Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kufuta madeni ya muda mrefu kwa wafanyabiashara wa ndani yatokanayo na ukosefu wa elimu juu ya matumizi sahihi ya mashine za EFD wanayodaiwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania?

Supplementary Question 1

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, nimesikia majibu ya Serikali lakini ukweli bado wafanyabiashara wana kilio hapa nchini, hawana raha na Serikali yao kulingana na madeni hayo maana hawakuwa na elimu ya hizi mashine za EFD. Hivyo sasa, naomba Mheshimiwa Waziri utoe kauli ili nchi nzima wajue kwamba walishasamehewa hayo madeni.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili je, ni lini sasa Serikali itafuta madeni ya mgodi wa Bulyanhulu ili waweze kutimiza makubaliano yao katika mkataba wao wa ujenzi wa barabara itokayo Kahama ya lami kwenda Bulyanhulu. (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango ya Mheshimiwa Nicodemus Maganga kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza suala la kauli ya Serikali kuhusu kusamehe madeni haliwezi kutolewa kwa utaratibu huu. Msamaha wa madeni unatokana na uko kwa mujibu wa sheria, hata yale maamuzi ambayo yalisababisha kusamehe madeni ya kipindi kile yalitokana na utaratibu wa kisheria ambao ulipitishwa na Bunge hili. Kwa hiyo, hatuwezi kusimama hapa tukatoa tu tamko la kusema tunamsamehe nani madeni. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili vilevile kuhusiana na kusamehe madeni na kwenyewe kuna repercussions zake. Kwa mfano, best practice wataalam wanasema kwamba utaratibu ule wa kusamehe madeni hauwezi kufanywa kila wakati kwa sababu unaathiri wigo mpana wa ukusanyaji kodi chini.

Kwa hiyo, lengo kubwa lilikuwa ni kuhakikisha kwamba kwanza tunawasaidia wale ambao walikuwa na madeni ya muda mrefu, lakini la pili ilikuwa ni kuhakikisha kwamba tunakusanya kwa kipindi kile ambacho maamuzi yale yalitoka kwa haraka.

Kwa hiyo, ili msamaha mwingine utoke, lazima tukae chini na kuweza kufanya tathmini na utafiti wa kina kupima athari na faida za kufanya hivyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili kuhusiana na hoja ya Bulyanhulu napokea maelekezo yako nadhani ni suala mahsusi kwa hiyo basi tutalifanyia kazi na kumpatia majibu Mheshimiwa Mbunge baada ya kupata hizo takwimu. (Makofi)