Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza: - Je, nini kinazuia kukamilika kwa ujenzi wa Barabara ya Makutano – Sanzate kwa kiwango cha lami ambayo ina miaka tisa sasa?

Supplementary Question 1

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu ya Serikali, lakini nakuomba katika swali hili utupe msaada, maana sasa tunahitaji msaada wako.

Mheshimiwa Spika, mwezi wa pili mwaka huu 2021 tulikuwa na Waziri wa Ujenzi pale Butiama na Mkuu wa Wilaya ya Butiama alileta meseji ya Mama Maria kwamba anazunguka mno kutoka Musoma kuja kule mpaka apitie Kyabakari eneo lake limeshindwa kukamilika. Hii barabara Mkandarasi alipewa 2013 amalize 2015, miaka miwili hakumaliza;2015 -2017 hakumaliza; 2017-2019 hakumaliza; na 2019-2021 hajamaliza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, juzi tulikuwa na Waziri wa Ujenzi nikamwambia huyu hatamaliza. Sasa hii miradi inayopita Butiama pale kuna shida gani? Katika mradi ambao unatia aibu katika Mkoa wa Mara ni mradi huu wa barabara. Tunaomba msaada wako, yule Mkandarasi hatamaliza ule mradi, hilo ni suala la kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; Mkandarasi yule ameshindwa hata kwenda site mpaka sasa hivi. Toka tulipoongea na Waziri mwezi wa Pili, aliondoka mpaka leo. Barabara ya diversion ya kupita kwenye ile barabara haipitiki: Je, Waziri au Serikali ipo tayari kuwaambia TANROADS wa Mkoa wa Mara waende wakatengeneze diversion ya ile barabara? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ni mradi wa aibu, naomba msaada wako. (Makofi)

Name

Eng. Dr. Leonard Madaraka Chamuriho

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Getere, Mbunge wa Bunda kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba barabara hii ilipewa Mkandarasi huyu kwa muda mrefu uliopita na kama ilivyojibiwa katika jibu la msingi barabara hii ilipewa Wakandarasi hawa wazawa kama barabara ya kuwajengea uwezo. Tumekuwa tukiendelea kuwajengea uwezo hao lakini ilitokea changamoto mbalimbali ambazo tunaendelea kukabiliana nazo.

Mheshimiwa Spika, changamoto ambazo zilijitokeza ambazo zilikuwa ni ngumu kidogo kwa Wahandisi wapya wazawa ni baada ya kukutana na miamba ambayo ni dhaifu ambapo ilibidi wahangaike kutafuta miamba ambayo ni migumu kidogo. Kwa hiyo, tumekuwa tukishirikiana nao katika kuwajengea huo uwezo wa kutafuta miamba migumu ili kuweza kukabiliana na barabara hiyo.

Mheshimiwa Spika, nilichukua fursa hiyo ya kwenda mwenyewe kufanya ule ukaguzi na Mheshimiwa Mbunge tulikuwa naye na tukaahidiana kwamba tutaweza kulishughulikia jambo hilo kwa haraka ili usiwe ni mradi wa aibu.

Mheshimiwa Spika, hivi sasa tunaendelea vizuri na tayari tumeshamwambia yule Mkandarasi na ameshatekeleza kupata kokoto mbadala kutoka sehemu ambayo inapatikana na tunaendelea kuwahimiza ili waweze kumaliza katika hii miezi minne ambayo tumewaongezea.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, japokuwa ni kweli kwamba mradi huu umechelewa, tayari tumeshachukua hatua muhimu za kuhakikisha kwamba mradi huu utakamlika kwa wakati na usiwe mradi wa aibu na Wakandarasi wazawa tuendelee kuwajengea uwezo ili waendelee kuaminika katika miradi kama hii. Naomba kuwasilisha. (Makofi)

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza: - Je, nini kinazuia kukamilika kwa ujenzi wa Barabara ya Makutano – Sanzate kwa kiwango cha lami ambayo ina miaka tisa sasa?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii. Swali langu dogo ni hili kwamba: Je, Serikali itaanza lini ujenzi wa barabara inayotoka Chekereni – Kahe kwenda Mabogini? Hii ni barabara pekee ambayo ni bypass kwa magari ambayo yanatoka Dar es Salaam kwenda Moshi na hakuna bypass nyingine. Kwa hiyo, ni lini wataanza ujenzi huo ambao pia upo kwenye Ilani? Ahsante. (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Kimei, Mbunge wa Vunjo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba eneo ambalo anataja tunalifahamu, lakini tumeweka mipango ya Serikali kutafuta fedha. Tutaanza mara moja baada ya kupata fedha kujenga barabara hiyo ambayo ni muhimu ili kuendeleza shughuli za kiuchumi katika eneo lake. Ahsante.