Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. MOHAMED L. MONNI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Handeni- Kiberashi-Kiteto – Mrijo – Chemba – Kwa mtoro hadi Singida kwa kiwango cha lami kwa kuwa ipo kwenye Ilani na pia Ahadi ya Mheshimiwa Rais?

Supplementary Question 1

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Naibu Spika, swali hili limeulizwa mara mbili kwa mujibu wa Taarifa mbalimbali kutoka Bunge lako majibu yamekua ya kitolewa hayo hayo, sasa naomba kujua hata hizo bilioni 6 ambazo zimetengwa kwa ajili ya mwaka unaoishia mwenzi mmoja ujao hazijawahi kutumika mpaka leo. Naomba kujua lini sasa hizi bilioni 6 sasa zinaanza kufanya ujenzi kwenye barabara ile.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili ni nini commitment ya Serikali kwa ajili ya ujenzi wa barabara hiyo kwasababu Mheshimiwa Rais alipokuja kwenye ziara ya kuomba kura aliahidi itajengwa kwa kiwango cha lami, naomba kujua…

NAIBU SPIKA: umeshauliza Mheshimiwa, ahsante sana.

Name

Eng. Dr. Leonard Madaraka Chamuriho

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza napenda kumshukuru Mbunge kwa jinsi ambavyo ifuatilia barabara hii barabara ndefu na kweli ni kiunganishi cha mikoa tangu Singida hadi Tanga na imepangiwa katika bajeti bilioni 6.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kumuahidi Mbunge huyu kwamba kabla ya bajeti hii kwisha barabara hii itatangazwa katika kipande ambacho kimepangiwa kilomita 20. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.

Name

Miraji Jumanne Mtaturu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mashariki

Primary Question

MHE. MOHAMED L. MONNI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Handeni- Kiberashi-Kiteto – Mrijo – Chemba – Kwa mtoro hadi Singida kwa kiwango cha lami kwa kuwa ipo kwenye Ilani na pia Ahadi ya Mheshimiwa Rais?

Supplementary Question 2

MHE. MIRAJI J. MTATURU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana barabara hii tuna maslahi nayo kama alivyojibu swali Mheshimiwa Naibu Waziri na kwa sababu barabara hii inaunganisha mikoa minne na barabara hii inahistoria katika nchi yetu imefika wakati sasa Serikali iamuwe kuijenga barabara hii kilometa 461 iishe kuliko kuanza kuwa na vipande vidogo vidogo.

Name

Eng. Dr. Leonard Madaraka Chamuriho

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii ina Wabunge wengi ambao wanaifuatilia sana na ninawashukuru sana kwa kuweza kuwa wanatukumbusha kila mara umuhimu wa barabara hii. Lakini kama alivyosema Mbunge barabara hii inaurefu wa kilometa 460 na tunaendelea kujenga kwa vipande kulingana na upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka huu unaoendelea kama nilivyosema katika swali lilipita tutajenga kipande kimoja na katika bajeti hii ambayo tuna ijadili mwaka huu barabara hiyo vilevile imezingatiwa kwa hiyo napenda kuwaahidi wananchi tangu mikoa ya Singida hadi Tanga ambayo barabara hiyo inapita kwamba vipande vinaendelea kujengwa na barabara hiyo tutaizingatia kulingana na upatikanaji wa fedha.