Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza:- Je, ni kwa nini Hospitali ya Mji Tarime isipandishwe hadhi na kuwa Hospitali ya Kanda Maalum ya Tarime na Rorya?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushuru.

Mheshimiwa Naibu Spika, Hospitali ya Mji wa Tarime mpaka leo imesajiliwa kama Hospitali ya Wilaya na kiuhalisia inahudumia wananchi wote wa kutoka Tarime Vijijini kwa huduma za upasuaji, kutoka Rorya, lakini pia watu wengine wanatoka nje ya nchi kwa maana ya kule Kenya tuko mpakani.

Ningetaka kujua ni kwa nini Serikali haijaifanya hospitali hii ili iweze kupata stahiki kama Hospitali ya Wilaya kama vile ilivyo Hospitali ya Kahama Mjini ambayo inahudumia Ushetu na Msalala, kama vile ilivyo Hospitali ya Nzega Mjini ambayo inahudumia Bukene na Nzega Vijijini ili sasa ihudumie sio kwa idadi ya watu wa Tarime Mji bali kwa idadi ya watu halisia wa kutoka Wilaya nzima ya Tarime na wengine kutoka Rorya?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kupelekea kupokea watu wengi nje ya Tarime Mji, hospitali ile inaelemewa, haina matabibu wa kutosha, na kama nilivyosema awali wanaleta fedha chache, leo hata ukienda mortuary unakuta ina burst kwa sababu inachukua watu wote kutoka nje.

Ningetaka kujua ni lini Serikali itapanua chumba cha kuhifadhi maiti ili sasa wakati mkibadilisha usajili kuwa wa Wilaya na kuweka stahiki za Wilaya ili mortuary ile iweze kupokea Watanzania ambao wamekutwa wamefariki na kuja kuhifadhiwa pale Tarime Mji?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA, (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Esther Nicholas Matiko, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba hospitali ya Mji wa Tarime inahudumia pamoja na wananchi wa kutoka katika Halmashauri za jirani na Tarime na ni utaratibu wa kawaida katika hospitali zetu ambazo mara nyingi zipo mipakani, lakini hata zile ambazo zinahudumia wananchi ambao wapo karibu na Halmashauri hiyo.

Kwa hiyo, kuna baadhi ya hospitali za Halmashauri nchini kote ambazo pamoja na wananchi wa ndani wa Halmashauri husika pia zinahudumia wananchi wanaotoka katika Halmashauri nyingine, ni suala la kawaida na utaratibu wetu sisi katika afya hatuna mipaka.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nitambue kwamba ni kweli tunafahamu hospitali hii inazidiwa na wagonjwa, lakini takwimu zimeonesha kwa wastani kwa siku wagonjwa wanaolazwa ni 70 lakini pia 140 wa OPD. Na Serikali inatambua kwamba tunahitaji kuendelea kuboresha miundombinu katika hospitali hii na sisi tutaendelea kuhakikisha kwamba tunaongeza idadi ya watumishi kwa maana ya waganga na wauguzi ili waweze kuendana na mzigo wa hospitali hii. Lakini pia ujenzi wa mortuary ni kipaumbele katika Serikali yetu, lakini pia katika Halmashauri husika.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba hili nilichukue ili twende na sisi tukalifanyie tathmini kuona kwa maana Serikali Kuu na Halmashauri namna gani tutafanya ili tuweze kuondoa adha ya kuwa na mortuary ndogo na kuboresha huduma hizi kwa wananchi. (Makofi)

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza:- Je, ni kwa nini Hospitali ya Mji Tarime isipandishwe hadhi na kuwa Hospitali ya Kanda Maalum ya Tarime na Rorya?

Supplementary Question 2

MHE. STANSLAUS H. NYONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, kinachotokea Tarime hata Maswa kinatokea hicho kwamba Hospitali ya Maswa inazidiwa kwa wagonjwa na imekadiriwa kwanza kuwa Hospitali ya Wilaya, lakini inahudumia zaidi ya Wilaya moja. Kuna wagonjwa wanatoka Itilima, wagonjwa wanatoka Wilaya ya Meatu na wagonjwa wa Wilaya ya Maswa. Hospitali inaonekana kama ya Wilaya lakini inazidiwa kwa sababu watu wengi wanakwenda pale.

