sekta Binafasi na moja ya jambo tutakalokwenda kulikazania kwa huyo mtu atakayekuja kwa ajili ya PPP ya ubia ni kuhakikisha atuoneshe dalili na matumaini ya pamoja na kuvua lakini upatikanaji wa vyombo kuanzia katika ukanda wetu wote wa bahari hata na visiwani pia vilevile kwa lengo la kuimarisha upatikanaji wa samaki kwa kutumia vyombo vipya vya kisasa na hii ni pamoja na Mkoa wa Mtwara.