Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Antipas Zeno Mgungusi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza:- Sehemu kubwa ya maeneo ya Kilimo cha Mpunga Malinyi imemegwa na Mamlaka ya Wanyamapori (TAWA) kwa Mipaka mipya iliyowekwa Mwaka 2017 bila maridhiano na Wananchi wa sehemu ya bonde la Kilombero. Je, Serikali haioni kuwa ni vema kufanya upya mapitio shirikishi kwenye mipaka ya eneo la Hifadhi?

Supplementary Question 1

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI: Mheshimiwa Spika, wakati tunasubiri hatma ya mgogoro wa bonde hilo na mipaka hiyo kutoka kwa Kamati ya Mawaziri Wanane maisha yaliendelea na wananchi wa kule tulilima na sasa mpunga uko tayari kwa ajili ya kuvunwa. Je, Wizara haioni haja ya kutoa ushirikiano na wananchi tuweze kuvuna mpunga huo?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Antipas, Mbunge wa Malinyi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli bonde hili kuna baadhi ya wananchi walikuwa wamevamia kwa ajili ya kilimo na sasa hivi ni kipindi cha mavuno. Kama alivyoomba Mheshimiwa Mbunge kwamba, Serikali inaweza ikawaruhusu na sisi kwa sababu, yale ni mazao na ili kuepuka njaa kwa wananchi wetu. Na kwa kuwa Serikali hii inawathamini wananchi, tutatoa vibali maalum ambavyo vitawasaidia kwenda kwenye maeneo hayo wavune kwa utaratibu ambao utasimamiwa na Serikali.

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza:- Sehemu kubwa ya maeneo ya Kilimo cha Mpunga Malinyi imemegwa na Mamlaka ya Wanyamapori (TAWA) kwa Mipaka mipya iliyowekwa Mwaka 2017 bila maridhiano na Wananchi wa sehemu ya bonde la Kilombero. Je, Serikali haioni kuwa ni vema kufanya upya mapitio shirikishi kwenye mipaka ya eneo la Hifadhi?

Supplementary Question 2

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, napenda kumshukuru Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Naibu wake, walipokuja jimboni kwetu walichukua hatua kuhusu askari wa TAWA, baadhi ambao walikuwa wakiwaonea wananchi wetu. Na kuwa Mheshimiwa Waziri aliahidi pale katika mkutano ule kwamba atatujengea soko la samaki, Ifakara, Kilombero. Naomba kuiuliza Serikali ni lini ahadi ile nzuri ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii itaanza?

Name

Dr. Advocate Damas Daniel Ndumbaro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Answer

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, nimpongeze Mheshimiwa Asenga kwa kuuliza swali hilo na kujali wananchi wake:-

Mheshimiwa Spika, mpango wa kujenga soko katika Daraja la Mto Kilombero upo katika bajeti ya Wizara katika mwaka huu 2021/2022. Kwa hiyo, mara baada ya bajeto hiyo kupitishwa mkakatin huo utaanza.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza:- Sehemu kubwa ya maeneo ya Kilimo cha Mpunga Malinyi imemegwa na Mamlaka ya Wanyamapori (TAWA) kwa Mipaka mipya iliyowekwa Mwaka 2017 bila maridhiano na Wananchi wa sehemu ya bonde la Kilombero. Je, Serikali haioni kuwa ni vema kufanya upya mapitio shirikishi kwenye mipaka ya eneo la Hifadhi?

Supplementary Question 3

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza:-

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Liwale inazungukwa na Pori la Selous, lakini sasahivi mkakati wa Serikali ni kuimarisha utalii wa picha badala ya utalii wa uwindaji na sisi kwenye Kanda ya Kusini kuanzia ukanda wa Kilwa mpaka Tunduru hakuna lango la utalii wa picha.

Je, Serikali haioni umuhimu wa kutuwekea sisi lango la utalii wa picha na sisi tuweze kunufaika na uwepo wa Selous?

SPIKA: Mheshimiwa kule Liwale unadhani lango lingeweza kukaa wapi kwa mfano?

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, palepale Liwale Mjini ndio panafaa kwa sababu, Kambi ya Selou iko palepale Liwale.

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka, Mbunge wa Liwale, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Kuchauka kwa maswali yake mazuri, lakini pia kwa kutambua wananchi wanaoishi Liwale. nimuahidi tu kwamba, mageti yanayohusiana na hii hifadhi yatafunguliwa kwa mwaka wa fedha 2021/2022 na mageti mengine yote.

Mheshimiwa Spika, hili naliongea kwa kujiamini kwa sababu, wiki iliyopita tu nilikuwa katika Mkoa wa Kilimanjaro, Same pamoja na Mwanga, pia kuna maombi hayo ya kufungua mageti mbalimbali kwenye Hifadhi ya Mkomazi. Kwa hiyo, niwaombe Waheshimiwa Wabunge kwenye maeneo yale ambayo yanahitaji kufunguliwa mageti ya ziada, ili kurahisisha watalii mbalimbali waweze kuingia na kurahisisha namna ya kuingia kwenye hifadhi, tutayafungua na bajeti hii itakayoanza keshokutwa imezingatia kufunguliwa kwa mageti hayo. Naomba kuwasilisha.