Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza:- (a) Je, ni matukio mangapi ya moto yametokea kwenye Shule na masoko katika kipindi cha miaka mitano iliyopita? (b) Je, uchunguzi uliofanyika ulibaini vyanzo vya moto huo ni nini?

Supplementary Question 1

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nina maswali mawili ya nyongeza, swali la kwanza; kwa kuwa katika majibu yake ya msingi ameeleza wazi kwamba, Zimamoto huwa wanahusika sana katika kutuliza moto huo endapo majanga yanatokea. Hata hivyo, sio siri mara nyingi Jeshi hilo likifika linakuta magari hayana maji au wamechelewa sasa swali langu kwa Serikali, imejipangaje kuimarisha Jeshi hilo la Zimamoto ili wawe more efficient? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, mioto hiyo ipo katika maeneo yetu tunayoishi au vijijini au kwenye kata zetu au mitaa yetu, lakini wananchi hao nikiweko mimi hatujapatiwa mafunzo ya kutosha kwenye kuzima mioto mikubwa kama hiyo. Wengi ni waathirika wa maeneo hayo na sitaki kurudi nyuma kukumbusha vilio vya Shauritanga na mashule mengine ambayo sitaki kutaja ikaja kuharibu sifa za shule hizo kupata wanafunzi. Je. Serikali itatoa lini mafunzo na kwa msisitizo kabisa ili watu hawa wapate elimu ya kusaidia kuzima mioto hiyo? (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nachukua fursa hii kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Shally Raymond, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza ameuliza, je, ni nini sasa Serikali inafanya au hatua ambazo inazichukua katika kuhakikisha kwamba inapunguza haya majanga ya moto ambayo yanajitokeza mara kwa mara? Ziko hatua nyingi ambazo kama Serikali tumezichukua ili kuona namna ambavyo tunapunguza, hatuwezi kuondosha moja kwa moja kwa sababu, mengine yanakuja, lakini tunapunguza. La kwanza, ni kuendelea kutoa elimu ama kuendelea kutoa taaluma kwa jamii, kwa sababu tunaamini jamii ikipata taaluma ama ikishiba taaluma ya kutosha majanga haya yatapungua.

Mheshimiwa Naibu Spika, kingine tunaendeleza ukaguzi wa majengo. Yapo majengo lazima tuyakague kwanza, yako majengo ya binafsi, yako majengo ya Serikali na yako majengo mengine. Kwa hiyo, tunakuwa tunafanya ukaguzi wa kwenye majengo ili kuona namna ambavyo tunawaelimisha namna ya kujikinga na haya majanga ya moto. Kikubwa zaidi tunao mpango na tumeshaanza, wa kuongeza visima vya dharura kitaalam tunaviita fire hydrants ili ikitokezea taharuki kama ya moto tuwe tuna maeneo ya kuweza kuchota maji na kuweza kuokoa maisha ya watu.

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ni kwamba Je. taaluma huko vijijini inafikaje? Tunavyo vitu vingi ambavyo tumeviandaa ambavyo vinaendelea kutoa taaluma, tunazo zile fire clubs ambazo ziko huko vijijini kwenye kata kwenye vijiji, kwenye shehia ambazo zinaendeleza kutoa taaluma kwa watu. Pia hivi karibuni nimewahi kusema sana tu, hivi karibuni tulifanya makubaliano na watu wale wa skauti ambao wengi wao ni wanafunzi na wako vijijini huko ambao wanafanya kazi kubwa ya kuendelea kutoa taaluma na kuelimisha jamii namna bora ya kujikinga na haya majanga. Vile vile kuelimisha jamii namna bora ya kutoa taarifa mapema kwa sababu changamoto inakuja kwenye utoaji wa taarifa. Nakushukuru sana.

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza:- (a) Je, ni matukio mangapi ya moto yametokea kwenye Shule na masoko katika kipindi cha miaka mitano iliyopita? (b) Je, uchunguzi uliofanyika ulibaini vyanzo vya moto huo ni nini?

Supplementary Question 2

MHE. MAIMUNA S. MTANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kuuliza swali la nyongeza; kwanza nishukuru kwa majibu ya Serikali, lakini nataka kujua namna ambavyo Wizara ya Mambo ya Ndani inashirikiana na Wizara ya TAMISEMI wenye shule kuhakikisha kwamba matukio haya sasa yanakoma kwa sababu, yamekuwa yakisumbua mara kwa mara katika shule zetu hasa za mabweni. Ahsante. (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimtoe hofu tu Mheshimiwa Mbunge kwamba, tunao ushirikiano wa karibu baina ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi na TAMISEMI na hata hawa watu wa Wizara ya Elimu katika kuhakikisha kwamba tunapunguza idadi kubwa ya majanga ya moto na majanga mengine hasa katika maeneo ya shule na maeneo mengine. Tayari tumeshakuwa tunakaa vikao mbalimbali, tumeshapanga mipango mbalimbali ambayo ni mikakati ya kuhakikisha kwamba tunapunguza haya majanga.

Kwa hiyo, hilo Mheshimiwa asiwe na wasiwasi juhudi zinaendelea kazi inaendelea na tutahakikisha kwamba tunapunguza haya majanga kwa kiasi kikubwa. Nakushukuru.