Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Rashid Abdalla Rashid

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiwani

Primary Question

MHE. RASHID ABDALLA RASHID aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi katika Jimbo la Kiwani ili kuepusha wananchi kufuata huduma za Polisi masafa marefu?

Supplementary Question 1

MHE. RASHID ABDALLA RASHID: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimshukuru Naibu Waziri kwa majibu mazuri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza kwa kuwa eneo tayari lipo na kwa kuwa nafahamu kwamba kuna matofali ya kutosha katika Kambi ya Mfikiwa yaliyobaki kwa ajii ya ujenzi wa nyumba za Polisi Mfikiwa na mimi nikiwa mdau wa upatikanaji wa matofali hayo.

Je, ni lini Wizara itatupatia matofali hayo ili kwa kushirikiana na wananchi wangu wa Jimbo la Kiwani tuweze kuanza ujenzi wa kituo hicho?

Swali la pili, wananchi wa Shehia ya Kendwa kwa kushauriwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Kusini Pemba walitakiwa waanzishe Jengo kwa ajili ya polisi jamii na wananchi hao kwa kutii walianzisha jengo hilo ambapo sasa lina miaka nane.

Je, ni lini Wizara italimaliza jengo hilo ili wananchi waweze kupata huduma?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Rashid Abdalla, Mbunge wa Jimbo la Kiwani kutoka Kusini Pemba.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza linazungumzia kuhusu matofali; ni kweli katika eneo lile la Mfikiwa yapo matofali na matofali yale jumla yake ni 32,000 na matofali yale yaliletwa pale kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za askari makazi ya askari pale Mfikiwa na siyo matofali tu, lakini yapo na mabati ipo na rangi. Lakini kwa bahati nzuri au bahati mbaya ikafika wakati kidogo tukapungukiwa na fedha za kutosha kwa ajili ya kuendeleza ujenzi huu.

Kwa hiyo, matofali haya nimwambie Mheshimiwa Mbunge kwamba hayapo tu kwamba maana yake kazi imekwisha, kazi ya ujenzi wa nyumba zile azma ya Serikali iko pale pale, kwa hiyo, kikubwa nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba aendelee kustahimili tupo mbioni tutahakikisha kwamba kwa kushirikiana yeye na wadau wengine werevu tupate matofali na vifaa vingine vya kutosha ili tukajenge Kituo cha Polisi hapo Kiwani.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo nimwambie tu kwamba azma ya Serikali ni kuendeleza kujenga nyumba hizi na nyumba hizi zipo katika hali ya kujengwa kwa sababu tayari ipo nyumba moja imeshaanza kujengwa na imeshafikia katika hatua ya lenta.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, je, ni lini sasa Serikali itamaliza boma lile la polisi jamii. Kwanza nichukue fursa hii nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwa kazi kubwa na nzuri ambayo anaifanya katika Jimbo la Kiwani, kwa sababu amekuwa ni mdau mzuri ambaye anatusaidia Serikali hasa katika masuala ya ulinzi na usalama, hiki kituo ambacho kinazungumzwa cha polisi jamii amesaidia kwa kiasi kikubwa kuhakikisha kwamba anasaidia wananchi kuweza kupata huduma hizi. Kwa hiyo kikubwa nimwambie tu kwamba tutajitahidi katika mwaka ujao wa fedha tuweke hilo fungu kwa ajili ya kumsaidia kumalizia hili boma ama hiki kituo ambacho kimeshaanza cha askari jamii katika Shehia hii ya Kendwa. Nakushukuru.

NAIBU SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Naibu Waziri nilikuwa naangalia kwenye jibu la msingi linaonesha kwamba huko Kiwani mpaka sasa hivi hakuna eneo lililotengwa; wakati huo huo kuna mahali kuna matofali yamewekwa na ujenzi umefika mahali. Sasa hebu fafanua kidogo, haya matofali yako wapi ili nijue swali la nyongeza la Mbunge linaendana na hili jibu la msingi au hapana?

