Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ravia Idarus Faina

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Makunduchi

Primary Question

MHE: RAVIA IDARUS FAINA aliuliza: - Je, Kwa nini Vyama vya Michezo ikiwemo TFF na TOC vimekuwa vikibadili Katiba zao kwa lengo la kulinda viongozi waliopo madarakani na kudhibiti watanzania wengine wasigombee nafasi katika vyama hivyo?

Supplementary Question 1

MHE. RAVIA IDARUS FAINA: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri lakini kwenye TFF ukomo wa uongozi ni vipindi vitatu vya miaka minne minne. Lakini, kwenye TOC hakuna ukomo. Je. haoni inazuia uhuru wa watu wengine kugombea? (Makofi)

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Spika, kwa upande wa TFF wao wamekwenda vizuri kama alivyosema lakini TOC wanaendelea kufanya marekebisho katika katiba yao. Katiba yao Mwaka 2019 walirekebisha, 2020 msajili aliweza kuipitisha Novemba na katika marekebisho ambayo amefanya sasa, wameweka kipengele cha kwamba, mtu akigombea nafasi ya Urais basi ahudumu kwa term 3 akishahudumu kwa term 3 ya miaka minne minne ya miaka 12, baada ya hapo asirudie kugombea nafasi hiyo bali sasa apande juu aende IOC au kwenye nafasi zingine. Kwa hiyo, wameendelea kuboresha vile vipengele ambavyo vinaminya uhuru wa watu wengine na wengine kuendelea kugombea. Ahsante.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE: RAVIA IDARUS FAINA aliuliza: - Je, Kwa nini Vyama vya Michezo ikiwemo TFF na TOC vimekuwa vikibadili Katiba zao kwa lengo la kulinda viongozi waliopo madarakani na kudhibiti watanzania wengine wasigombee nafasi katika vyama hivyo?

Supplementary Question 2

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kama ilivyo kwa Chama cha TFF kwenye eneo la ngumi kumekuwa na ubabaishaji mwingi sana kwa kitu kinachoitwa Rais wa ngumi.

Je, Serikali ina mpango gani wa kusimamia uongozi huu unaokaa kwa muda mrefu bila kufuata katiba kama inavyosema? Ahsante kwa kunipa hiyo nafasi. (Makofi)

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Spika, sisi kama Wizara kupitia BMT lakini kupitia kwa Msajili, tunaendelea kufuatilia hizi katiba ambazo wamechomeka vipengele ambavyo vinawafanya watu kuendelea kukaa madarakani. Mheshimiwa Mwakagenda suala lako tunalipokea na pia nitafanya ziara katika maeneo hayo na tutapitia katiba yao pia kwa upya tuone ni wapi wameweka vipengele hivyo. Nikuhakikishie kupitia msajili tutaangalia na tutashauri lakini pia wanachama, mtushauri pale ambako mnaona hizi katiba zinakandamiza uhuru wenu katika vyombo hivyo ambavyo mnashiriki vya kimichezo. Tuko tayari kupokea ushauri wenu.