Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaunga mkono juhudi za wananchi katika ujenzi wa Zahanati na Vituo vya Afya Kata za Arumeru Mashariki?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu ya Serikali, lakini bado niseme kwamba Arumeru Mashariki kuna shida nyingi sana hususan katika sekta ya afya. Wananchi wanahangaika sana kujijengea zahanati wenyewe, mimi mwenyewe tangu nianze harakati za kurudisha jimbo kwenye jengo, nimezunguka kwenye jimbo kushoto, kulia, kusini, magharibi, kaskazini kuhakikisha kwamba, wananchi wanajua kwamba tunahangaika nao.

Mheshimiwa Naibu Spika, utakubaliana nami kwamba Wabunge hatupitwi na changizo lolote jimboni, kwa hiyo, kila zanahati inayojengwa kila kituo cha afya kinachojengwa Mbunge anahusika.

NAIBU SPIKA: Uliza swali Mheshimiwa.

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Naibu Spika, swali, je, ni lini Serikali itaingilia kati ujenzi wa Zahanati iliyoko Katiti, Zahanati ya Kolila, Zahanati ya Zengon, Zahanati ya Majengo na sehemu nyingine nyingi jimboni. (Makofi)

Pili, je, Waziri yuko tayari kuambatana na mimi baada ya Kikao hiki cha Bajeti tukakague aone ninalolizungumza hapa kama ni la kweli au la? Nakushukuru sana. (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza ambalo Mheshimiwa Mbunge amejaribu kulieleza ili Serikali iweze kutoa ufafanuzi, ni kwa namna gani Serikali inatoa mchango katika maeneo ambayo wananchi wamekuwa wakianzisha ujenzi, hususan wa maboma ya afya; na ameainisha baadhi ya maeneo ikiwemo Kikatiti, Kolila na maeneo mengineyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwa kuzingatia hilo, ndiyo maana Serikali katika mwaka huu wa fedha tumeamua kutenga shilingi milioni 150 mpaka 200 kwenye kila jimbo ili kwenda kusaidia kumalizia zahanati ambazo zimeanzishwa na wananchi. Kwa hiyo, tutaendelea kufanya hivyo kulingana na fedha tunazopata na tutaendelea kuzingatia mchango mkubwa ambao unatolewa na wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali dogo la pili la nyongeza lilikuwa, kama niko tayari kuongozana naye Mheshimiwa Mbunge; nimhakikishie, nipo tayari na nitaifanya hiyo kazi kwa uaminifu mkubwa. Ahsante. (Makofi)