Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza:- Kituo cha Afya Upuge kinahitaji jengo kwa ajili ya mashine za mionzi yaani x-ray na ultra sound: - Je, ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya mashine hizo?

Supplementary Question 1

MHE. ATHUMAN A. MAIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri sana ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza.

Kwa kuwa Jimbo la Tabora Kaskazini na Tarafa mbili na kata 19 na lina kituo kimoja tu cha afya; je, ni lini Serikali itaunga mkono juhudi za Mbunge na wananchi za kujenga vituo vya afya katika Kata za Mabama, Usagari, Chitage ikiwa ni pamoja na kukiinua hadhi kituo cha Lolangulu? Swali la kwanza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa hospitali mpya ya Wilaya ya Uyui imevunja rekodi ya kuwapa referral wagonjwa kwenye kituo cha afya tena kwa bodaboda.

Je, Serikali lini itapeleka gari la wagonjwa la kubebea wagonjwa katika zahanati nyingine zote katika Jimbo langu? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Almas Athuman Maige, Mbunge wa Tabora Kaskazini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kimsingi Serikali kwa kuthamini afya za wananchi wa Halmashauri ya Uyui na Jimbo la Tabora Kaskazini imepeleka fedha ndani ya miaka mitatu zaidi ya bilioni 3.4 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Vituo vya Afya vitatu ambavyo vinatoa huduma, lakini ni kweli kwamba tunahitaji gari la wagonjwa katika Hospitali ya Halmashauri na Serikali imeshaweka mipango madhubuti kabisa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ya kutafuta magari ya wagonjwa kwa ajili ya Hospitali zetu za Halmashauri lakini pia kwa ajili ya vituo vya afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo naomba nimhakikishe Mheshimiwa Maige kadri mipango hii inavyoendelea kutekelezwa tutahakikisha tunapata gari la wagonjwa kwa ajili ya Hospitali ya Halmashauri, lakini pia kwa ajili ya vituo vya afya, lakini tunaamini kwamba tunahitaji kuwa na vituo vya afya katika kata zetu zote kama Sera na Mpango wa Maendeleo ya Afya ya Msingi yanavyoeleza likiwemo jimbo hili la Tabora Kaskazini kwa maana ya Halmashauri ya Uyui. Naomba nimhakikishe Mheshimiwa Mbunge kwamba kila mwaka tunaendelea kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka ujao wa fedha tumetenga fedha kwa ajili ya vituo vya afya 221, lakini tutaendelea kutenga fedha ili kuhakikisha jimbo hili pia linapata vituo vya afya.

Name

Yahya Ally Mhata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza:- Kituo cha Afya Upuge kinahitaji jengo kwa ajili ya mashine za mionzi yaani x-ray na ultra sound: - Je, ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya mashine hizo?

Supplementary Question 2

MHE. YAHYA A. MHATA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuuliza swali la nyongeza.

Kwa kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu ina vituo vya afya vinne ambavyo vyote havina gari la wagonjwa; je, ni lini Serikali itatuletea magari ya wagonjwa kwa vituo hivyo vya afya? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mhata, Mbunge wa Nanyumbu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo nimetangulia kujibu katika jibu langu la msingi Serikali kwa kuwa imeendelea kujenga vituo vya afya kwa wingi na Hospitali za Halmashauri automatically tumekuwa na uhitaji mkubwa sana wa magari ya wagonjwa katika vituo vyetu vya afya, lakini pia katika Hospitali za Halmashauri.

Mheshimiwa Naibu Spika, safari ni hatua tumeanza na hatua ya ujenzi wa vituo vya afya sasa tunakwenda na hatua ya kutafuta magari ya wagonjwa. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge Mhata kwamba tutakwenda kuangalia na kukipa kipaumbele Halmashauri ya Nanyumbu ili magari ya wagonjwa yakipatikana tuweze kupata gari hilo kwa ajili huduma bora za afya katika Halmashauri ya Nanyumbu. Nakushukuru. (Makofi)

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza:- Kituo cha Afya Upuge kinahitaji jengo kwa ajili ya mashine za mionzi yaani x-ray na ultra sound: - Je, ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya mashine hizo?

Supplementary Question 3

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, kwa kuwa Jimbo la Tunduru Kusini lina vituo vya afya vitatu kimojawapo ni kituo cha Afya Utina ambacho kinahudumia kata nne kata ya Lukumbule, Mchesi, Utina yenyewe, Tuwemacho, pamoja na Msicheo.

