Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA - K.n.y. MHE. SALIM A. HASHAM aliuliza:- (a) Je, Serikali ina mpango gani kutengeneza barabara za Ulanga na kutenga bajeti ya dharura ili TARURA iweze kukarabati barabara mara tu zinapoharibika? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuipatia TARURA ya Halmashauri Ulanga usafiri ili kuongeza ufanisi katika kazi zao?

Supplementary Question 1

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA: Mheshimiwa Naibu Spika, naishukuru Serikali kwa majibu mazuri, na kwa niaba ya Mbunge wa Ulanga Mheshimiwa Salim, naomba kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza kama ifutavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa lazima ukitaka kwenda Ulanga upite Jimbo la Kilombero na kwa kuwa Wilaya ya Malinyi, Ulanga, Jimbo la Mlimba na Jimbo la Kilombero ni ukanda mmoja.

Mheshimiwa Naibu Spika, je, Mheshimiwa Waziri haoni kwamba ni muhimu kuwa na timu ya dharura ya TARURA ikaenda kwenye eneo hilo kwa sababu Wilaya ya Kilombero, Jimbo la Mlimba, Ulanga na Malinyi hakuendeki?

Mheshimiwa Naibu Spika, pili: Je, Mheshimiwa Waziri pia haoni kwa udharura huo akatafuta haraka iwezekanavyo gari la kuwapelekea wananchi wa Wilaya ya Ulanga kwa maana ya timu ya TARURA ikapata gari la dharura wakati huu wa mvua ambapo njia hazipitiki? Ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Jambo la kwanza ameiomba Serikali kupeleka timu ya dharura kwa ajili ya kwenda kupitia zile barabara ambazo zimebadilika na kufanya tathmini. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, hivi ninavyozungumza sasa hivi kuna timu zipo huko kwa ajili ya kuangalia zile barabara zote mbovu ambazo zilipitiwa na hili janga la mvua yakiwemo maeneo ya kule Malinyi. Kwa hiyo, watu wapo kazini na hiyo timu inaendelea.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu katika Bunge hili wengi huwa wanatusikiliza sasa hivi, ninaagiza wapitie tena upya waangalie hiyo tathmini ya barabara ya Kilombero kupitia Ulanga inafanyiwa kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili ameomba kwamba tuwe na gari la dharura kwa ajili ya Ulanga. Kama nilivyoeleza katika jibu la msingi kwamba, tumeshatengewa fedha na katika hizo fedha tutanunua magari 30 na miongoni mwa maeneo ambayo tumeyapa kipaumbele, tutapeleka gari kwa ajili ya TARURA ni katika Jimbo la Ulanga. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshmiwa Mbunge, Ulanga watapata hilo gari.

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA - K.n.y. MHE. SALIM A. HASHAM aliuliza:- (a) Je, Serikali ina mpango gani kutengeneza barabara za Ulanga na kutenga bajeti ya dharura ili TARURA iweze kukarabati barabara mara tu zinapoharibika? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuipatia TARURA ya Halmashauri Ulanga usafiri ili kuongeza ufanisi katika kazi zao?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi. Barabara za Ulanga ni sawa sawa na barabara za Mlimba:-

Je, ni lini barabara ya kutoka Mlimba Mjini mpaka Tanganyika Masagati ambayo inatengenezwa na TARURA itaweza kukarabatiwa na kutengenezwa kwa sababu kutokana na mvua ni mbaya sana kiasi cha kuleta taabu ya kupitika? Ahsante sana. (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Mheshimiwa Mbunge anauliza ni lini barabara ya kutoka Mlimba kwenda Tanganyika Msagati itajengwa kwa sababu ipo katika hali mbaya?

Mheshimiwa Naibu spika, nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali tumelipokea ombi lake na Ofisi ya TARURA watafanya tathmini na watatafuta fedha kwa ajili ya matengenezo ya eneo hilo. Ahsante sana. (Makofi)