Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika vijiji 127 vilivyobaki vya Mkoa wa Songwe?

Supplementary Question 1

MHE. JULIANA D. SHONZA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini vilevile kwa commitment ambayo ameitoa kwa wananchi wa Mkoa wa Songwe. Nataka nitoe tu ushauri kwamba katika kutekeleza mkakati huo, wasisahau taasisi muhimu, hususan shule za boarding, kwa sababu katika Mkoa wa Songwe, shule nyingi sana za boarding zinakabiliwa na changamoto ya kutokuwepo kwa umeme. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba niulize swali langu moja la nyongeza. Utakubaliana nami kwamba upatikanaji wa umeme wa uhakika ni aspect muhimu sana katika kukuza uchumi wa eneo husika; nasi wananchi wa Mkoa wa Songwe tunakabiliwa na changamoto kubwa sana ya kukatika katika kwa umeme mara kwa mara; na hii imekuwa ni changamoto kubwa hususan katika ile miji mikubwa ya kibiashara kwa maana ya Miji ya Mlowo, Tunduma kule kwa Mheshimiwa David Silinde na Vwawa:- (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nataka kujua kwamba je, Mheshimiwa Waziri atakuwa tayari kwenda ama kutuma wataalam wake katika Mkoa wa Songwe ili kuweza kubaini changamoto hiyo na kuipatia ufumbuzi? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, kwanza napenda nimpongeze sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri katika swali la msingi la Mheshimiwa Shonza. Kwanza, ni kweli zipo taasisi nyingi ambazo kimsingi zinahitaji kupatiwa umeme, hasa huu wa Programu ya REA; na tumeainisha taasisi zote zikiwemo shule za msingi, sekondari na vituo vya afya, na tumetoa maelekezo kwa wakandarasi kuzingatia kipaumbele cha kupeleka umeme kwenye taasisi za Umma kama kipaumbele. Kwa hiyo, naomba nitoe msisitizo kwa wakandarasi kuzingatia hilo. Pili, nawaomba Wakurugenzi na Wenyeviti wa Halmashauri kutenga fedha kidogo angalau kulipia kupelekea taasisi za Umma umeme. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, katika swali la pili ambalo ni la uimara wa umeme katika Mkoa wa Songwe. Nampongeza sana Mheshimiwa Shonza na Wabunge wa Songwe kwa ujumla kwa kufuatilia masuala ya umeme katika mkoa wao. Ni kweli Mkoa wa Songwe unapata umeme kutoka Iyunga iliyoko Mbeya, na ni takribani kilometa 70 kutoka kwenye kituo cha kupoozea umeme.

Mheshimiwa Spika, tumechukua hatua mbili madhubuti, na niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge na wananchi wa Songwe kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, hatua ya kwanza, tumejenga njia ya kusafirisha umeme kwa dharura kwa kuepusha kukatika kwa umeme katika Mkoa mzima wa Songwe kwa kujenga laini ya kilometa 70 kutoka Iyunga mpaka Mlowo; na tumeanza hivyo toka Januari na mradi unakamilika Mei mwaka 2021. Tumetenga shilingi bilioni 2.4 ambazo ni fedha za ndani.

Mheshimiwa Spika, maeneo yatakayopelekewa umeme ni Mlowo, Tunduma, Vwawa yenyewe pamoja na Momba; na tutagawa laini specific kwa kazi hiyo. Kwa hiyo, kuazia mwezi Mei mwaka huu, maeneo ya Songwe yatapata umeme wa uhakika. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika vijiji 127 vilivyobaki vya Mkoa wa Songwe?

Supplementary Question 2

MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi. Tatizo ambalo lipo katika Mkoa wa Songwe linafanana kabisa na tatizo ambalo liko katika Mkoa wa Dar es Salaam kwenye baadhi ya maeneo, na hasa katika Jimbo la Ukonga kwenye baadhi ya Mitaa ya Kata za Msongola, Chanika, Zingiziwa na Buyuni:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inasema nini kwa habari ya kuhakikisha kwamba Mkoa wa Dar es Salaam unapata umeme?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Dar es Salaam una mahitaji makubwa sana ya umeme, ingawa Dar es Salaam tuna jumla ya Megawati 572 zinazotumika kwa Dar es Salaam, lakini mahitaji yanaongezeka kila leo. Tumejenga dedicated line ya kutoka Kinyerezi kupita Gongo la Mboto kwenda mpaka Ukonga – Pugu mpaka Dondwe kule Chanika Zingiziwa kwa ajili ya kupelekea umeme wananchi wa huko.

Mheshimiwa Spika, tumewapatia mkandarasi wa peri-urban atakayepeleka umeme katika maeneo ya Bomba Mbili, Majohe, Mvuti, Songambele pamoja na Zingiziwa mpaka Kisasa, mpaka Magerezani kule Dondwe ndani. Kwa hiyo, wananchi wa Dar es Salaam watapata umeme, na ni ndani ya miezi sita utaratibu utakamilika na wananchi kupata umeme wa uhakika.