Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwantumu Mzamili Zodo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU M. ZODO K.n.y. MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Mtwara?

Supplementary Question 1

MHE. MWANTUMU M. ZODO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa kuwa changamoto iliyopo Jimbo la Mtwara Mjini la kukosa Hospitali ya Wilaya linafanana sana na changamoto ya Jimbo la Kilindi: Je, ni lini sasa Serikali itapeleka pesa kujenga Hospitali ya Wilaya ya Kilindi ili kuokoa maisha ya akina mama wa Kilindi na Mkoa wa Tanga kwa ujumla? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Mpango wa Serikali ni kuhakikisha kwamba tunajenga Hospitali za Wilaya na Halmashauri katika Halmashauri zote ambazo hazina Hospitali hizo nchini kote. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika mwaka wa fedha ujao 2021/2022, Serikali imetenga shilingi milioni 500 kwa ajili ya Halmashauri zote ambazo hazina Hospitali za Halmashauri na fedha hizo zitapelekwa kwa ajili ya kuanza ujenzi wa hospitali hizo. Kwa hiyo, pamoja na Jimbo hili la Kilindi kwa maana ya Halmashauri ya Kilindi itatengewa fedha hizo kwa ajili ya ujenzi huo. Nakushukuru.

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. MWANTUMU M. ZODO K.n.y. MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Mtwara?

Supplementary Question 2

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa hii. Kwa kuwa sisi Mkoa wa Ruvuma tuna changamoto; hatuna hospitali kubwa ya kisasa ya Mkoa wa Ruvuma; sehemu iliyopo ni ndogo sana; sasa hivi ukitaka kuongeza jengo lazima ubomoe jengo linguine:-

Je, Serikali ipo tayari kutupangia na kutujengea Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, mipango ya Serikali ni kuhakikisha kila Mkoa unajengewa Hospitali ya kisasa ya Rufaa ya Mkoa na Hospitali za Rufaa za Mkoa ambazo zimeendelea kujengwa katika mikoa mipya zipo hatua za mwisho kabisa za ukamilishaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Mkoa wa Ruvuma una Hospitali ya Rufaa ya Mkoa, lakini hii ni ya siku nyingi nae neo ni dogo. Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa kushirikiana na Wizara ya Afya tutakwenda kufanya tathmini na kuona kama kuna uwezekano wa kuboresha hospitali iliyopo au kama kuna uwezekano wa kujenga hospitali nyingine mpya, tutapeleka taarifa katika Mkoa wa Ruvuma baada ya kufanya tathmini hiyo. Nakushukuru. (Makofi)

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU M. ZODO K.n.y. MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Mtwara?

Supplementary Question 3

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona na kunipa nafasi.

Katika Mkoa wa Arusha, Jimbo ambalo lina jiografia ngumu sana, ni Jimbo la Ngorongoro; na ukisema uweke tu Hospitali ya Wilaya pale Loliondo Mjini, Kata nyingine zenye umbali mkubwa hawawezi kupata hii huduma:-

Je, Serikali inalitizamaje Jimbo hili ili wale wananchi waweze kupata huduma nzuri za afya na zinazotakiwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, ni kweli kwamba Jimbo la Ngorongoro ni kubwa na jiografia yake ina changamoto, lakini Serikali imeweka mpango mkakati wa kuhakikisha kwamba kwanza kupitia Sera ya Mpango wa Maendeleo ya Afya Msingi kila Kijiji kinakuwa na zahanati, lakini pia kila Kata inakuwa na kituo cha afya na Halmashauri kuwa na Hospitali ya Wilaya.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kupitia mpango huo ambao utakwenda kujenga zahanati katika kila Kijiji, lakini pia kujenga vituo vya afya katika kila Kata, tutakwenda kutatua changamoto ya ukubwa na jiografia ya Jimbo la Ngorongoro na hivyo tutahakikisha kwamba huduma za afya zinawafikia ipasavyo wananchi wa Wilaya ya Ngorongoro.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.