Kwa hiyo nilikuwa naomba aji-commit Mheshiwa Naibu Waziri je, na Maswa atai-consider na yenyewe iweze kuongezewa hadhi? Ahsante sana.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA, (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Stanslaus Nyongo, Mbunge wa Maswa Mashariki kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge ameongea kuhusiana na Hospitali ya Halmashauri ya Maswa ni hospitali ambayo ni kongwe, lakini ina hudumia wananchi wengi wa ndani ya Halmashauri ya Maswa, lakini pia na Halmashauri zingine kama Itilima na Meatu. Lakini naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali iliona hilo na imelifanyia kazi. Kwanza kwa kujenga Hospitali ya Halmashauri katika Halmashauri ya Wilaya ya Itilima ili kuhakikisha wananchi wa Itilima ambao walikuwa wanalazimika kufika Maswa sasa watatibiwa Itilima, lakni pia imeboresha sana hospitali ya Halmshauri ya Meatu.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pamoja na hayo bado tunatambua kwamba kuna kazi ya kufanya katika Hospitali ya Halmashauri ya Maswa na ni muhakikishie tunaji-commit kwamba tutaendelea kuhakikisha tunaboresha miundombinu, vifaa tiba na upatikanaji wa wataalam ili tuhakikishe hospitali ile inatoa huduma bora zaidi. (Makofi)

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza:- Je, ni kwa nini Hospitali ya Mji Tarime isipandishwe hadhi na kuwa Hospitali ya Kanda Maalum ya Tarime na Rorya?

Supplementary Question 3

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Wilaya ya Urambo ina hospitali ya wilaya iliyojengwa mwaka 1975 na hali yake siyo nzuri. Je, Serikali yetu inayosikiliza maombi ya wananchi ni lini itakuja kuingalia itengenezwe upya ili iende na wakati? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA, (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Margaret Simwanza Sitta, Mbunge wa Urambo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Hospitali ya Halmashauri ya Urambo ni kweli ni hospitali kongwe sana ambayo imejengwa mwaka 1975 na bahati njema katika ziara yangu pia nilifika katika hospitali ile tukashirikiana vizuri sana na Mheshimiwa Mama Margaret Sitta, tukaikagua hospitali ile na kuona kwa kweli tunahitaji kuweka mpango mkakati wa kuzikarabati hospitali kongwe zote nchini ikiwepo ya Hospitali hii ya Urambo.

Kwa hiyo, naomba nimuhakikishie kwamba mipango ya Serikali tumeshapanga katika mwaka ujao wa fedha kuanza kukamilisha ujenzi wa Hopitali za Halmashauri katika Halmashauri zote ambazo hazina Hospitali za Halmashauri. Lakini baada ya hapo tutakwenda kwenye awamu ya kukarabati au kujenga kulingana na tathmini hospitali nyingine za Halmashauri katika Halmashauri zenye hospitali kongwe sana ikiwepo Urambo.

Kwa hiyo, naomba nimhakikishie kwamba suala hili tunalifanyia kazi na tutahakikisha kwamba tunalitekeleza. (Makofi)

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza:- Je, ni kwa nini Hospitali ya Mji Tarime isipandishwe hadhi na kuwa Hospitali ya Kanda Maalum ya Tarime na Rorya?

Supplementary Question 4

MHE. VITA RASHID KAWAWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.

Kwa kuwa Serikali ilitufanyia kazi nzuri sana Jimbo la Namtumbo kutujengea Kituo cha Afya cha Mtakanini na kukarabati Kituo cha Afya cha Mji wa Namtumbo lakini vituo vya afya hivi viwili havina watumishi.

Je, Serikali ipo tayari sasa kutupangia watumishi ili ifanye kazi kama ilivyokusudiwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA, (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi ofisi ya Rais - TAMISEMi, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Vita Kawawa, Mbunge wa Namtumbo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nipokee shukrani nyingi za Mheshimiwa Mbunge wa Namtumbo kwa kazi kubwa sana ambayo Serikali imefanya kuhakikisha inakarabati na kujenga vituo vya afya katika Jimbo la Namtumbo. Lakini nimhakikishie kwamba Serikali inatambua sana kwamba tuna upungufu wa watumishi katika vituo vile vya afya. Lakini kama tunavyoona, hivi sasa Serikali imetangaza ajira 2,796 za wataalam wa afya, lakini pia katika mwaka wa fedha tutakwenda kuomba vibali kuhakikisha kwamba tuna ajiri watumishi hawa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba nimhakikishie kwamba Jimbo la Namtumbo litapewa kiupaumbele kuhakikiha tunaendelea kupelekea watumishi pale na kuboresha huduma za afya. (Makofi)