Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni kwa sababu Hospitali iliyopo haikidhi mahitaji kutokana na uchakavu na ongezeko la watu?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Spika, kwanza nashukuru kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza; je, ni lini sasa tathmini ya uchakavu wa miundombinu ya Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni itaenda kukamilika?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa hii hospitali ilianza mwaka 1973 na mwaka 1992 ilipandishwa hadhi kuwa Hospitali ya Wilaya na kwa kuwa bado inaendelea kutoa huduma katika Wilaya ya Manyoni na kwa kuwa tuna upuungufu mkubwa sana wa wataalam katika hospitali na Jimbo zima la Manyoni Mashariki, nini commitment ya Serikali ya kupeleka wataalam katika Jimbo la Manyoni Mashariki? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Pius Stephen Chaya, Mbunge wa Manyoni kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imekwishaweka utaratibu wa kufanya tathmini katika hospitali zetu zote kongwe na chakavu 43 ambazo tumekwishazitambua ikiwemo hospitali hii ya Manyoni na kazi hiyo tayari imeanza na inaendelea. Tunatarajia ifikapo mwezi wa tatu mwaka ujao tutakuwa tumekamilisha na kufanya maamuzi wapi tutajenga hospitali mpya na wapi tutakwenda kuzikarabati zile hospitali ambazo bado zinahitaji ukarabati.

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba kuna changamoto ya upungufu wa watalaam katika huduma za afya katika vituo vyetu na Hospitali za Halmashauri ikiwemo Manyoni na Serikali imeendelea kuomba na kutoa vibali bvya ajira na katika mwaka huu wa fedha tumeomba vibali vya watumishi 12,000 lakini kipindi hiki tunaendelea na mchakato wa kuajiri watumishi 2,796 wa kada mbalimbali za afya. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Manyoni pia itapewa kipaumbele cha kupata watumishi hawa wa afya.