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, swali aliloliuliza kwamba kule Kusini Pemba kuna eneo la tuseme ni Kambi ya Askari Polisi panaitwa Mfikiwa, pale Mfikiwa Serikali kupitia Jeshi la Polisi iliamua ijenge nyumba za makazi ya askari polisi yaani Mfikiwa na huko Jimboni kwake ni mbali kidogo.

Kwa hiyo, kilichokuja kuamuliwa kwamba kuna matofali yale yeye ameona kwamba yako kwa muda mrefu yamekaa, kwa hiyo, anaona kwanini Serikali yale matofali yasichukuliwe yakapelekwa Kiwani ili wananchi wa Shehia za Jombwe, Kendwa, Muwambe, Mchake, Mtangani, Kiwani wajengewe kituo kile cha polisi sasa yale matofali azma ya Serikali ilikuwa ni kujenga nyumba za askari na kila kitu kipo tulipungukiwa kidogo na fedha ndicho ambacho anataka apelekewe yale matofali tukamwambia kwamba tutamfanyia maarifa tumpelekee matofali mengine.

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RASHID ABDALLA RASHID aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi katika Jimbo la Kiwani ili kuepusha wananchi kufuata huduma za Polisi masafa marefu?

Supplementary Question 2

MHE. JULIANA D. SHONZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kituo cha polisi cha Itaka ambacho kinahudumia kata zaidi ya tano ikiwepo kata ya Nambizo pamoja na Halungu kinakabiliwa na changamoto kubwa sana kwanza jengo lake limechakaa, lakini pili hakuna pia vitendea kazi lakini kama haitoshi kituo kile cha polisi kina polisi wanne tu. Naomba kufahamu Serikali imejipanga vipi katika kukabiliana na hiyo changamoto? Ahsante.

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, Kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Juliana Shonza kama ifuatavyo; Serikali tunafahamu na tunatambua changamoto iliyoko katika Jeshi la Polisi na tunafahamu kwamba bado kuna vituo vimechakaa, tunafahamu kwamba tuna changamoto ya vitendea kazi, lakini pia tunafahamu kwamba tuna baadhi ya upungufu wa watumishi katika Jeshi. Kikubwa nimwambie Mheshimiwa aendelee kutustahimilia kwa sababu hatua za kuhakikisha kwamba tunachanganua ama tunatatua hii changamoto ama hizi changamoto tumeshazianza zikiwemo za uajiri, za upatikanaji wa vitendea kazi na za kurekebisha majengo yaliyochakaa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo kubwa nimuombe tu Mheshimiwa aendelee kustahimili sisi kama Serikali kama Wizara tupo mbioni kuhakikisha kwamba watengenezea mazingira mazuri wananchi kwa ajili ya kupata huduma nzuri za ulinzi na usalama.

Name

Khalifa Mohammed Issa

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Mtambwe

Primary Question

MHE. RASHID ABDALLA RASHID aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi katika Jimbo la Kiwani ili kuepusha wananchi kufuata huduma za Polisi masafa marefu?

Supplementary Question 3

MHE. KHALIFA MOHAMED ISSA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana; kama ilivyo vituo vingi vya polisi vilivyochakaa, Kituo cha Matangatuwani kilichoko katika Jimbo la Konde Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba kimechakaa na kwa kweli ni kibovu, ikinyesha mvua ni bora ukae chini ya mwembe utapata stara kuliko Kituo cha Matangatuwani.

