Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Francis Isack Mtinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza:- Je ni lini Serikali itaweka vifaa vya maabara kwenye maabara zote za Shule za Sekondari katika Wilaya ya Mkalama zilizojengwa kwa nguvu za wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. FRANCIS I. MTINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nashukuru kwa majibu mazuri yaliyotolewa na Serikali lakini nina maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Serikali imepeleka vifaa vya maabara kwenye shule 18 kati ya 19: Je, sasa wana kauli gani kuhusu kupeleka walimu wa kutosha wa sayansi katika huu mgao unaokuja wa walimu ili vifaa hivi viweze kuwatendea haki wanafunzi wetu wa Mkalama?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Kwa kuwa Wilaya ya Mkalama ina High School moja tu na ambayo iko kwenye mchepuo wa Sanaa: Je, Serikali ina mpango gani kuhusu kuongeza hostel katika Sekondari ya Gunda ambayo sasa wana hostel moja ili angalau sasa tuweze kuanzisha mchepuo wa sayansi katika sekondari hii? Ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Francis Isack Mtinga, Mbunge wa Iramba Mashariki, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa tunapokea pongezi ambazo amezitoa kwa sababu, Serikali imefanya kazi nzuri katika jimbo lake na Halmashauri yake ya Mkalama kwa kupeleka vifaa vya maabara katika sekondari 18 kati ya 19 za jimbo lake. Swali lake la msingi ambalo ameiliza ameuliza tu ni lini Serikali itapeleka Walimu wa Sayansi wa kutosha katika shule hizo zenye maabara, ili angalau sasa pamoja na vifaa basi pawepo na basi pawepo na Walimu wa kutosha kwenye huo mgawo unafuatia. Nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tumepokea ombi lake na tutazingatia wakati wa mgawanyo ambao tutautoa hivi karibuni kabla ya mwisho wa mwezi Juni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, ameomba tujenge hostel ya Sekondari ya Dunga ili angalau na wao waweze kupata kidato cha tano na cha sita. Niseme tu ombi lake limepokelewa na tutalifanyia kazi kulingana na mahitaji ya jimbo lake.

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza:- Je ni lini Serikali itaweka vifaa vya maabara kwenye maabara zote za Shule za Sekondari katika Wilaya ya Mkalama zilizojengwa kwa nguvu za wananchi?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. STEVEN L. KIRUSWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa katika baadhi ya shule zetu za sekondari zilizoanzishwa kabla ya Serikali kuweka mkazo kwamba, lazima shule kabla haijasajiliwa iwe na maabara, kuna shule chache zimebaki zikiwa hazina maabara kabisa kama Shule ya Flamingo iliyoko katika Wilaya ya Longido, Tarafa ya Ketumbeine, Kata ya Meirugoi. Je, Serikali ina mpango gani wa kutenga fedha za kutosha, ili kila shule ya kata iwe na maabara ukizingatia kwamba, sayansi ni muhimu? Pia wananchi wanajitahidi kuchanga, lakini bajeti ya TAMISEMI imetoa 25,000/= tu kama umaliziaji wa maabara ambazo zimeshafikia hatua ya juu; hii ambayo haina kabisa Serikali ina mpango gani kutusaidia?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Kiruswa, Mbunge wa Longido, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge anataka kufahamu upi niseme ni mkakati wa Serikali wa kuhakikisha katika zile shule zote, yaani ikiwemo Shule yake ya Flamingo iliyopo katika jimbo lake, ambazo hazina maabara tunazikamilisha. Moja ya mpango wetu na ndio maana katika bajeti mtaona kabisa tumetenga fedha, moja kwa ajili ya kuhakikisha tunamalizia maabara zote ambazo wananchi walikuwa wamezianzisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, tumezitaka halmashauri zote nchini kuhakikisha katika yale maeneo ambayo kuna shule za sekondari za kata ambazo hazina maabara zinaanzisha ujenzi, ili sisi tuweze kuongezea fedha. Kwa hiyo, moja ya huo mkakati ni pamoja na kumalizia katika sekondari ya Mheshimiwa Mbunge. Kwa hiyo, nimhakikishie kabisa kwamba, hata hiyo Sekondari ya Flamingo itakuwa na maabara, tutapeleka vifaa na watoto watasoma sayansi kwa vitendo. Ahsante.