Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE K.n.y. MHE. VUMA A. HOLLE aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Barabara ya Kasulu - Uvinza kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina swali moja la nyongeza:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kipande cha barabara ya kutoka Uvinza hadi Malagarasi, kilometa 48, Serikali iliahidi kukijenga kwa msaada wa pesa za Falme za Kiarabu. Tangu mwaka juzi, 2019 Serikali imekuwa ikisema kwamba kipande hicho kitajengwa kwa pesa hizo za msaada wa Falme za Kiarabu:-

Je, ni lini sasa Serikali itajenga kipande hicho cha kutoka Uvinza hadi Malagarasi? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, Barabara ya Malagarasi hadi Uvinza yenye urefu wa takribani kilometa 53 ni kati ya barabara kuu ambayo inaunganisha Mkoa wa Kigoma na Tabora. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hiyo fedha ipo na muda wowote, hata kabla ya mwisho wa mwaka wa fedha huu, itatangazwa kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami ili sasa tuweze kukamilisha barabara kwa kiwango cha lami kutoka Kigoma – Malagarasi – Kaliuwa – Urambo – Tabora hadi Dodoma. Ahsante sana.

Name

Robert Chacha Maboto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda Mjini

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE K.n.y. MHE. VUMA A. HOLLE aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Barabara ya Kasulu - Uvinza kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. ROBERT C. MABOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Halmashauri ya Mji wa Bunda ni makutano kati ya barabara itokayo Ukerewe – Mwanza – Simiyu kwenda Sirari – Tarime – Musoma kuja Mwanza na Serengeti kuja Mwanza:-

Je, ni lini Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi itaweka taa za barabarani za kuongoza magari ili kupunguza ajali zinazotokea eneo hilo? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba, kwa sasa barabara zote zinazojengwa na zinazopita kwenye miji, katika mikataba lazima watengeneze barabara katika miji. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, mpango upo sasa wa TANROADS kuhakikisha kwamba sehemu zote za miji ambazo zilikuwa hazina barabara za kuongozea magari kama alivyosema, wafanye usanifu ili tupate gharama yake na tuweze kuweka taa za kuongozea magari, hasa maeneo ambayo yana magari mengi. Kwa hiyo, study hiyo inaendelea. Naamini Bunda itakuwa ni sehemu ya wanufaika. Ahsante.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE K.n.y. MHE. VUMA A. HOLLE aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Barabara ya Kasulu - Uvinza kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. ANTHONY P. MAVUNDE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Ubovu wa Barabara ya Ihumwa – Hombolo unaleta adha kubwa kwa wananchi wa Chahwa, Ipala na Hombolo yenyewe na hivyo kuongeza gharama za usafiri: Je, ni lini sasa Serikali itakuwa tayari kutekeleza mpango wa ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami kuanzia Ihumwa mpaka Hombolo ili kuwaondolea adha wananchi hawa? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, ni azma ya Serikali kujenga barabara zote kwa kiwango cha lami, lakini suala hili linafanyika kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha. Barabara ya Ihumwa – Hombolo hadi Mayamaya yenye urefu wa takribani kama kilometa 7.3 ni ya kiwango cha changarawe na kama fedha itapatikana, itajengwa kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, Serikali imetenga fedha kwa ajili ya kuhakikisha kwamba muda wote inapitika ili wananchi wa eneo hilo ikiwa ni pamoja na wanafunzi na wafanyakazi wa Chuo cha Hombolo wasiweze kupata taabu. Kwa hiyo, tumetenga fedha kwa matengenezo ya muda na kuhakikisha kwamba maeneo yote yale korofi yanatengenezwa ili kusiwe na changamoto ya usafiri na usafirishaji kwa barabara hiyo. Ahsante.