Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza: Je, mpaka sasa ni wawekezaji wangapi wamemilikishwa ardhi na kupata Hati kupitia Kituo cha Uwekezaji TIC?

Supplementary Question 1

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza, nitakuwa tu na swali moja.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika taarifa za Benki ya Dunia za Easy Way of Doing Business moja wapo ya kikwazo kwa wawekezaji ni uchelewaji wa kupatikana hati kwa wakati na utaratibu uliopo ni kwamba ile Kamati ya Kugawa Ardhi ya Kitaifa inakaa mara nne tu kwa mwaka. Je, Serikali ipo tayari kurahisisha walau hiyo Kamati ikakaa hata kila mwezi ili wawekezaji wapate hati kwa wakati? (Makofi)

Name

William Vangimembe Lukuvi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ismani

Answer

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri na kwa niaba ya Wizara hiyo, ningependa kujibu swali la Mheshimiwa Chumi, Mbunge wa Mafinga Mjini la nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Kanuni zilikuwa zinataka Kamati hii ikutane mara nne kwa mwaka na ndivyo walivyokuwa wanafanya lakini kutokana na ripoti hiyo na outcry ya wawekezaji na umuhimu wa kuharakisha uwekezaji, kwa sababu Kamati hii inaundwa na mimi, nimeelekeza sasa Kamati hii ikutane kila mwezi badala ya miezi minne. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, na kuanzia Awamu hii ya Sita wameshaanza kukutana mara moja kila mwezi na mwezi uliopita wamekutana kila wiki na ndio maana imewezesha katika maombi 174 yaliyowasilishwa katika Awamu ya Sita ya Mheshimiwa Rais Samia, tayari maombi 173 yameshapata vibali na yameshaandikiwa hati za uwekezaji na tayari zimeshakabidhiwa kwa EPZA na TIC kwa ajili ya utekelezaji. (Makofi)