Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Khalifa Mohammed Issa

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Mtambwe

Primary Question

MHE. KHALIFA MOHAMED ISSA K.n.y. MHE. KHATIB SAID HAJI aliuliza:- Je, Serikali inachukua hatua gani kukabiliana na Waganga wapiga ramli chonganishi na Manabii wa uongo wanaodanganya na kutapeli wananchi kila siku?

Supplementary Question 1

MHE. KHALIFA MOHAMED ISSA: Mheshimiwa Naibu Spika, nimshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake. Lakini, hata hivyo ningependa kujua kuna mfano gani kwa waganga hao wa ramli chonganishi na manabii wa uongo hatua ambazo wamechukuliwa baada ya kupatikana na kadhia hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, je, Serikali haioni sasa wakati umefika wa wale manabii ambao wanadai wanao uwezo wa kuwafufua waliokufa ili kukaa nao kwa karibu ili kuweza kuwafufua wapendwa wetu. Ahsante. (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI: Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza je ni mfano gani wowote ambao uliowahi kuchukuliwa hatua wa hawa waganga matapeli na Manabii.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama Mheshimiwa Khalifa atarejea kwenye jibu langu la msingi ni kwamba mpaka kufika kipindi cha mwaka 2020 jumla ya kesi 57 za waganga chonganishi na wengine tayari zimesharipotiwa kwasababu ili kesi iwe kesi kwanza iwe reported. Kwa hiyo, kikubwa nimwambie kwamba zipo kesi ambazo zimeshafika kwenye ofisi yetu au zimeshafika Mahakamani, tayari zimo katika mchakato wa kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa taratibu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kingine nimwambie kwamba hili jambo ni jambo amablo linahitaji utulivu wa kukaa tukafanya utafiti na takwimu za kutosha ili tukilileta hapa tuliseme kwa mujibu wa uhalisia lilivyo. Kikubwa ni kwamba zipo kesi ambazo zimeshakuwa reported. Kuna kesi ilijitokeza Mkoa wa Njombe, yupo kijana aliambiwa na babu yake ili uwe Tajiri na huo utajiri tupate mimi na wewe basi lazima uwe unawaua watoto mpaka wafike idadi fulani. Mwisho wa siku ile kesi ikaripotiwa na tukamshtaki huyo mtu kwa kosa la mauaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna kesi imejitokeza Misungwi huko ya mtu mmoja aliambiwa na mganga hivyo hivyo tapeli ili mimi na wewe tuwe matajiri hakikisha unawaua wanawake halafu unatembea nao. Lengo na madhumuni tuwe matajiri. Hii kesi imeletwa na tumeichukulia hatua kwa hivyo. Kikubwa niseme kwamba hizi kesi zipo kwa zile ambazo zimeripotiwa na hatua za kisheria kwa mujibu wa taratibu zinachukuliwa na majibu yatapatikana.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali jingine lilikuwa linauliza je, hakuna haja ya kukaa sasa na hawa wafufuaji ili tuweze kuwafufua wapendwa wetu?

Mheshimiwa Naibu Spika, imani ya kibinadamu inaamini na ndivyo ilivyo kwamba mwenye uwezo wa kuondosha na kurejesha, yaani kufanya mtu akaondoka, akafa ni Mwenyezi Mungu peke yake. Ndiyo maana ilifika wakati tukawa tunasema kwamba kama kutakuwa kuna watu wa namna hii kama alivyoshauri Mheshimiwa Mbunge, tuko tayari kukaa nao tuwaeleweshe, tuwafahamishe ili wafike wakati wasije wakazua migogoro katika jamii. Kwasababu anaweza akatokezea mtu akasema mimi nina uwezo wa kufufua, akachukua pesa za watu. Mwisho mtu akazikwa akafa akasahauliwa. Mwisho wa siku migogoro katika jamii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kikubwa nimwambie tuko tayari kukaa na hao watu ili tujue namna ya kuwaelimisha kuwaeleza kwamba mwenye uwezo wa kufufua na kuondosha mtu kwa maana ya kufa ni Mwenyezi Mungu Subhana Wataalah. Nakushukuru. (Makofi)