Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Primary Question

MHE. JUMANNE A. SAGINI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha Kata za Bwiregi, Nyamimange, Buswahili na Sirorisimba zinapata maji ya Ziwa Victoria kwa kuwa Mradi wa Maji wa Mgango – Kyabakari – Butiama hautazifikia?

Supplementary Question 1

MHE. JUMANNE A. SAGINI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu fasaha ya Mheshimiwa Naibu Waziri. Lakini kama alivyosema mradi huu wa Mugango, Kiabakari, Butiama ndio kwanza wanaanza utekelezaji. Lakini, kwa kuwa Mji wa Musoma una maji mengi kiasi Wizara imewahi kutamka kwamba, wingi wa maji mpaka mabomba yanapasuka na umbali kutoka Musoma mpaka baadhi ya hizi Kata anazozitaja ni mfupi. Kwa nini Serikali isiamue kutoa maji Musoma Mjini na kuyafikisha vijiji vya Kata za Bukabwa, Nyankanga na Bwiregi, ikiwemo Ryamisanga, Kamugendi, Kitasakwa na Masurura? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini swali la pili, ni lini Serikali itaanza kutumia Mto Mara kama chanzo cha maji na kuyapeleka kwenye vijiji vya Kata za Nyamimange, Buswahili na Sirorisimba? Vikiwemo Wegero, Paranga, Kongoto, Buswahili, Nyambiri, Rwasereta na Kitaramanka. Ahsante. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, kama ambavyo ameeleza Mji wa Musoma una maji mengi ni kweli na ni dhahiri wakati wote huduma ya usambazaji maji huwa ni rahisi, ila kupata chanzo cha maji ndio kazi. So, kwa sababu tayari maji Mji wa Musoma ni mengi, nikuhakikishie Mheshimiwa Waziri tayari watendaji wetu wameweka katika mipango mikakati yao. Kadri tutakavyopata fedha, watahakikisha tunaendelea kutumia hiki chanzo tulichonacho, ili kunusuru yale mabomba yasiendelee kupasuka tutasogeza huduma kwa wananchi.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili ni matumizi ya Mto Mara. Naamini wakati wa usomaji wa bajeti hapa Mheshimiwa Waziri alijidadavua ya kutosha kwamba, maji yote ya mito mikuu huu ndio mpango wa kuona kwamba, Wizara inakwenda kuyatumia kwa vyanzo vya uhakika. Hivyo, Mto Mara pia, ni moja ya Mito ambayo kama Wizara, tunatarajia tuitumie kama chanzo cha uhakika. Hivyo, kulingana na namna tutukavyokuwa tunapata fedha, tutahakikisha mito na maziwa makuu yote tunakwenda kuyatumia kwa ufasaha. (Makofi)