Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA (K.n.y. MHE. HAMIDU H. BOBALI) aliuliza:- Jimbo la Mchinga na Mtama linaunda Halmashauri ya Wilaya ya Lindi na ukubwa wa Halmashauri hii ni kikwazo cha kuwafikia wananchi kwa urahisi katika kuwapelekea huduma za jamii. Je, kwa nini Serikali isiigawe Halmashauri hii ili kuwa na Halmashauri mbili yaani Mchinga na Mtama?

Supplementary Question 1

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa tatizo la Mchinga linafanana sana na tatizo la Halmashauri ya Tandahimba iliyopo Mkoani Mtwara, je, Serikali ina mpango gani sasa wa kugawanya Halmashauri ya Tandahimba ili kuwe na Halmashauri mbili?
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali la pili, Wilaya ya Mtwara sasa hivi ina Halmashauri tatu, Mtwara Manispaa, Halmashauri ya Mtwara na Halmashauri ya Mji wa Nanyamba, je, Serikali ina mpango gani kumpunguzia mzigo Mkuu wa Wilaya ya Mtwara, ili kuanzisha Wilaya mpya ya Nanyamba?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA:Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema awali katika jibu langu la msingi ni kwamba mgawanyo huu wa Halmashauri na halikadhalika uanzishaji wa kata mpya, uanzishwaji wa vijiji halikadhalika uanzishwaji wa Wilaya una taratibu zake. Na nilizungumzia kwamba, kwa mujibu wa Katiba Ibara ya 145 Ibara ya 146 inayoanzisha Mamlaka ya Serikali za Mitaa, lakini kwa mujibu wa Sheria ya 287 inaainisha jinsi gani mchakato huu unaenda.
Sasa kwa Wilaya, Halmashauri ya Tandahimba, kwa mujibu wa Mheshimiwa Mbunge alivyoshauri ni kwamba mimi ninamshauri kwa sababu najua Mheshimiwa Chikota ni Mtaalamu mkubwa sana wa Serikali za Mitaa, tukimkumbuka katika reference yake alipokuwa katika ngazi ya mkoa hapo awali. Kwa hiyo, naona kwamba yeye awe chachu kubwa ya kutosha na mimi naona jambo hili halitamshinda. Mchakato ule utakapokamilika katika maeneo yake akija katika Ofisi ya Rais – TAMISEMI sisi hatutasita kufanya maamuzi sahihi kulingana na vigezo vitakavyokuwa vimefikiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini katika suala zima la hizi Halmashauri sasa kupata Wilaya Mpya ya Nanyamba ni kama nilivyosema awali. Nakuomba Mheshimiwa Chikota fanya utaratibu huo, wataalam watakuja site, wata-survey kuangalia vigezo vinafikiwa vipi; na mimi najua Kanda ile ukiangalia eneo lake ni kubwa sana siku nilipokuwa natoka Songea kwenda mpaka Masasi hapa katikati jiografia ya maeneo yale unaona kwamba, jinsi gani maeneo ya kiutawala mengine yako makubwa sana. Kwa hiyo, fanyeni hayo, baadae sasa Ofisi ya TAMISEMI itafanya tathmini na kuona kufanya maamuzi sahihi.

Name

Ignas Aloyce Malocha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA (K.n.y. MHE. HAMIDU H. BOBALI) aliuliza:- Jimbo la Mchinga na Mtama linaunda Halmashauri ya Wilaya ya Lindi na ukubwa wa Halmashauri hii ni kikwazo cha kuwafikia wananchi kwa urahisi katika kuwapelekea huduma za jamii. Je, kwa nini Serikali isiigawe Halmashauri hii ili kuwa na Halmashauri mbili yaani Mchinga na Mtama?

Supplementary Question 2

MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza.
Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga ilishatuma maombi ya kugawa Halmashauri ambayo iliambatana na maombi ya Wilaya, Jimbo na kupitia vikao vyote kuanzia Vijiji, WDC, DCC, RCC na kuonekana kwamba, ina vigezo vyote na hata watawala ambao wametawala maeneo hayo wanaujua ukweli huo; kwa mfano Mheshimiwa Manyanya, Mheshimiwa Mkuchika, hata baadhi ya Wabunge ndani humu, hata Waziri Mkuu aliyepita alishashuhudia ndani ya Bunge. Je, ni lini wananchi hawa watapata haki yao ya kugawanya Halmashauri?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, katika kumbukumbu yangu Mheshimiwa Malocha ndiye alinisababisha mpaka nikaanda database ya kuona kwamba Halmashauri zilizoleta matakwa ya kugawanywa Halmashauri halikadhalika Mikoa. Nikiri wazi kwamba Mheshimiwa Malocha alikuja mpaka ofisini kwangu tukalijadili suala hili na ndio maana nikawatuma wataalam wangu waandae database hiyo ikiwemo pamoja na uanzishwaji wa mji mpya kwa kaka yangu hapa kukata maeneo ya Korogwe ilikuwa yote pamoja katika mchakato huo, Mheshimiwa Profesa Maji Marefu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, na lile ndio maana tumepata muongozo sasa hivi kama viongozi wapya katika eneo hilo. Tumewatuma wataalam wetu sasa hivi wanaandaa kikosi kazi kwa ajili ya kutembelea maeneo yote ya Tanzania ili kubainisha yale maombi yaliyokuja waliofikia vigezo, kama ndugu yangu Mheshimiwa Malocha anavyosema huko, waliofikia vigezo kwamba waweze kupata hizi halmashauri na Wilaya mpya au halikadhalika Mikoa mipya ambayo imependekezwa. Basi haya yakifanyika, naomba nikuahidi Mheshimiwa Malocha kwamba timu itafika kule site kufanya final finishing, kumalizia zoezi la mwisho la kuhakiki na nikijua kwamba, eneo lako kweli ni eneo kubwa na umekuwa ukililalamikia kwa muda mrefu. Kwa hiyo kikosi kazi kitafika kule site kama maelekezo tuliyopeana pale ofisini kwangu.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA (K.n.y. MHE. HAMIDU H. BOBALI) aliuliza:- Jimbo la Mchinga na Mtama linaunda Halmashauri ya Wilaya ya Lindi na ukubwa wa Halmashauri hii ni kikwazo cha kuwafikia wananchi kwa urahisi katika kuwapelekea huduma za jamii. Je, kwa nini Serikali isiigawe Halmashauri hii ili kuwa na Halmashauri mbili yaani Mchinga na Mtama?

