Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Joseph Kizito Mhagama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Madaba

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA - K.n.y. MHE. MICHAEL C. MWAKAMO aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kutatua migogoro ya mipaka ya kiutawala baina ya Mikoa, Wilaya na Vijiji hapa nchini?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Hata hivyo, nilikuwa na swali la nyongeza.

Kwa vile migogoro hii kwa sehemu kubwa inachangiwa sana na kutokamilika kwa utengenezaji wa mipango bora ya matumizi ya ardhi katika Mikoa, Wilaya na Vijiji vyetu. Ni lini basi Serikali itakamilisha upimaji na utekelezaji wa sera ya kuwa na mipango ya kuwa na matumizi bora kwa kila Kijiji? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana na kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Joseph Mhagama, Mbunge wa Madaba kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge alikuwa anauliza kwamba moja ya sababu kubwa ya hii migogoro ni sisi ama Serikali kushindwa kwa wakati kukamilisha hii mipango ya matumizi bora ya ardhi.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nimwambie tu jambo moja kwamba ili Serikali iweze kupima hizo ardhi katika maeneo mengine yote. Ni lazima ngazi za Halmashauri zote nchini zipange bajeti ili watu/sisi kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi tuje tupime hayo maeneo ili kuhakikisha kabisa tunaondoa hiyo kero iliyopo.

Kwa hiyo, nizitake Halmashauri zote nchini kuhakikisha katika bajeti zao wawe wanatenga fedha kwa ajili ya upimaji wa ardhi ili kuhakikisha kwamba hii migogoro tunaiondoa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu matumizi ya ardhi katika ngazi za vijiji nafikiri ni kama nilivyoeleza katika jibu langu la msingi kwamba tutaendelea kuhamasisha ngazi za Halmashauri kuhakikisha wote wanafuata sheria lakini tutaendelea kutenga fedha na kuainisha maeneo yote ili kuondoa hii migogoro ambayo inaendelea kujitokeza kila wakati. Kwa sababu hilo ndiyo lengo la Serikali kuhakikisha kwamba migogoro hii ya mipaka pamoja na maeneo inatatuliwa kabisa. Ahsante.