Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA aliuliza:- Kumekuwa na changamoto ya huduma za Afya katika Zahanati zetu hasa ukosefu wa dawa pamoja na huduma bure kwa wazee, watoto na akinamama wajawazito. Je, ni lini Serikali itahakikisha Sera ya Afya inatekelezwa bila tatizo lolote?

Supplementary Question 1

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa kunipa fursa ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kila mwaka tumekuwa tunaongeza bajeti ya dawa katika Serikali yetu na tumekuwa tukiona bado zahanati na vituo vya afya havipati dawa. Swali langu: Je, mmefanya utafiti gani wa kuhakikisha kwamba hizo fedha, shilingi bilioni 270 na hiyo shilingi bilioni 140 ndizo zitakwenda kutatua changamoto ya dawa katika zahanati zetu na vituo vya afya?

Swali langu la pili; hivi tunavyozungumza wananchi wenye changamoto hizi wa kutoka Jimbo la Kalenga na wengine wengi wanaangalia; je, wananchi wategemee nini kuwa hizi dawa katika zahanati na vituo vya afya itakuwa ni historia?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kama ambavyo Mheshimiwa Grace Victor Tendega ametangulia kusema, Serikali imeendelea kuongeza bajeti ya fedha kwa ajili ya ununuzi wa dawa, vitendanishi na vifaa tiba kwa takriban mara tisa ndani ya miaka mitano na hii ni kwa sababu Serikali inajali sana wananchi na inahitaji kuona wananchi wanapata dawa za kutosha ili kuhakikisha kwamba huduma za afya ni bora zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo ni kweli kwamba bado tuna changamoto ya uhitaji wa dawa na Serikali inatambua kwamba bado tuna kazi ya kufanya kuhakikisha tunaendelea kupunguza sana upungufu wa baadhi ya dawa katika vituo vyetu vya huduma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana katika jibu langu la msingi nimeeleza namna ambavyo Serikali imepeleka fedha mpaka sasa, zaidi ya shilingi bilioni 140 zimepelekwa katika vituo vyetu na mpaka mwisho wa mwaka huu wa fedha, ifikapo Juni, tutakuwa tumepeleka fedha zaidi kuhakikisha tunaendelea kuboresha upatikanaji wa dawa katika vituo hivyo na kwa makundi maalum na wananchi kwa ujumla.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, nimhakikishie kwamba Serikali imefanya tathmini kwamba kadri inavyoongeza fedha ndivyo upungufu wa dawa unavyopungua na ndiyo maana lengo la Serikali ni kuendelea kuongeza fedha. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, tutaendelea kuhakikisha tunatenga fedha kwa ajili ya kuboresha upatikanaji wa dawa na kuondoa kabisa upungufu wa dawa katika vituo vyetu.

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. GRACE V. TENDEGA aliuliza:- Kumekuwa na changamoto ya huduma za Afya katika Zahanati zetu hasa ukosefu wa dawa pamoja na huduma bure kwa wazee, watoto na akinamama wajawazito. Je, ni lini Serikali itahakikisha Sera ya Afya inatekelezwa bila tatizo lolote?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nakushukuru sana. Kusema kweli Serikali imetenga fedha nyingi. Kwenye Jimbo letu la Vunjo Kata 16 hakuna kituo cha afya cha Serikali isipokuwa vituo vikongwe, vichakavu vya Mwika, OPD Himo na Kiruavunjo. Ni chakavu hata havistahili kuitwa vituo vya afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, namwomba Waziri atueleze ni lini watakarabati vituo hivi na kuviinua hadhi ili viweze kuwa vituo vya afya vinavyotumika na watu wa Vunjo? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kimsingi tunatambua sana kwamba katika Jimbo la Vunjo kuna upungufu mkubwa wa vituo vya afya lakini hata vile vituo vya afya ambavyo vipo, vina uchakavu kwa sababu ni vya siku nyingi. Ndiyo maana katika mpango wetu ambao tumeuwasilisha na bajeti yetu ya mwaka 2021/2022 tumeweka kipaumbele kwanza cha kwenda kuhakikisha tunajenga vituo vya afya 211 katika maeneo ambayo hayana vituo vya afya.

Pili, kuhakikisha tunaweka mpango wa kwenda kukarabati na kupandisha hadhi vile vituo ambavyo vina sifa hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Kimei kwamba Jimbo la Vunjo pia litapewa kipaumbele kuhakikisha kwamba tunafanyia kazi vituo hivyo vya afya. (Makofi)