Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abeid Ighondo Ramadhani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE K.n.y. MHE. ABEID R. IGHONDO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutengeneza barabara za Singida Kaskazini zinazounganisha Vijiji ambazo hazipitiki kwa sasa?

Supplementary Question 1

MHE. ABEID R. IGHONDO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushuru. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ninayo maswali mawili ya nyogeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya kutoka Singida Mjini kupitia Kinyeto hadi Sagala eneo la Kinyagigi linalounganisha Kijiji cha Minyaa na Kinyagigi ilikatika kabisa na wakati wa mvua ilikuwa haipitiki ambapo maji hujaa inakuwa kama bwawa vile. Pia barabara inayotoka Makuro kuelekea Jagwa nayo pia ilikatika kabisa na ilikuwa haipitiki kutokana na utengenezaji wa chini ya kiwango. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha barabara hizi zinapitika wakati wote hasa wakati wa masika?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, je, Naibu Waziri yupo tayari kuambatana na mimi wakati wowote kuanzia sasa kwenda kutembelea jimbo zima kuona uhalisia wa barabara zake zilivyo hoi na ambavyo hazipitiki? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ramadhani Ighondo, Mbunge wa Singida Kaskazini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la kwanza ambalo Mheshimiwa Mbunge ameuliza upi ni mpango mkakati wa Serikali wa kusaidia hizi barabara ziwe zinapitika wakati wote. Nimwambie tu Mheshimiwa kwamba Mpango Mkakati wa Serikali ni kuhakikisha kwamba tunakarabati, tunatengeneza na tunaanzisha barabara mpya ili kuhakikisha tunatoa huduma hiyo kwa wananchi kwa wakati wote. Ndio maana katika bajeti ambayo mmetutengea sasa hivi kuna ongezeko la fedha na kazi mojawapo ya hizo fedha zilizoongezeka ni kuhakikisha kwamba tunakwenda kushughulikia barabara hizi.

Mheshimiwa Naibu Spika, tuna barabara za aina tatu; za lami, changarawe na udongo na zaidi ya asilimia 80 za barabara zetu ni za udongo. Kwa hiyo, lengu letu sisi kwa awamu ya kwanza chini ya Rais wetu wa Awamu ya Sita ni walau tuifikie nchi nzima kwa kiwango cha changarawe kwa asilimia 50. Tukijenga kwa kiwango hicho cha changarawe na tukijenga na madaraja, naamini kabisa huu uharibifu ambao unasababisha hizi barabara zisipitike wakati wote tutakuwa tumeutatua ikiwemo za Jimbo lake la Singida Kaskazini.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini jambo la pili la kuongozana naye, naomba kusema kwamba nipo tayari. Bahati nzuri nilishafika Singida Kaskazini, nafahamu miundombinu yake na changamoto zake na nilikwenda wakati ni msimu wa mvua. Kwa hiyo, tutarudi tena tukafanye kazi kwa sababu huo ndiyo wajibu ambao tumedhamiria kuufanya. Ahsante.

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE K.n.y. MHE. ABEID R. IGHONDO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutengeneza barabara za Singida Kaskazini zinazounganisha Vijiji ambazo hazipitiki kwa sasa?

Supplementary Question 2

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Changamoto ya wananchi wa Singida ni sawa na changamoto wanayopitia watu wa Kyerwa na hasa Kata ya Songambele, eneo la Kitebe ambalo wanazalisha sana mahindi lakini kuna changamoto ya barabara tangu lile eneo limekuwepo kwenye Kijiji cha Kitega. Nataka kupata commitment ya Serikali kuhakikisha wanaiunganisha hiyo Kitega na Kata nzima ya Songambele ili tuweze kufanya biashara na Jimbo la Karagwe lakini pia na Rwanda kwa sababu ni mpakani mwa Rwanda pia?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Anatropia Theonest, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali tunatambua mchango mkubwa ambao wamekuwa wakiutoa, tunatambua umuhimu wa barabara zote nchini na ndiyo maana tunaendelea kuongeza fedha na tumekuwa tukizitenga ili kuhakikisha kwamba tunazitengeneza na zinapitika. Hata wananchi wa Kitega katika hiyo Kata ya Songembele tutahakikisha tunawaunganisha ili kuwaondolea hiyo adha ambayo ina wakabili. Kwa hiyo, tutatafuta fedha ili tuzipeleke katika eneo husika. Ahsante sana.

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE K.n.y. MHE. ABEID R. IGHONDO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutengeneza barabara za Singida Kaskazini zinazounganisha Vijiji ambazo hazipitiki kwa sasa?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kituo cha Afya pekee kinachotegemewa na watu zaidi ya 300,000 pale Vunjo ni cha Kilema. Kwenda kwenye kituo hiki, barabara iliyopo ni hiyo ya Mandaka – Kilema au barabara ya Nyerere. Sasa hivi barabara ile haipitiki kabisa, wagonjwa hawawezi kwenda kwenye kituo hiki cha afya. Naomba Mheshimiwa Naibu Waziri, chonde chonde atoe tamko la dharura watu waende kushughulikia barabara hii. Nitashukuru sana akitoa tamko hilo. (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Dkt. Charles Kimei ameelezea hiyo barabara inayoelekea katika Kituo cha Afya Kilema kinachohudumia zaidi ya wananchi 300,000 kwamba haipitiki wakati huu na ameitaka Serikali itoe tamko. Niiagize TARURA kwamba waende wakafanye tathmini watuletee katika Ofisi ya Rais, TAMISEMI ili tuweze kusaidia, tuone namna gani tunapata fedha na kuitengeneza hiyo barabara kwa dharura ili wananchi waweze kupita.