Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Primary Question

MHE. OSCAR I. KIKOYO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza utekelezaji wa Mradi wa Maji wa Katerela kwa ajili ya Kata za Kasharunga na Rulanda?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO: Mheshimiwa Naibu Spika, Nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Lakini ninalo swali moja tu la nyongeza. Kutokana na uhaba mkubwa wa maji katika Wilaya ya Muleba na jiografia ya Wilaya ya Muleba inapakana na Ziwa Victoria. Serikali inao mpango wowote wa kutumia Ziwa Victoria kuvuta maji kwa ajili ya Wilaya ya Muleba? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mhehsmiwa Naibu Spika, Mradi wa Ziwa Victoria ni mradi wa kimkakati na ni mradi ambao tunautarajia uhudumie maeneo mengi sana kwasababu ni mradi unaopita katika majimbo mengi na mikoa mbalimbali. Hivyo niweze kumwambia Mhehimiwa Mbunge kwamba maeneo yake ambayo bomba hili kubwa litakuwa likipita basi na yeye atanufaika katika vijiji vile ambavyo viko kilometa 12 kutoka kwenye bomba kwa pande zote kulia na kushoto.

Name

Felista Deogratius Njau

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. OSCAR I. KIKOYO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza utekelezaji wa Mradi wa Maji wa Katerela kwa ajili ya Kata za Kasharunga na Rulanda?

Supplementary Question 2

MHE. FELISTA D. NJAU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, nilikuwa nataka niiulize Serikali ni lini itamaliza kero ya maji ambayo imekuwa ni sugu katika Kata ya Wazo, Mitaa ya Nyakasangwe, Mitaa ya Salasala na Mivumoni Kata ya Mbezi Mtoni, Sakuveda na Mabwepande Mtaa wa Mbopo?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara kupitia DAWASA wanafanya kazi nzuri sana maeneo yote ambayo Mheshimiwa Mbunge ameyataja. Na tayari mikakati kabambe inaendelea na kufikia mwaka ujao wa fedha maeneo mengi sana ya maeneo hayo yote uliyoyataja Mheshimiwa Mbunge yatakuwa yamefikiwa na maji bombani.