Je, ni lini Serikali itakifanyia ukarabati mkubwa kituo hiki cha Matangotuwani?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Khalifa Mohamed kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nichukue fursa hii nimpongeze sana Mheshimiwa Khalifa amekuwa ni mdau wetu muhimu wa kutusaidia kwanza kutuonesha maeneo ambayo tunatakiwa sisi kama Serikali tuyafanyie marekebisho, lakini pia amekuwa mstari wa mbele kuhakikisha kwamba anatoa hata kilicho mfukoni kwake au katika Mfuko wa Jimbo kuhakikisha kwamba anawasaidia wananchi katika kupata huduma za ulinzi na usalama, hili nimpongeze sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kikubwa nimwambie kwamba nirejee tena kwamba bado tunatambua kwamba kuna baadhi ya changamoto ambayo sisi ni sehemu ya wajibu wetu kuhakikisha kwamba tunazitatua ili kuhakikisha kwamba wananchi wetu wanapata huduma nzuri za kiulinzi na usalama. Kituo ambacho anakizungumza ni kweli kipo na mimi binafsi nimefika na hali nimeiona, lakini kikubwa nimwambie hata kama akinifaa kwenye bajeti ambayo tumeiwasilisha tumeisoma hivi karibuni tumezungumzia namna ambavyo tunaenda kurekebisha vituo vya polisi na nyumba na baadhi ya huduma nyingine ili sasa wananchi waweze kupata huduma bora za kiulinzi na usalama. Nimwambie tu kwamba na yeye ni miongoni mwa vituo ambavyo tutajitahidi turekebishe ili tuone namna ambavyo na wao wanapata huduma nzuri. Nakushukuru.

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. RASHID ABDALLA RASHID aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi katika Jimbo la Kiwani ili kuepusha wananchi kufuata huduma za Polisi masafa marefu?

Supplementary Question 4

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi; Kituo cha Polisi Nanyamba kilijengwa huko nyuma kwa ajili ya kuhudumia Tarafa ya Nanyamba lakini sasa hivi Halmashauri ya Mji wa Nanyamba ni Makao Makuu ya Halmashauri hiyo mpya na kuna ongezeko la watu na kituo hicho kimechoka na keshokutwa nitakabidhi bati 70 kwa ajili ya kukarabati.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuunga jitihada zetu kufanya ukarabati mkubwa wa kujenga Kituo kipya cha Polisi Nanyamba?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, naomba sasa nijibu swali la Mheshimiwa Chikota kama ifuatavyo:-

Kwanza nimpongeze sana kwa juhudi ambazo anazifanya za kutusaidia na ninajua anafanya haya kwa sababu aliwaahidi wananchi kwamba atawatumikia na atawasaidia kuhakikisha kwamba wanapata huduma bora.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, azma ya kutoa mabati na vingine ambavyo utahakikisha kwamba wananchi wanahitaji aendelee kufanya hivyo na sisi tuko pamoja na yeye.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimwambie tu kwamba zipo jitihada ambazo sisi kama Serikali kama Jeshi la Polisi tuna mpango wa kufanya si kituo hiki tu cha alichokitaja, lakini na vituo vingine. Kwa hiyo, kikubwa tumwambie kwamba tutaangalia na bajeti itakavyoturuhusu, lakini tumwahidi kwamba moja ya miongoni mwa maeneo ambayo tutayapa kipaumbele kuhakikisha kwamba wananchi wanapata kituo bora na kukifanyia marekebisho ni katika kituo chake cha Nanyamba. Nakushukuru.

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. RASHID ABDALLA RASHID aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi katika Jimbo la Kiwani ili kuepusha wananchi kufuata huduma za Polisi masafa marefu?

Supplementary Question 5

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru; ili askari wangu pale Iringa wapate utulivu na kuimarisha ndoa zao na familia wanahitaji makazi bora. Je, ni lini Serikali sasa itatujengea makazi bora ya askari katika Kituo Kikuu cha Polisi Iringa?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, Kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jesca Msambatavangu, Mbunge wa Iringa Mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze sana na yeye kwa juhudi kubwa ambayo anatusaidia katika kuhakikisha kwamba anawasaidia wananchi, lakini kikubwa nimuahidi kwamba katika mwaka wa fedha ujao tutajitahidi na tutahakikisha kwamba hili eneo ambalo yeye amelizungumza tulipe kipaumbele ili tu wananchi wa eneo hilo waweze kupata na wao huduma za ulinzi na usalama bila ya tatizo lolote, nakushukuru.