Supplementary Question 3

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kunipa nafasi. Wilaya ya Tanganyika ni Wilaya mpya ambayo ina Jimbo moja tu la Uchaguzi la Mpanda Vijijini. Eneo hili la kiutawala ni kubwa mno, lina uwezo wa kutoa mgawanyo wa halmashauri mbili, kwa maana ya Ukanda wa Ziwa, Halmashauri ya Karema na ukanda wa huku juu eneo la makazi mapya ya Mishamo. Je, ni lini Serikali itafikiria kutoa mamlaka ya kugawa maeneo haya, ili yaweze kuwasaidia wananchi wa Mpanda kwa ujumla?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba, Wilaya ya Mpya ya Tanganyika, lakini pale awali nadhani tulikuwa katika mchakato ulikuwa hatuna Wilaya hii, lakini baadaye mchakato ukafanyika tukapata Wilaya, lakini bado changamoto ni kubwa sana ya Halmashauri hii. Kwa hiyo, naomba niseme tena vilevile Mheshimiwa Kakoso kama nilivyosema katika majibu yangu ya msingi ya awali kwamba mimi naomba Mheshimiwa Mbunge kwa sababu najua eneo lenu nalo limegawanyika sana hapa katikati, Halmashauri nyingi zimepatikana katika eneo hilo, lakini bado kijiografia eneo bado ni kubwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, nipende tena nitoe maelezo yaleyale kama niliyotoa mwanzo ni kwamba, andaeni tena ule mchakato upite katika vigezo vyote, katika vijiji, WDC, Halmashauri, RCC, halafu ikifika katika Ofisi ya Rais – TAMISEMI kama nilivyosema ni kwamba, tutafanya maamuzi sahihi kutokana na vigezo vitakavyokuwa vimefikiwa katika eneo hilo.

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA (K.n.y. MHE. HAMIDU H. BOBALI) aliuliza:- Jimbo la Mchinga na Mtama linaunda Halmashauri ya Wilaya ya Lindi na ukubwa wa Halmashauri hii ni kikwazo cha kuwafikia wananchi kwa urahisi katika kuwapelekea huduma za jamii. Je, kwa nini Serikali isiigawe Halmashauri hii ili kuwa na Halmashauri mbili yaani Mchinga na Mtama?

Supplementary Question 4

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa kuwa mazingira ya Mchinga yanafanana kabisa na Wilaya ya Tunduru yenye kilometa za mraba 18,776; na kwa kuwa tayari kuna majimbo mawili na taratibu zote za kuigawa Wilaya ile zilishafanyika siku za nyuma; na kwa kuwa zilitolewa ahadi za viongozi wa Awamu ya Nne kuigawa Wilaya ile na Mkoa kwa ujumla. Je, ni lini taratibu za kuigawa Wilaya ile na Mkoa mpya wa Selous zitafanyika?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, katika kumbukumbu zangu nilizokuwanazo ni kwamba eneo analozungumzia Mheshimiwa Mpakate ni kweli jambo hili liko ofisini, lakini nadhani kuna baadhi ya vitu vingi zaidi ya hapo hata kuna suggestion ya kugawa kupata Mkoa mpya wa Selous, kama sikosei katika eneo hilo! Na Mheshimiwa Ngonyani alikuwa akizungumza jambo hilo na hata Mheshimiwa Ramo Makani alikuwa katika mchakato huo wa pamoja kuhakikisha kwamba maeneo hayo, kutokana na jiografia yake, tunapata Mkoa mpya wa Selous.
Kwa hiyo, sasa kama Ofisi ya TAMISEMI itafanya uhakiki jinsi gani, aidha hizo Wilaya, Halmashauri au Mkoa mpya, mwisho wa siku tutakuja na majibu sahihi.
Mheshimiwa Naibu Spika, lengo kubwa ni kwamba kupeleka utawala katika eneo hilo kwa sababu, ni kweli, kuna wananchi wengine saa nyingine ukitoka huku Tunduru kwenda hata kule Ruvuma kuna changamoto, lakini uko karibu hapa karibu na Masasi. Kwa hiyo, walikuwa na maombi mengi kwa pamoja na viongozi waliopita walitoa ahadi mbalimbali.Ofisi ya TAMISEMI italifanyia kazi na mwisho wa siku ni kwamba, eneo hilo ki-jiografia litagawanywa vizuri kwa suala zima la kiutawala ilimradi wananchi wapate huduma ya karibu katika maeneo yao