Je, ni lini Serikali itaboresha Kituo cha Afya Utina?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mpakate, Mbunge wa Tunduru Kusini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Kituo cha Afya cha Utina ni miongoni mwa vituo ambavyo Serikali imeendelea kuvifanyia tathmini na kuona namna bora zaidi ya kukiongezea miundombinu ya majengo, lakini pia vifaa tiba kwa hiyo, naomba nimhakikishie kwamba tayari Serikali inafanya tathmini lakini pia kutafuta fedha kwa ajili ya kukiboresha Kituo cha Afya cha Utina, ahsante sana.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza:- Kituo cha Afya Upuge kinahitaji jengo kwa ajili ya mashine za mionzi yaani x-ray na ultra sound: - Je, ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya mashine hizo?

Supplementary Question 4

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Kwa kuwa mimi Mbunge wa Jimbo la Nyang’hwale nilijitokea ujenzi wa kujenga nyumba ya mama na mtoto na jengo hilo tayari limeshakamilika lakini kuna mapungufu ya vifaa vya kutunzia watoto njiti yaani incubator.

Je, Serikali ina mpango gani sasa wa kusaidia Kituo cha Afya vifaa hivyo? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hussein Amar, Mbunge wa wa Nyang’hwale kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nianze kwa kumpongeza sana Mheshimiwa Mbunge kwa kujitolea kujenga Jengo la Huduma ya Afya ya Mama na Mtoto katika Jimbo lake la Nyang’hwale, huu ni mfano mzuri sana wa kuunga mkono nguvu za Serikali katika kuboresha huduma za afya, lakini naomba nimhakikishie kwamba tunatambua kwamba tunahitaji kuwa na vifaa tiba vya kutosha katika vituo vyetu hivi zikiwemo hizi incubator kwa ajili ya kusaidia watoto wachanga na mimi naomba nimhakikishie kwamba Serikali tunalichukua hili na lipo ndani ya uwezo wetu tutalifanyia kazi ili tuweze kupata incubator kwa ajili ya kuboresha huduma za afya katika kituo cha afya hiki kilichojengwa.

Name

Lucy Thomas Mayenga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza:- Kituo cha Afya Upuge kinahitaji jengo kwa ajili ya mashine za mionzi yaani x-ray na ultra sound: - Je, ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya mashine hizo?

Supplementary Question 5

MHE. LUCY T. MAYENGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana Hospitali Kuu ya Mkoa wa Dodoma imekuwa ikihudumia wagonjwa wengi sana hasa kutokana na kwamba idadi kubwa ya wananchi wamehamia hapa Dodoma, lakini huduma za afya katika hospitali hii haziridhishi sana kwasababu kwa mfano sasa hivi ultra sound katika huduma za kawaida, wale wagonjwa wa kawaida ultra sound haifanyi kazi kwa muda mrefu, wananchi wamekuwa wakilalamika, lakini pia vitu vingi sana vina kasoro mimi nilikuwa naomba kuuliza.

Je, ni lini Wizara hii itaweka mkakati wa kuwa wanaiangalia hospitali hii kwa karibu zaidi ili kuhakikisha inatoa huduma kama ambavyo wananchi wanataka? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Lucy, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeweka mikakati na inaitekeleza mikakati ya kuhakikisha kwamba hospitali zetu zote kuanzia Hospitali za Rufaa za Mikoa, Hospitali za Halmashauri, Vituo vya Afya lakini hata Hospitali za Kanda na ya Taifa zinatekeleza utoaji huduma bora kwa wananchi kwanza kwa kuhakikisha kwamba vifaa tiba vyote vinapatikana.

Kwa hiyo ninaomba nimhakikishe kwamba Hospitali hii ya Rufaa ya Mkoa nayo ni moja ya hospitali ambazo zinasimamiwa kwa karibu na tutaendelea kuhakikisha tunasimamia kwa karibu.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini changamoto ya vifaa tiba kama ultra sound naomba hili nilichukue tulifanyie tathmini kwa haraka tuone kwa nini ultra sound haifanyi kazi na kama kunahitajika ultra sound mpya basi Serikali itaweka mipango mizuri ya kununua mapema iwezekanavyo ili wananchi waweze kupata huduma bora. (Makofi)