Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. NOAH L.S. MOLLEL aliuliza:- Je, ni lini Serikali itawalipa fidia ya kupisha njia kubwa ya umeme wananchi wa Vijiji vya Lengijape, Ilkurot na Olkejulenderit katika Jimbo la Arumeru Magharibi?

Supplementary Question 1

MHE. NOAH L.S. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, kwanza jina langu naitwa Noah Lemburis Sabutu Mollel.

Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza kabisa, namshukuru Naibu Waziri kwa kurekebisha kwamba siyo milioni 314 badala yake ni bilioni 314 ndiyo inayodaiwa na Halmashauri Arusha DC.

SPIKA: Amerekebisha wapi.

MHE. NOAH L.S. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, kwenye majibu ya maswali hayo iliandikwa milioni 314 badala ya bilioni 314.

SPIKA: Sasa wewe ndiyo unatutaarifu hilo Mheshimiwa, siyo walitakiwa waseme wao kama hivyo ndivyo? Endelea na swali lako lakini.

MHE. NOAH L.S. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, naomba kuuliza maswali yangu mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, kwa kuwa suala hili la ulipaji wa fidia ya umeme lilikuwa liende sambamba na usambazaji wa umeme kwenye Jimbo la Arumeru Magharibi na vijiji vyake hasa ukizingatia kwamba mkandarasi amechimba mashimo ameacha, ameweka nguzo ameacha ajaweka waya, ni lini sasa Serikali itamaliza tatizo hilo?

SPIKA: Tatizo gani?

MHE. NOAH L.S. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, la kutokuwepo kwa umeme kwenye jimbo.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa sasa hali ni tete kwenye jimbo kuhusu masuala hayo mawili ya fidia na usambazaji wa umeme, Naibu Waziri yupo tayari tuweze kuongozana naye kwenda kuokoa jahazi ambapo hali ni tete kwenye jimbo?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri kwenye swali la msingi naomba niliweke vizuri hoja ya Mheshimiwa Mbunge na Waheshimiwa Wabunge wengine ambao wanapitiwa na mradi wa kilovolt 400 wa kwenda Namanga. Ni kweli Serikali imetoa shilingi bilioni 52.67 katika maeneo yote ambako laini inapita. Lakini kila eneo ilipewa fidia yake kulingana na idadi ya watu waliofanyiwa tathmini kwa hiyo pesa hiyo inagawanywa katika maeneo yote ambako line imepita.

Mheshimiwa Spika, juzi nilikuwa Arusha na kati ya changamoto ambazo nilikutana nazo ni pamoja na hii, akiwepo na Mheshimiwa wa Longido, nilitoa maelekezo ya jumla kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, wananchi ambao hawajalipwa fidia kwa sasa ambao pesa zao zimeshapelekwa tayari kwa Wakurugenzi wao walipwe fidia hizo mara moja toka juzi. Ni kweli zinaweza zikawa zinatofautiana kiwango kwa kiwango kila wilaya lakini ya jumla ya fedha zake ni hizi. Lakini majibu ya jumla nishatoa juzi, kwa Mheshimiwa Mbunge wa Longido na wananchi walilidhika na Wakurugenzi walikubali na Wakuu wa Wilaya kuanza kulipa fidia hizo mara moja kutoka juzi ndani ya siku 10.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili kuhusiana na maeneo ambayo amezungumza ambayo ajapelekewa umeme nimetoa maelekezo na wakandarasi wote wako site na leo tunakutana nao, maeneo yote ambayo awajapatiwa umeme wakandarasi wameanza kazi toka Mwezi Machi na katika wilaya za Arusha wameanza wiki iliyopita na watapelekewa umeme ndani ya miezi 18 kutoka mwezi Machi hadi mwezi Mei. Ahsante sana.